Kinadada acheni kumsumbua Mungu

Kinadada acheni kumsumbua Mungu

Haya bwana Msumbuenii....msumbuenii...!

Aimeeen bwana shemeji

Ashindwe mara ngapi sasa, ashashindwa kitambo. Tumeshamkemea vya kutosha. Sasa hivi ni maombi ya kushukuru na kukiri tu ushindi. Baba tunasema Ahsante kwa sababu umesema "yote yalikwisha pale msalabani"

Yani huwa najisikia raha after praying, ni kama Umetua zigo la michongoma. Daah Acheni Mungu aitwe Mungu


Aimeeeen!! They better find another job maana kwa hili mission impossible!! Wamfikishie tu salamu bwana lucifer.
 
Wanakera sana hasa ukiwa unakumbuka matusi yao kabla hawajazaa
 
Na tuwakumbuke katika maombi sana, maana kwa uzi huu nimegundua hawa vijana wetu wa kiume we realy need to pray very hard for them, they have a long way to man up, so tuzidi kupiga maombi.

#hapamaombitu
Itabidi wote tu tuungane katika maombi. Maombi ya mapatano yana nguvu sana honestly. Na Mungu akutane na haja za mioyo yetu.
 
Disappointed, kila siku huwa unatoa nondo,leo sijui upepo umepita pabaya....au umekataliwa maana huu ni uchungu unaoutoa....
Wewe anza kwa nduguzo wa kike utakuta wanatumika vibaya mno..hebu ngoja nianze siku yangu kwa baraka wacha niishie hapa....
mdogo wangu @brenda18 kwanza nikuambie tu ukweli kuwa mimi sijawahi kutongoza mwanamke yoyote humu ndani.

Pili sijawahi kukataliwa kwa kuwa Sijawahi kutongoza na wala sinaga tabia ya kutongoza Ovyo.

Ukweli usiofichika na ambao unawaumiza wengi na wewe ukiwa mmoja wapo ni hili nililosema.

Wanawake wengi mnajisahau mnapokuwa kwenye wakati wenu, mnashindwa kujitengeneza kwa wakati ujao.

Mnasahau kuwa maisha yanasonga na Hayarudi nyuma. Mmekuwa ni watu wa kufake kila kitu na wakati huo wote mnakuwa hamumjui mwenyezi Mungu.

Mnafanya vitu kwa makusudi bila kuwa na Hofu na Mungu.. Mnakuwa juu kwa mambo hata ya Kipuuzi bila kutambua uwepo wa athari zake..

Lakini cha Ajabu mnapokuja kuchuja na kuona kila kitu kimekuwa kipa Kwenu ndipo hapo mnapouhitaji msaada Wa Mungu.... Mmemfanya Mungu ni kama Shimo la taka ambazo mliziweka kwa makusudi Licha ya kujua Kwamba Hazifai.

Ni ukweli Usiofichika Jf inaficha Mambo Mengi sana.. Kukosekana kwa sura zetu kumeifanya jf iwe ni sehemu yenye wanawake Wazuri ambao hawana hata kasoro.. Inawezekana mimi nakufahamu kwa sura na wewe wanifahamu hivyo hivyo lakini kile tunachokiandika Humu Kinapita mbali katika Ukweli:

nilichokisema ni kweli.. Wengi mmekongoloka na hampo katika hadhi ya haya mnayoyaandika Humu. Mna Umri mdogo lakini mpo kama ma mama wa miaka Arobaini au hamsini. Muonekano wenu umekuwa wa kutiliwa mashaka na mnakuwa katika wakati ambao mnajuta kwa yale mliyoyafanya.

Kuhusu ndugu Zangu kutumika vibaya hilo sina shaka nao kwa kuwa Kila mmoja ameshakuwa na Mji wake na Anaishi katika ndoa Yake. Hawakupata wasaa wa kumfanyia Mungu majaribio kama Wengine.

Kuhusu kuandika kwangu nondo Kila Siku Hilo ni jukumu langu pale ninapohisi natakiwa kufanya Hivyo.

Mdogo wangu @brenda18 Hii ni vita. Vita ambayo inapigwana kwa kila aina Ya Silaha. Vita ambayo Haiangalii huyu ni Rafiki Huyu ni nani... Vita ya kutetea kile kilicho Cha msingi... Vita ya kuwarudisha Wanawake Waliopotea Mikononi kwa mwenyezi Mungu. Vita ya kuwakumbusha Cha kufanya kabla Hamjajuta....

Kama Maneno Yangu yamekupiga na umeshindwa kustahimili basi Rudi mikononi kwa Mungu... Yeye Hajashindwa, hajawahi kushindwa na hatashindwa.

Ibra87 hajawahi kumtongoza mwanamke Jf... Au nikupe password Zangu uangalie?

Naamini humu ndani Hakuna mwanamke wa kunifaa mimi kwa kuwa wote ni wale wale tu.

Nisamehe @brenda18 huu ndio ukweli wangu Ibra87 au Ibrahim Masimba.... Am very sorry mama
 
Kuanzia kumekucha busara na hekima huku mkilitaja jina lake Mungu limechukua nafasi zaidi. Haya sasa Munge aendele kutawala midomo yenu nene mabaya tena
 
Mxiuuuuuuuuuuu! WANAUME WENYEGUBU KAMA MTOA MADA NDO WANAKUFUJA MPAKA UNAKIONA CHA MTEMA KUNI. Hapo hajakuoa nyodo ndo zipo level hiooo! Hahahaaaaaaaa! Ndo ile mume wa kuchoraa, mume mume jina hakujui kwa sabuni wala kanga. Hahahaaa! Kwenda KFC sahau. Ndo maana nawaambia Wanawake TUFANYE KAZI USIJIBWETEKEEE. Ukipata jibaba kama hili utavaa lonya na wanao mpaka ukomeee. Kariakoo itakukoma, sare za jiji ndo zako, ofisini kama mfagizi. Nguo ya ghali kumiliki 30,000. Hahahaaa! Ngachokaaa! Nguo za kina TK Fashions kijitonyama za 150,000 cheappest kwa 300,000 utaziona dukani tu Hahahaaa! Jibaba hili likupe 200,000 ununue gauni thubutuuuuu!

Ila kuna WANAUME WANA ROHOOOOOO! We acha tu! Mpaka unashukuru Mungu! Anakupa matunzo unadhibitisha bila shaka yoyote ni uzao wa Abel! Anakuoa na mitoto yako na kuilea kabisaaa. NDO KUSEMA HUMUONI ZARI AU? Na mitoto yake 3 na bado katupiga vikumbo wali tusioijua lebaaa.
Kubwa la Maadui in Action,
Wallahi usingekuja ningeshangaa sana
 
Ni jambo jema kukumbushana kumrudia Mungu,
Tatizo linakuja pale ambapo lugha inayotumika na namna tunayotumia kukumbushana.
Mda mwengine tunakumbushana kama vile sie tunaowakumbusha ni wasafi saana,
@ibra87
 
Ni jambo jema kukumbushana kumrudia Mungu,
Tatizo linakuja pale ambapo lugha inayotumika na namna tunayotumia kukumbushana.
Mda mwengine tunakumbushana kama vile sie tunaowakumbusha ni wasafi saana,
@ibra87

Kwani bwana shemeji wewe una dhambi eti?? Subiri kwanza ukongoroke bwana now we ni handithamu Mungu hakuhusu, sema aimeeeeeeen!!
 
Back
Top Bottom