Kinachosababisha JK aogopwe

akashube

JF-Expert Member
Dec 24, 2009
401
23
Huyu jamaa ni mlipa visasi namba moja nchi hii, na pia ni mlipa fadhila mkubwa.

1. P. Mang'ula aliyekuwa mkti wa kampeni za CCM 2005 alionyesha kutomkubali matokeo yake kila alikojaribu kugombea kwenye chama kapigwa chini. Mkono wa JK haukumwacha Ikiwemo kwenye kugombea uenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa. Leo hii kakaa benchi mpaka amegeuka benchi yeye mwenyewe.

2. S. A. Salim alipoamua kugombea urais 2005, JK alimuona kama msaliti na kumzushia kuwa ni mwarabu wa Oman hivyo hastahili kuwa Rais. Hili limerudiwa kwa Bashe ambaye hata ugomvi wake haukuwa na JK bali na kundi la RK. Lakini JK mwenyewe akarudia yale ya Salim, kwamba Bashe, kada wa CCM ati ni msomali......

3. Prof. F. Sarungi katika moja ya mikutano ya mwisho ya bunge 2005 aliombwa na JK wakiwa bungeni, wote wakiwa mawaziri ili amsaidie kwa kuwa JK alikuwa na nia ya kugombea. Prof alikataa ombi hilo kwa dharau kubwa, matokeo yake tunayaona leo Sarungi kafifishwa kabisa.

4. E.N Lowasa, B.P Mramba, A. Mgonja, A. Chenge, J. Mungai na wengineo walionyesha kuanza kuleta fukuto za chini chini za kuhoji utendaji kazi wa JK, kilichotokea ni kwamba katika jambo lililohusu serikali nzima ya JK wametolewa kafara wao. Swahiba wake Z. Meghji ambaye ni muhusika mkuu, tena siku zote ndiye mweka hazina wa pesa za wizi zinazotumika kumuweka JK ikulu ikiwemo zile za EPA, yeye hakuguswa. Na Rostam je? Na Kagoda je? wakiguswa nchi itapasuka????? Na hapa Watanzania wamepigwa changa la macho......

5. H. Mwinyi na uwaziri wa ulinzi ni matokeo ya kulipa fadhila kwa Mzee A. H. Mwinyi.

Mengineyo utajaza mwenyewe kama:

i) V. Kamata na kanafasi ka BOT, na ubunge viti maalum, na kusomeshwa nje, fadhila kwa kazi gani?

ii) Mrema alivyolamba miguu ya JK na kusaidiwa matibabu, kisha karudi, sifa zote kwa JK, JK tayari katoa ridhaa yake kuwa CCM wamsaidie Vunjo apate ubunge.

iii) N. Nnauye mambo vipi? hapa siongezi neno....maana ya juzi haya unayakumbuka???

iv) L. Masha muajiri wa RK naye ni muajiriwa wa baba yake RK au ikoje?.....

v) Unadhani wabunge waliotetea sana kiswahili bungeni walifanya hivyo kwa uzalendo??? no..no...no... usidanganyike kirahisi, hapo watu walikuwa wanamkingia kifua mama.....mama....mama jamani hamuelewi....mama SK ebo? fadhila zinatafutwa.

Shibuda shibuda, naona kalamu inagoma goma

USIONE WATU WANAUNGA UNGA MKONO CCM NA JK HUMU NA KWINGINEKO. MOYONI HAWAMTAKI LAKINI WANAHOFU KUBWA JUU YA KITAKACHOJIRI AKICHUKUA NCHI.

NCHI HAITAWEZA KUENDELEA BILA WATU KUACHA UNAFIKI NA WOGA HUU WA KIPUUZI!!!!

JK wapi Babu Seya!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Huyu jamaa ni mlipa visasi namba moja nchi hii, na pia ni mlipa fadhila mkubwa.

1. P. Mang'ula aliyekuwa mkti wa kampeni za CCM 2005 alionyesha kutomkubali matokeo yake kila alikojaribu kugombea kwenye chama kapigwa chini. Mkono wa JK haukumwacha Ikiwemo kwenye kugombea uenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa. Leo hii kakaa benchi mpaka amegeuka benchi yeye mwenyewe.

2. S. A. Salim alipoamua kugombea urais 2005, JK alimuona kama msaliti na kumzushia kuwa ni mwarabu wa Oman hivyo hastahili kuwa Rais. Hili limerudiwa kwa Bashe ambaye hata ugomvi wake haukuwa na JK bali na kundi la RK. Lakini JK mwenyewe akarudia yale ya Salim, kwamba Bashe, kada wa CCM ati ni msomali......

