G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,881
Wakati Membe akitamba kuwa alienda mbele ya kamati ya maadili ya CCM kuwafunda na kuwaelimisha kuhusu mambo mbalimbali, Kinana amegoma kufika mbele ya kamati hiyo.
Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika, Kinana ameona ni kama kudharauliwa kwa kuitwa kuhojiwa mambo ambayo kimsingi ni malalamiko aliyotoa kuhusu namna alivyokuwa akipakwa matope na mtu anayejiita Cyprian Musiba. Inaelezwa kuwa aliyetakiwa kuitwa ni Musiba na siyo Kinana.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi ndani ya chama, Kinana jana ijumaa alitakiwa kuwepo mbele ya kamati hiyo ya maadili lakini alisubiriwa hadi jioni na hakuna taarifa yoyote rasmi iliyopatikana juu ya kutokuhudhuria kwake mbele ya kamati hiyo.
Aidha hakutuma ujumbe wowote wa udhuru kuelezea kuhusu yeye kushindwa kufika mbele ya kamati hiyo kama ilivyopangwa.
Tusubiri tuone.
Kwa mujibu wa chanzo cha kuaminika, Kinana ameona ni kama kudharauliwa kwa kuitwa kuhojiwa mambo ambayo kimsingi ni malalamiko aliyotoa kuhusu namna alivyokuwa akipakwa matope na mtu anayejiita Cyprian Musiba. Inaelezwa kuwa aliyetakiwa kuitwa ni Musiba na siyo Kinana.
Kwa mujibu wa taarifa rasmi ndani ya chama, Kinana jana ijumaa alitakiwa kuwepo mbele ya kamati hiyo ya maadili lakini alisubiriwa hadi jioni na hakuna taarifa yoyote rasmi iliyopatikana juu ya kutokuhudhuria kwake mbele ya kamati hiyo.
Aidha hakutuma ujumbe wowote wa udhuru kuelezea kuhusu yeye kushindwa kufika mbele ya kamati hiyo kama ilivyopangwa.
Tusubiri tuone.