Mkutano wa Kuwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya CCM Jimbo la Hai

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,897
942
Mbunge wa Jimbo la Hai, Mhe. Saashisha Mafuwe tarehe 05 Septemba, 2023 katika Mkutano Mkuu wa Jimbo la Hai Aliwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya CCM ambapo Mgeni rasmi alikuwa ni Makamu Mwenyekiti wa (CCM) Bara Ndugu Abdulrahman Kinana

Mkutano Mkuu Maalum wa Jimbo la Hai ulilenga sana kwa Mbunge wa Jimbo la Hai, Mhe. Saashisha Mafuwe kusoma Utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Jimbo la Hai ambao ulihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Chama, Serikali na Wabunge.

MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Ndugu Abdulrahman Kinana, ameziagiza kamati za siasa za CCM, kuwafuatilia na kuwachukulia hatua wanachama walioanza kupitapita kusaka ubunge na udiwani.

"Nataka nitumie fursa hii kuziagiza kamati za siasa za CCM nchi nzima, zikisaidiwa na kamati za maadili nchi nzima, kuwafuatilia wale ambao wameanza kuzungukazunguka kutafuta ubunge, udiwani, uenyekiti wa mtaa au kitongoji kuanzia sasa" - MAKAMU Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Tanzania Bara, Ndugu Abdulrahman Kinana

Katika Mkutano huo, Mhe. Saashisha Mafuwe alipata nafasi ya kuwasilisha mbele ya Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Jimbo la Hai miradi mbalimbali ya Elimu, Afya, Miundombinu, Uchumi iliyotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan

Mhe. Saashisha Mafuwe amemshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumpa maneno mengi ya kusema kwa kupitia miradi ya maendeleo aliyoipeleka ndani ya Jimbo la Hai.

Aidha, Mhe. Saashisha Mafuwe amemshukuru Ndugu Abdulrahmani Kinana, Makamu Mwenyekiti Tanzania Bara kwa kukubali kuwa mgeni rasmi tarehe 05.09.2023 kwenye Mkutano Maalum Mkuu CCM wa Wilaya ya Hai wa kuwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM.

Vilevile, Mhe. Saashisha Mafuwe amewashukuru sana Kamati ya Siasa Wilaya ya Hai kwa maandalizi, Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Wilaya, Viongozi wa Dini na Mila, Viongozi wa Mila kwa Daraja la Umangi waliomvalisha ngozi ya Mbelele.

WhatsApp Image 2023-09-07 at 01.46.00(1).jpeg
WhatsApp Image 2023-09-06 at 00.02.12.jpeg
WhatsApp Image 2023-09-06 at 00.02.07(2).jpeg
WhatsApp Image 2023-09-06 at 00.01.45.jpeg
WhatsApp Image 2023-09-06 at 00.02.11.jpeg
 
Mbunge wa Jimbo la Hai, Mhe. Saashisha Mafuwe tarehe 05 Septemba, 2023 katika Mkutano Mkuu wa Jimbo la Hai Aliwasilisha Taarifa ya Utekelezaji wa Ilani ya CCM ambapo Mgeni rasmi alikuwa ni Makamu Mwenyekiti wa (CCM) Bara Ndugu Abdulrahman Kinana
Kiukweli japo Mbunge wa Jimbo la Hai, Mhe. Saashisha Mafuwe amejitahidi sana kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM, but it's very unfortunately jimbo la Hai ni miongoni mwa majimbo ya maridhiano, limeingizwa kwenye mgao wa nusu mkate!. Hivyo 2025 linarejeshwa kwa mwenyewe mwenye jimbo lake lililopokwa ile 2020!.
p
 
Kiukweli japo Mbunge wa Jimbo la Hai, Mhe. Saashisha Mafuwe amejitahidi sana kutekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM, but it's very unfortunately jimbo la Hai ni miongoni mwa majimbo ya maridhiano, limeingizwa kwenye mgao wa nusu mkate!. Hivyo 2025 linarejeshwa kwa mwenyewe mwenye jimbo lake lililopokwa ile 2020!.
p
Mkuu Mayala ..ndio maana kwa kulitambua hilo, Mhe sana Saashisha kaamua kumualika Makamu Mwenyekiti WA Chama Taifa kuja kushuhudia tukio hilo ambapo kimkakati ni sawa na kujiwekea mazingira mazuri kichama
 
Mkuu Mayala ..ndio maana kwa kulitambua hilo, Mhe sana Saashisha kaamua kumualika Makamu Mwenyekiti WA Chama Taifa kuja kushuhudia tukio hilo ambapo kimkakati ni sawa na kujiwekea mazingira mazuri kichama
Ni kweli, japo anayeingia kwenye kikao cha mgao wa kugawana nusu mkate ni yeye huyo huyo!. Unless maridhiano yavunjike lakini 2025 jimbo la Hai, linarekeshwa kwa mwenyewe mwenye jimbo lake!.
P
 
Ni kweli, japo anayeingia kwenye kikao cha mgao wa kugawana nusu mkate ni yeye huyo huyo!. Unless maridhiano yavunjike lakini 2025 jimbo la Hai, linarekeshwa kwa mwenyewe mwenye jimbo lake!.
P
Kwani kwa nyundo na makelele ambayo mwenye jimbo lake unayemtaja anayafanya kupitia majukwa ya kisiasa si ni kiashiria Cha mambo hayako tena sawa sawa kama walivyoridhiana!? Au ndio kusema kwamba hayo makelele na nyundo anazopigwa mwenye nchi ni sehemu ya maridhiani kimkakati!?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom