Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,603
- 29,748
naziona hekima za Baba wa taifa hapa.Uwe mwepesi wa kusoma mada lakini sio kujibu, inahitaji uwe 'great thinker' na ninaamini ndivyo ulivyo, ila hapa hukujitendea haki. Jiulize yafuatayo:
1. Unahalalisha mtu aambiwe si raia wa Tanzania na kunyimwa haki yake ya kuchaguliwa kwa kuwa tu ametumia haki yake kwa kuamua kugombea cheo unachogombea wewe au pengine amekupinga???
2. P. Mang'ula kwa mfano ujue hakuwa mnafiki, alimwonyesha wazi JK kuwa hamuungi mkono, je unahalalisha kwa hilo kuwa afanyiwe fitina kwa mkono wa JK hata pale alipotumia haki yake kugombea nafasi ndani ya chama chake. Ukumbuke hii ilikuwa kwenye kura za maoni ndani ya CCM, na alipopita JK, Mang'ula alimuunga mkono kama mgombea wa chama chake....na alichangia kwa kiasi kikubwa sana kuleta ushindi...kumbuka alikuwa ni mwenyekiti wa kampeni. Sasa visasi hivi unaviunga mkono.
Yaani mtu awe anapita kwa asilimia 100% yaani asipingwe? anayekupinga ni adui? hiyo ni demokrasia au domokrasia?
3. Uswahiba na unafiki ndio iwe 'qualification' ya watu wa karibu na wewe. Halafu matokeo yake unabadilisha badilisha baraza la mawaziri, tena si kwa matakwa yako bali kwa sababu Dr. Slaa amekuja juu na hataki mambo yenu ya uendeshaji serikali kipuuzi.
Suala hapa ni ule upofu na jazba ya kulipa fadhila au kisasi badala ya kufanya kazi ya nchi.
Hey 'THINK'. acha ushabiki.
Thanx sana AKASHUBE umetoa assumption ya karne sana hapo.
Asomaye na afahamu