Mambo yanayohusu ulinzi na usalama ni classified, hayapaswi kupewa media attention, vifaru ni silaha za kivita na sio vifaa vya kutunzia usalama, hivyo ukiona vifaru, ujue tayari taarifa za kiintelijensia zimeishawafikia, na wanausalama makini kote dunia, hujipanga kukinga ni bora kuliko tiba, hivyo vifaru huko ni kwa ajili ya tahadhai kabla ya hatari, kuna mambo fulani kuna magaidi fulani wamepanga kufanya ugaidi fulani, hivyo kitendo tuu cha kuviona vifaru na ulinzi ulioimarishwa, hao magaidi, hawataendelea tena kutekeleza nia zao ovu!.
Kwa hayo yanayotokea kwa vile Wanzanzibari wenyewe wapo na wameyakubali, ulitaka wafanye nini?!. Viongozi sio ni kama hawapo, bali kiukweli hawapo kikatiba na kisheria, muda wao ulikwisha asmi November 4, sasa wapo wapo tuu kama hawapo!. Wana dini pia wapo kuwafikisha watu mbinguni na sio kuwaingiza magaidi ikulu!, taasisi za kiraia zipo kufanya kazi za kiaia na sio kuingilia mambo ya siasa!, taasisi za haki za binadamu zipo na zinasubiri malalamiko yoyote rasmi kuhusu ukiukwaji wa haki za binaadamu, na hakuna malalamiko yoyote so far!, hii inamaanisha watu wote wameridhika na yote yanayotendwa!. Taasisisi za kisheria pia zipo, taratibu za taasisi zozote za kisheria ni kwa watu wenye malalamiko yoyote ya kisheria kuzifuata kuomba msaada wa kisheria, lakini kwa yote yanayotokea Zanzibar, hakuna yoyote aliyechukua hatua yoyote kulalamika popote, hivyo ulitegemea taasisi hizo zifanye nini?!, yaani daktari atoke hospitalini aanze kutembelea majumbani kuulizia wagonjwa?!, kikawaida kama mahali kuna mgonjwa, mgonjwa huyo ndie atakwenda hospitali kufuata tiba na sii vinginevyo!. Vyama vya siasa ndio kabisa, vipo kama havipo kwa sababu wao ndio waathirika wakuu, sheria taratibu na kanuni wanazijua, hawakufanya lolote zaidi ya kuitisha press conference na kupiga mikelele tuu, unategemea nini?!.
Usalama kwanza, mengine yote baadae!.
Pasco