Kipindi cha Covid-19 ilipunguza magonjwa ya milipuko kama kipindupindu, red-eyes na typhoid sababu ya kila sehemu kulikuwa na ndoo za kunawa mikono

Kaka yake shetani

JF-Expert Member
Feb 1, 2023
3,604
8,733
Ugonjwa wa covid19 ulipoingia tulijaribu kuweka mbinu nyingi kila mtu kujua atajisaidia vipi ili kujiokoa na gonjwa ili sitosahau mpaka malimau yakapanda bei.

Serikali ikaweka mpango maalumu wa kila sehemu kuhakikisha kuna ndo ya maji safi na kila sehemu utakapo kwenda kunawa mikono kabla ya kuingia.

Kwa kiasi kikubwa ilipunguza magonjwa mengi sehemu nyingi kama kipindupindu na mengine ila tokea ugonjwa huu kuto kuwekewa umakini tena watu wamerudi kwenye tabia zao za kutozingatia usafi wa mikono ndio maana ni rahisi kusambaa magonjwa haya ambayo tuliyasahau.

Swala la kunawa mikono liwe lazima ili kupunguza magonjwa.
 
Back
Top Bottom