3. Prof. F. Sarungi katika moja ya mikutano ya mwisho ya bunge 2005 aliombwa na JK wakiwa bungeni, wote wakiwa mawaziri ili amsaidie kwa kuwa JK alikuwa na nia ya kugombea. Prof alikataa ombi hilo kwa dharau kubwa, matokeo yake tunayaona leo Sarungi kafifishwa kabisa.

4. E.N Lowasa, B.P Mramba, A. Mgonja, A. Chenge, J. Mungai na wengineo walionyesha kuanza kuleta fukuto za chini chini za kuhoji utendaji kazi wa JK, kilichotokea ni kwamba katika jambo lililohusu serikali nzima ya JK wametolewa kafara wao. Swahiba wake Z. Meghji ambaye ni muhusika mkuu, tena siku zote ndiye mweka hazina wa pesa za wizi zinazotumika kumuweka JK ikulu ikiwemo zile za EPA, yeye hakuguswa. Na Rostam je? Na Kagoda je? wakiguswa nchi itapasuka????? Na hapa Watanzania wamepigwa changa la macho......

5. H. Mwinyi na uwaziri wa ulinzi ni matokeo ya kulipa fadhila kwa Mzee A. H. Mwinyi.

Mengineyo utajaza mwenyewe kama:

i) V. Kamata na kanafasi ka BOT, na ubunge viti maalum, na kusomeshwa nje, fadhila kwa kazi gani?

ii) Mrema alivyolamba miguu ya JK na kusaidiwa matibabu, kisha karudi, sifa zote kwa JK, JK tayari katoa ridhaa yake kuwa CCM wamsaidie Vunjo apate ubunge.

iii) N. Nnauye mambo vipi? hapa siongezi neno....maana ya juzi haya unayakumbuka???

iv) L. Masha muajiri wa RK naye ni muajiriwa wa baba yake RK au ikoje?.....

v) Unadhani wabunge waliotetea sana kiswahili bungeni walifanya hivyo kwa uzalendo??? no..no...no... usidanganyike kirahisi, hapo watu walikuwa wanamkingia kifua mama.....mama....mama jamani hamuelewi....mama SK ebo? fadhila zinatafutwa.

Shibuda shibuda, naona kalamu inagoma goma

USIONE WATU WANAUNGA UNGA MKONO CCM NA JK HUMU NA KWINGINEKO. MOYONI HAWAMTAKI LAKINI WANAHOFU KUBWA JUU YA KITAKACHOJIRI AKICHUKUA NCHI.

NCHI HAITAWEZA KUENDELEA BILA WATU KUACHA UNAFIKI NA WOGA HUU WA KIPUUZI!!!!

JK wapi Babu Seya!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Hivi wewe jaribu kuangalia hali halisi ya kisiasa, je unaweza kuwachaguwa watu ambao hawajakuunga mkono kwenye kutafuta uongozi au madaraka...? Itakapotokea kuwa umewachaguwa tena na kukuendea kinyume utasemaje...!?

Malalamiko mengine hayana maana hata kidogo.
 
Major Ganeral Lupogo . Alimfanyia mavisa hadi leo . Jk ni Hoolgan
 
Hivi wewe jaribu kuangalia hali halisi ya kisiasa, je unaweza kuwachaguwa watu ambao hawajakuunga mkono kwenye kutafuta uongozi au madaraka...? Itakapotokea kuwa umewachaguwa tena na kukuendea kinyume utasemaje...!?

Malalamiko mengine hayana maana hata kidogo.
Obama kamchagua Mama Clinton, Mkapa alimchagua Kikwete na hata Dr.Slaa atamchagua Kikwete kuwa balozi wetu Marekani!...
 
Liyumba alimchukulia Bibi miaka hiyooo....................

Mwaka 2005 walipotangaza matokeo, Lipumba akaanza kulia.......

Akasema wazi kabisa kuwa "mwenzenu ni mfungwa sasa.............."

Mwakawago yalimpata hayahaya na Mzee FMes alitumwagia hapa shule alivyofanyiwa Unyama.

RIP Mwakawago.
 
Hivi wewe jaribu kuangalia hali halisi ya kisiasa, je unaweza kuwachaguwa watu ambao hawajakuunga mkono kwenye kutafuta uongozi au madaraka...? Itakapotokea kuwa umewachaguwa tena na kukuendea kinyume utasemaje...!?

