Buldoza
JF-Expert Member
- May 2, 2013
- 2,307
- 987
Wewe ni mwongo mkubwa. Julius Nyerere hakuwa anatibiwa Uingereza, na hakuwahi kulazwa hospitali yoyote ile iwe ndani ya nchi au nje ya nchi ukiacha huo ugonjwa uliochukua maisha yake. Ukumbuke pia hata kwenye ugonjwa huo uliochukua maisha yake, Nyerere alikuwa hataki kabisa kwenda Uingereza, jambo lililowafanya viongozi kadhaa kumsihi na kumbembeleza sana ili akubali. Waulize wote waliokuwa karibu naye watakuambia namna Mwalimu ambavyo hakuridhika kabisa na uamuzi wa serikali wa kumpeleka Uingereza.
Nyerere hakuwa kama akina Kikwete ambao kila wakipata mafua tu wanaenda USA.
Si kweli. Wakianguka kifafa huwa tunawapeleka kwa "fundi" zao bwagamoyoooo!!!!!!!