Wabunge wa CCM Tusiyumbe.
Nimeanza kwa Wabunge wa CCM kwa sababu kubwa kwanza sisi chama chetu ndicho kilicho na dhamana ya kuwaongoza watu wa nchi hii.
Lobbing zimeanza za Makampuni makubwa ya Migodi kupinga sheria ya Fao la kujitoa.makampuni binafsi nayo yataanza soon kupinga uamuzi huu kwa maslahi ya wachache Maslahi yasiyozingatia maono ya nchi na Usalama wa Taifa.Maslahi yanayoangalia siasa za muda za kuwafurahisha wanaharakati huku taifa likikosa nguvu ya kiuchumi.
Nawatahadharisha wabunge wote na hasa wa Chama changu CCM,tuwe makini na kila move hasa kipindi hiki ambacho Rais Magufuli amekuja na mwanga juu ya hatma ya viwanda vya nchi hii;Magufuli ameamua nchi iwe ya viwanda kupitia Mifuko hii ya kijamii,Lakini naona mapandikizo yakutaka kuidhoofisha mifuko hii,Mipango hii wanajua wanaoiratibu nia yao lakini wabunge wenzangu na wana CCM fao lakujitoa ni miongoni mwa mipango ovu ya kutaka kumdhoofisha Rais Magufuli na kudhoofisha mapato ya mifuko hii iliyoelekezwa kusimamia mageuzi ya viwanda nchini.
Kwanini watanzania kila jambo tuliwekee siasa?Uimara wa mifuko.ya kijamii popote duniani ndio kiini cha Usalama wa Taifa,Usalama.wa nchi katika kila nyanja iwe ya dharura za kiulinzi au kukuza uchumi hii ni roho ya nchi hasa nchi Hizi zinazoendelea.
Tuwe makini sana juu ya hawa wanaotaka kuturudisha nyuma.Rais anadira ya viwanda,Mifuko hii imepewa jukumu hili kwanini tuanze kutaka kuwadhoofisha.Kwa haraka haraka NSSF wanaweza kuokoa karibu biln 60 pesa ambazo kwa nchi changa kama hii zikiwekezwa kwa busara na uzalendo zinalifanya taifa lipae kiuchumi.
Watanzania tuache siasa pesa hizi ni za watanzania wakifikisha umri unaostahili watalipwa nchi hii lazima itangulize maslahi ya wengi kwa faida ya vizazi,tuache harakati na siasa za kutaka sifa kwa mambo mazito yanayogusa ustawi na usalama wa nchi.
Tuache mifuko ikusanye pesa a kuwekeza kwenye viwanda .Tuache ubinafsi kwa faida ya vizazi vinavyokuja.
Kingu Elibariki
MP Singida West
Wadau, Mimi huwa nashangaa kwanini huwa tunawachagua mazombie kama hawa kuwa wawakilishi wetu bungeni, Poleni wana singida magharibi,
Hivi jitu Zima halioni hata aibu kusema eti wana mpango wa kujenga viwanda kwa kutegemea hela za mifuko ya hifadhi za jamii !!
Hizo hela ni za wanachama wa mifuko na si za serikali, hata mifuko yenyewe huwa inafanya makosa kuzitumia kwenye uwekezaji bila kuwa shirikisha wenye hela zao, mwisho wa siku mifuko ndio inayopata faida halafu mwanachama anapewa 1% Interest kwa mwaka,
Hao wabunge wao hufanya kazi miaka mitano wakimaliza wanapewa mafao yao, ambayo huwa hayakatwi kodi (Tax free)
Kwa nini wao wabunge wasichangie hizo hela waisaidie serikali kujenga hivyo viwanda,
Kwa nini watake hela za wafanyakazi ni si zao zikajenge viwanda ?
Hizo hela kwenye mifuko ya hifadhi zinatumika vibaya sana, Inafikia hatua mifuko ya hifadhi za jamii wanawakopesha mabenki hela za wanachama kwa riba ya asilimia chini ya 10 halafu mabenki wanakuja kuwakopesha wafanykazi kwa riba ya asilimia 18 mpaka 23
Unamwambia mfanyakazi asubiri afikishe miaka 60 ndio apate mafao yake na wakati serikali inakiri kwamba wastani wa umri wa watanzania ni miaka 45 !!
Lengo lao huwa sio zuri, wanajua wazi ukifikisha umri huo wa miaka 60 utakuwa umehoka vya kutosha huwezi kuwafuatilia kwa karibu na utakuwa umekaribia sana kufa,
Hizi kazi jamani zinatofautiana sana, kuna watu walikuwa wanafanya kazi migodini, mtu anapoteza ajira yake akiwa na miaka 35 kwa mfano kisha unamtaka asubiri miaka 25 ndio apate mafao yake !!
Hivyo viwanda tuliambiwa mmeshajenga 3000 naamini vinawatosha,
Achieni hizo hela za mafao ya wanaume wakazifanyie wanachotaka wao, hamkuwasaidia kuzichanga