Malalamiko mengine hayana maana hata kidogo.

Uwe mwepesi wa kusoma mada lakini sio kujibu, inahitaji uwe 'great thinker' na ninaamini ndivyo ulivyo, ila hapa hukujitendea haki. Jiulize yafuatayo:

1. Unahalalisha mtu aambiwe si raia wa Tanzania na kunyimwa haki yake ya kuchaguliwa kwa kuwa tu ametumia haki yake kwa kuamua kugombea cheo unachogombea wewe au pengine amekupinga???

2. P. Mang'ula kwa mfano ujue hakuwa mnafiki, alimwonyesha wazi JK kuwa hamuungi mkono, je unahalalisha kwa hilo kuwa afanyiwe fitina kwa mkono wa JK hata pale alipotumia haki yake kugombea nafasi ndani ya chama chake. Ukumbuke hii ilikuwa kwenye kura za maoni ndani ya CCM, na alipopita JK, Mang'ula alimuunga mkono kama mgombea wa chama chake....na alichangia kwa kiasi kikubwa sana kuleta ushindi...kumbuka alikuwa ni mwenyekiti wa kampeni. Sasa visasi hivi unaviunga mkono.

Yaani mtu awe anapita kwa asilimia 100% yaani asipingwe? anayekupinga ni adui? hiyo ni demokrasia au domokrasia?

3. Uswahiba na unafiki ndio iwe 'qualification' ya watu wa karibu na wewe. Halafu matokeo yake unabadilisha badilisha baraza la mawaziri, tena si kwa matakwa yako bali kwa sababu Dr. Slaa amekuja juu na hataki mambo yenu ya uendeshaji serikali kipuuzi.

Suala hapa ni ule upofu na jazba ya kulipa fadhila au kisasi badala ya kufanya kazi ya nchi.

Hey 'THINK'. acha ushabiki.
 
Hivi wewe jaribu kuangalia hali halisi ya kisiasa, je unaweza kuwachaguwa watu ambao hawajakuunga mkono kwenye kutafuta uongozi au madaraka...? Itakapotokea kuwa umewachaguwa tena na kukuendea kinyume utasemaje...!?

Malalamiko mengine hayana maana hata kidogo.

Kwani Hillary Clinton alimuunga mkono Obama.?we vipi bana
 
Kwani Hillary Clinton alimuunga mkono Obama.?we vipi bana

Huyu sidhani kama ali'think' kama great thinker, naona alikurupuka kujibu. Kama ameamua ku'think' atakuwa amejifunza ili aje na hoja ng'amuzi.

Hili swali lako litamwamsha.
 
Jamani si kila mtu huwa na vipa umbele vyake linapokuja suwala la kuchaguwa wasaidizi au viongozi!? Hapa mimi nashindwa kuelewa, alipaswa kuchaguwa vile alivyo ona yeye inafaha, vile mnavyo ona nyinyi inafaha?
 
Uwe mwepesi wa kusoma mada lakini sio kujibu, inahitaji uwe 'great thinker' na ninaamini ndivyo ulivyo, ila hapa hukujitendea haki. Jiulize yafuatayo:


3. Uswahiba na unafiki ndio iwe 'qualification' ya watu wa karibu na wewe. Halafu matokeo yake unabadilisha badilisha baraza la mawaziri, tena si kwa matakwa yako bali kwa sababu Dr. Slaa amekuja juu na hataki mambo yenu ya uendeshaji serikali kipuuzi.

Suala hapa ni ule upofu na jazba ya kulipa fadhila au kisasi badala ya kufanya kazi ya nchi.

Hey 'THINK'. acha ushabiki.
Mambo yenu tena, mbona hapo sijakuelewa, mambo yenu yapi?
 
Wana JF nasikia kwa mama Mbega nayo ni Fadhila, mwenye data please. Maana nilikuwa naongea na jamaa mmoja toka Iringa alinigusia hilo kuwa ni fadhila toka uchaguzi wa mwaka 2000 mpaka leo mama huyo huwa anabebwa katika kugombea ubunge kitu ambacho kimetokea kwa mwakalebela kupigwa chini ingawaje kutokana na maneno ya Makamba kuwa wote walitoa rushwa ingawaje walitofautiana, Sasa kwa mama huyo rushwa yake ilizidi ile Mwakalebela?au ndo mambo ya fadhila?

Vipi tena kuhusu mpiganaji selelii? usikute naye ni kisasi maana si yeye aliyehoji kuhusu upanuzi wa barabara ya chalinze-segera wakati ndo njia ya JK? Mwenye data please!

All da best
 
Kuna tofauti kubwa sana katika siasa za marekani na tzn "afrika kwa ujumla" sula la kuzushiwa uraia siliungi mkono ila swala zima la kumchaguwa mpinzani wako serikalini..??? Acha weweee... Waafrika sisi tukichuklia tumechukiwa anaweza akaharibu mipanga yako yoote ilimradi kukudhalilisha kwenye ndio akaweka sio na kwenye sio akaweka ndio
 
Jamani si kila mtu huwa na vipa umbele vyake linapokuja suwala la kuchaguwa wasaidizi au viongozi!? Hapa mimi nashindwa kuelewa, alipaswa kuchaguwa vile alivyo ona yeye inafaha, vile mnavyo ona nyinyi inafaha?
wewe ndio hujaelewa mleta mada, umeamua kuelewa kivyako... sikiliza usikilizwe!!
 
Wana JF nasikia kwa mama Mbega nayo ni Fadhila, mwenye data please. Maana nilikuwa naongea na jamaa mmoja toka Iringa alinigusia hilo kuwa ni fadhila toka uchaguzi wa mwaka 2000 mpaka leo mama huyo huwa anabebwa katika kugombea ubunge kitu ambacho kimetokea kwa mwakalebela kupigwa chini ingawaje kutokana na maneno ya Makamba kuwa wote walitoa rushwa ingawaje walitofautiana, Sasa kwa mama huyo rushwa yake ilizidi ile Mwakalebela?au ndo mambo ya fadhila?

Vipi tena kuhusu mpiganaji selelii? usikute naye ni kisasi maana si yeye aliyehoji kuhusu upanuzi wa barabara ya chalinze-segera wakati ndo njia ya JK? Mwenye data please!

All da best

Hapa kwa Selelii nadhani inabidi tumuulize Dr. Rosti tamu ya mzizi.....kumradhi ninamaanisha R.Aziz mwenye kuvuna asichopanda kupitia Caspian, jamaa wanachimba dhahabu na hawalipi chochote serikalini zaidi ya kuongeza ajira kwa watoto wa mafisadi na kutoa 'takrima' kwa JK....sasa muulize Rosti ya Mzizi...Selelii alihoji nini juu ya hili???

CCM kunanuka mambo nyie....ndo mana kuna watu wako radhi watoe mtu roho lakini sio CCM itoke madarakani maana wanajua uozo wao mwingi utajulikana.

Selelii kashadanganywa saa hizi kuwa atapewa ukuu wa mkoa......na advertise ya kwanza ni Nape, JK kweli noma...anaujua vyema mchezo wa karoti na fimbo.....jamaa wanachezewa kama ngedere wa kufugwa.
 
nakuaminia X hawa wenzetu wanataka nini, hakuna hata mkuu mmoja anaefanya tofauti hata huyo slaa akiingia naona watu jf wengi watakuwa mawaziri
 
kiongozi anachaguliwa na mungu bwana no matter what, mtasema mengi lakini hata slaa akiingia utashangaa ya firauni tupiganie kuondoa uovu ndani ya nchi yetu kwa amani si kwa kubezana, hakuna aneweza kutawala 100percent bwana,
 
mi nawauliza wenye kutaka mabadiliko, haya yametokea kwenye nchi zetu nyingi za kiafrica,Zambia n.k wamebadilisha vyama viliyooriginate kuleta uhuru, lakini kuna nini cha ajabu mlichokiona kimebadilika jamani tusijidanganye, tutatue matatizo yetu kwa njia sahihi. CCM hadi sasa haijakaa vyema tokaa ichukue nchi,miaka zaidi ya hamsini, hilo ni wazi , lakini tukiitoa madaraka leo tutegemee miaka mingine sitini au zaidi kwa chama kingine kukaa sawa,
 
Kuna tofauti kubwa sana katika siasa za marekani na tzn "afrika kwa ujumla" sula la kuzushiwa uraia siliungi mkono ila swala zima la kumchaguwa mpinzani wako serikalini..??? Acha weweee... Waafrika sisi tukichuklia tumechukiwa anaweza akaharibu mipanga yako yoote ilimradi kukudhalilisha kwenye ndio akaweka sio na kwenye sio akaweka ndio

Vipi kuhusu Mzee Mandela na Chifu Buthelezi wa Inkhata?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom