Kinachoendelea Zanzibar ni aibu kwa nchi

KISHADA

JF-Expert Member
Oct 18, 2012
2,224
3,290
Kwanza kuna matukio hayapati nafasi katika vyombo vya habari vingi kuhusu kile kinachoendelea Zanzibar. Zikiwa zimebaki siku sita tu kufanyika kile kinaitwa uchaguzi wa marudio hali ya Zanzibar ni Aibu.

Kwa sasa kumepelekwa vyombo vya ulinzi kwa wingi wakiwemo wanajeshi hasa kisiwani pemba na tayari vyombo hivyo vinaonekana wazi wazi kuleta athari. Kumeripotiwa taarifa za vifaru vya jeshi kuonekana vikitembea barabarani mchana kweupe na wananchi kuingiwa hofu.

Hali hii hujitokeza Zanzibar pekee katika Tanzania hii. Lengo lake halijulikani kama ni huu uchaguzi wa marudio au kuna zaidi ya uchaguzi.

Kuna mpasuko mkubwa wa kijamii. Imefika wakati hasa kisiwani Pemba watu wameshaanza kususiana mambo mbali mbali.

Mifano.

i. Kususiwa baadhi ya wananchi kusafirishwa kwa kivuko kutoka kisiwa kidogo (Kisiwa Panza) kwenda chokocho. Ifahamike mgogoro huu unafukuta na unahusishwa na siasa za uchaguzi wa marudio.

ii Kususiwa kwa baadhi ya mambo ya kijamii ikiwemo maziko na shughuli ya harusi. Maeneo mbali mbali yamejitokeza kwa njia baridi huko Pemba.

iii. Kuna taarifa za viongozi wa kitaifa Zanzibar (Sitaji Majina) kususiwa misikiti zaidi ya mara mbili pale inapopatikana habari kuwa wanakwenda kuswali jamii inasusa kwenda na kuwaachia viongozi wa serikali peke yao. Zipo taarifa ni hapa majuzi kiongozi mmoja alisusiwa ufunguzi wa msikiti hali iliyolazimu kuletwa askari wa kikosi fulani kuongeza idadi ya watu.

iv Kuzomewa baadhi ya viongozi wa kitaifa huko kisiwani Pemba na kususiwa kwenye shughuli za
maendeleo

Kwa ufupi kuna hali mbaya Zanzibar imeanza kujitokeza na inatarajiwa kukua na kuongeza uhasama zaidi. Watu wameanza kuchoma nyumba moto na baraza za vyama vya siasa.

Kuna hali ya kutiliana mashaka na ukimya wa kutisha unaoashiria shari, kuna kutishana kwa kutumia vyombo vya dola. Kumeanza kupigwa marufuku mikusanyiko katika baadhi ya maeneo Zanzibar.

Kuna masuali ya kujiuliza Nini hatima ya Zanzibar ikiwa hali iko hivi sasa kabla ya kufanyika uchaguzi wa marudio uliosusiwa na wadau wakubwa wa Zanzibar? jee Kutakuwa na suluhu yoyote?

Haya yanatokea viongozi ni kama hawapo, wana dini ni kama hawapo, taasisi za kiraia ni kama hazipo, taasisi za haki za binadamu ni kama hazipo, taasisisi za kisheria ni kama hazipo, vyama vya siasa ni kama havipo na wengineo.

Tutegemee nini? hii aibu kwa nchi
 
Haya yanatokea viongozi ni kama hawapo, wana dini ni kama hawapo, taasisi za kiraia ni kama hazipo, taasisi za haki za binadamu ni kama hazipo, taasisisi za kisheria ni kama hazipo, vyama vya siasa ni kama havipo na wengineo. Tutegemee nini? hii aibu kwa nchi
Mambo yanayohusu ulinzi na usalama ni classified, hayapaswi kupewa media attention, vifaru ni silaha za kivita na sio vifaa vya kutunzia usalama, hivyo ukiona vifaru, ujue tayari taarifa za kiintelijensia zimeishawafikia, na wanausalama makini kote dunia, hujipanga kukinga ni bora kuliko tiba, hivyo vifaru huko ni kwa ajili ya tahadhai kabla ya hatari, kuna mambo fulani kuna magaidi fulani wamepanga kufanya ugaidi fulani, hivyo kitendo tuu cha kuviona vifaru na ulinzi ulioimarishwa, hao magaidi, hawataendelea tena kutekeleza nia zao ovu!.

Kwa hayo yanayotokea kwa vile Wanzanzibari wenyewe wapo na wameyakubali, ulitaka wafanye nini?!. Viongozi sio ni kama hawapo, bali kiukweli hawapo kikatiba na kisheria, muda wao ulikwisha asmi November 4, sasa wapo wapo tuu kama hawapo!. Wana dini pia wapo kuwafikisha watu mbinguni na sio kuwaingiza magaidi ikulu!, taasisi za kiraia zipo kufanya kazi za kiaia na sio kuingilia mambo ya siasa!, taasisi za haki za binadamu zipo na zinasubiri malalamiko yoyote rasmi kuhusu ukiukwaji wa haki za binaadamu, na hakuna malalamiko yoyote so far!, hii inamaanisha watu wote wameridhika na yote yanayotendwa!. Taasisisi za kisheria pia zipo, taratibu za taasisi zozote za kisheria ni kwa watu wenye malalamiko yoyote ya kisheria kuzifuata kuomba msaada wa kisheria, lakini kwa yote yanayotokea Zanzibar, hakuna yoyote aliyechukua hatua yoyote kulalamika popote, hivyo ulitegemea taasisi hizo zifanye nini?!, yaani daktari atoke hospitalini aanze kutembelea majumbani kuulizia wagonjwa?!, kikawaida kama mahali kuna mgonjwa, mgonjwa huyo ndie atakwenda hospitali kufuata tiba na sii vinginevyo!. Vyama vya siasa ndio kabisa, vipo kama havipo kwa sababu wao ndio waathirika wakuu, sheria taratibu na kanuni wanazijua, hawakufanya lolote zaidi ya kuitisha press conference na kupiga mikelele tuu, unategemea nini?!.

Usalama kwanza, mengine yote baadae!.

Pasco
 
Kwanza kuna matukio hayapati nafasi katika vyombo vya habari vingi kuhusu kile kinachoendelea Zanzibar. Zikiwa zimebaki siku sita tu kufanyika kile kinaitwa uchaguzi wa marudio hali ya Zanzibar ni Aibu.

Kwa sasa kumepelekwa vyombo vya ulinzi kwa wingi wakiwemo wanajeshi hasa kisiwani pemba na tayari vyombo hivyo vinaonekana wazi wazi kuleta athari. Kumeripotiwa taarifa za vifaru vya jeshi kuonekana vikitembea barabarani mchana kweupe na wananchi kuingiwa hofu.

Hali hii hujitokeza Zanzibar pekee katika Tanzania hii. Lengo lake halijulikani kama ni huu uchaguzi wa marudio au kuna zaidi ya uchaguzi.

Kuna mpasuko mkubwa wa kijamii. Imefika wakati hasa kisiwani Pemba watu wameshaanza kususiana mambo mbali mbali.

Mifano.

i. Kususiwa baadhi ya wananchi kusafirishwa kwa kivuko kutoka kisiwa kidogo (Kisiwa Panza) kwenda chokocho. Ifahamike mgogoro huu unafukuta na unahusishwa na siasa za uchaguzi wa marudio.

ii Kususiwa kwa baadhi ya mambo ya kijamii ikiwemo maziko na shughuli ya harusi. Maeneo mbali mbali yamejitokeza kwa njia baridi huko Pemba.

iii. Kuna taarifa za viongozi wa kitaifa Zanzibar (Sitaji Majina) kususiwa misikiti zaidi ya mara mbili pale inapopatikana habari kuwa wanakwenda kuswali jamii inasusa kwenda na kuwaachia viongozi wa serikali peke yao. Zipo taarifa ni hapa majuzi kiongozi mmoja alisusiwa ufunguzi wa msikiti hali iliyolazimu kuletwa askari wa kikosi fulani kuongeza idadi ya watu.

iv Kuzomewa baadhi ya viongozi wa kitaifa huko kisiwani Pemba na kususiwa kwenye shughuli za
maendeleo

Kwa ufupi kuna hali mbaya Zanzibar imeanza kujitokeza na inatarajiwa kukua na kuongeza uhasama zaidi. Watu wameanza kuchoma nyumba moto na baraza za vyama vya siasa.

Kuna hali ya kutiliana mashaka na ukimya wa kutisha unaoashiria shari, kuna kutishana kwa kutumia vyombo vya dola. Kumeanza kupigwa marufuku mikusanyiko katika baadhi ya maeneo Zanzibar.

Kuna masuali ya kujiuliza Nini hatima ya Zanzibar ikiwa hali iko hivi sasa kabla ya kufanyika uchaguzi wa marudio uliosusiwa na wadau wakubwa wa Zanzibar? jee Kutakuwa na suluhu yoyote?

Haya yanatokea viongozi ni kama hawapo, wana dini ni kama hawapo, taasisi za kiraia ni kama hazipo, taasisi za haki za binadamu ni kama hazipo, taasisisi za kisheria ni kama hazipo, vyama vya siasa ni kama havipo na wengineo.

Tutegemee nini? hii aibu kwa nchi
Jamani tuwe wakweli. Hivi hili figisu kalianzisha nani? Hebu kwanza naomba mtafakari haya matokeo yaliyotolewa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar kutoka majimbo 31 kati ya 54 wakati wakiendelea kupokea mengine[Matokeo hayo yaliyokuwa yametangazwa kufikia saa mbili jioni Oktoba 27 ni kama ifuatavyo:
Matokeo ya uchaguzi wa Rais wa Zanzibar (Majimbo31/54)]

Jina Chama Kura Asilimia
Khamis Iddi Lila ACT-W 189 0.1
Juma Ali Khatib ADA-TADEA 93 0.0
Hamad Rashid Mohamed ADC 252 0.1
Said Soud Said AFP 223 0.1
Ali Khatib Ali CCK 240 0.1
Ali Mohamed Shein CCM 139,557 57.9
Mohammed Massoud Rashid CHAUMMA 257 0.1
Seif Sharif Hamad CUF 93,699 38.9
Taibu Mussa Juma DM 118 0.0
Abdalla Kombo Khamis DP 86 0.0
Kassim Bakar Aly JAHAZI 227 0.1
Seif Ali Iddi NRA 63 0.0
Issa Mohammed Zonga SAU 127 0.1
Hafidh Hassan Suleiman TLP 107 0.0
Zanzibar ina jumla ya wapiga kura 503,860 waliojiandikisha kupiga kura, kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar.

Halafu twendeni kwenye matokeo aliyotangaza maalim seif
Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, ameitisha mkutano wa waandishi wa habari na kusema kuwa baada ya chama chake kukusanya fomu zote za matokeo kutoka vituoni, yeye amepata kura 200,007 dhidi ya kura 178,363 za mgombea wa CCM anayetetea nafasi yake, Dk. Ali Mohammed Shein.

Sasa twendeni kwenye tafakuri
1 Tume ilitangaza kuwa wapiga kura wote waliojiandikisha walikuwa 503,860
2. Kwenye majimbo 31 kati ya 54 iliripotiwa kuwa Dr. Shein alipata kura 139,557[57.9%] na Maalim Seif
alipata kura 93,699[38.9]
3 Vyama vingine vidogo vilipata kwa pamoja chini ya asilimia 3 ya kura zote

Alipotangaza ushindi maalim alidai kuwa alipata kura 200,0007 na shein alipata 178,363 hizi hesabu ni kwa zanzibara na pemba.
Hakuna kura zilizoharibika wala kura za vyama vingine

Hivi ndugu zangu hapa ni nani wa kulaumiwa? Hivi mlitaka tume ikubaliane na hesabu za maalimi seif ambazo alidai ni za visiwa vyote 2?

Maoni yangu ni kuwa[naomba msitukane ila mtafakari maana hili ni jamvi la 'those who dare to speak'
Maalim baada ya kuona hali ya matokeo kutoka majimbo 31 hadi tarehe 27 yalionyesha dhahiri kuwa ulikuwepo uwezekano mkubwa kwa chama chake kushindwa na ili afe kiume alipreempt tume kwa kuanza kutangaza yeye wakati akifahamu kuwa kwa sheria zilivyosasa ni tume pekee ambayo inahaki ya kutangaza matokeo.
 
Aibu iko wapi mkuu, ukizingatia kwamba zilionekana kasoro tume ikaamuru uchaguzi urudiwe na tarehe 20 ndio uchaguzi unafanyika?
 
Sisi tulitawaliwa sasa ni zamu yetu kuitawala Zanzibar.
Tutaiachia Zanzibar pindi wananchi watakapofanya kama ya Libya
 
Mambo yanayohusu ulinzi na usalama ni classified, hayapaswi kupewa media attention, vifaru ni silaha za kivita na sio vifaa vya kutunzia usalama, hivyo ukiona vifaru, ujue tayari taarifa za kiintelijensia zimeishawafikia, na wanausalama makini kote dunia, hujipanga kukinga ni bora kuliko tiba, hivyo vifaru huko ni kwa ajili ya tahadhai kabla ya hatari, kuna mambo fulani kuna magaidi fulani wamepanga kufanya ugaidi fulani, hivyo kitendo tuu cha kuviona vifaru na ulinzi ulioimarishwa, hao magaidi, hawataendelea tena kutekeleza nia zao ovu!.

Kwa hayo yanayotokea kwa vile Wanzanzibari wenyewe wapo na wameyakubali, ulitaka wafanye nini?!. Viongozi sio ni kama hawapo, bali kiukweli hawapo kikatiba na kisheria, muda wao ulikwisha asmi November 4, sasa wapo wapo tuu kama hawapo!. Wana dini pia wapo kuwafikisha watu mbinguni na sio kuwaingiza magaidi ikulu!, taasisi za kiraia zipo kufanya kazi za kiaia na sio kuingilia mambo ya siasa!, taasisi za haki za binadamu zipo na zinasubiri malalamiko yoyote rasmi kuhusu ukiukwaji wa haki za binaadamu, na hakuna malalamiko yoyote so far!, hii inamaanisha watu wote wameridhika na yote yanayotendwa!. Taasisisi za kisheria pia zipo, taratibu za taasisi zozote za kisheria ni kwa watu wenye malalamiko yoyote ya kisheria kuzifuata kuomba msaada wa kisheria, lakini kwa yote yanayotokea Zanzibar, hakuna yoyote aliyechukua hatua yoyote kulalamika popote, hivyo ulitegemea taasisi hizo zifanye nini?!, yaani daktari atoke hospitalini aanze kutembelea majumbani kuulizia wagonjwa?!, kikawaida kama mahali kuna mgonjwa, mgonjwa huyo ndie atakwenda hospitali kufuata tiba na sii vinginevyo!. Vyama vya siasa ndio kabisa, vipo kama havipo kwa sababu wao ndio waathirika wakuu, sheria taratibu na kanuni wanazijua, hawakufanya lolote zaidi ya kuitisha press conference na kupiga mikelele tuu, unategemea nini?!.

Usalama kwanza, mengine yote baadae!.

Pasco
Kwa maelezo yako unadhihirisha kwamba wanachofanyiwa wazanzibari ni sahihi ilimradi wazanzibari wenyewe wapo sasa unataka wajiripuwe ndio uamini kwamba hawakubaliani na ukoloni huu sio?

Pili unadhihirisha yale ya lukuvi kwamba wewe una imani wapinzani na wazanzibari ni MAGAIDi kwa hivyo hawapaswi kuingia ikulu na kwa mantiki hio Jamuhuri ina haki ya kutembeza vifaru na kutisha raia na wewe una imani kwa kufanya hivyo ndio amani inalindwa. Mpaka lini haya ?

Unajidhirisha jinsi ulivyo ndugu yangu. kwamba wanadini, wanasiasa, na wengine hawastahiki kushiriki kuzuwia shari ya manyanyaso na kukemea dhulma mpaka waombwe kwa barua sio? au wasemee mambo yanayowahusu ya kidini tu na sio mustawa wa nchi? Unaendeleza Aibu ninayoisema.

Tanzania na muungano hautajengwa kwa vifaru bali kwa haki na usawa.

Naiona aibu kuu inakuja.
 
Jamani tuwe wakweli. Hivi hili figisu kalianzisha nani? Hebu kwanza naomba mtafakari haya matokeo yaliyotolewa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar kutoka majimbo 31 kati ya 54 wakati wakiendelea kupokea mengine[Matokeo hayo yaliyokuwa yametangazwa kufikia saa mbili jioni Oktoba 27 ni kama ifuatavyo:
Matokeo ya uchaguzi wa Rais wa Zanzibar (Majimbo31/54)]

Jina Chama Kura Asilimia
Khamis Iddi Lila ACT-W 189 0.1
Juma Ali Khatib ADA-TADEA 93 0.0
Hamad Rashid Mohamed ADC 252 0.1
Said Soud Said AFP 223 0.1
Ali Khatib Ali CCK 240 0.1
Ali Mohamed Shein CCM 139,557 57.9
Mohammed Massoud Rashid CHAUMMA 257 0.1
Seif Sharif Hamad CUF 93,699 38.9
Taibu Mussa Juma DM 118 0.0
Abdalla Kombo Khamis DP 86 0.0
Kassim Bakar Aly JAHAZI 227 0.1
Seif Ali Iddi NRA 63 0.0
Issa Mohammed Zonga SAU 127 0.1
Hafidh Hassan Suleiman TLP 107 0.0
Zanzibar ina jumla ya wapiga kura 503,860 waliojiandikisha kupiga kura, kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar.

Halafu twendeni kwenye matokeo aliyotangaza maalim seif
Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, ameitisha mkutano wa waandishi wa habari na kusema kuwa baada ya chama chake kukusanya fomu zote za matokeo kutoka vituoni, yeye amepata kura 200,007 dhidi ya kura 178,363 za mgombea wa CCM anayetetea nafasi yake, Dk. Ali Mohammed Shein.


Sasa twendeni kwenye tafakuri
1 Tume ilitangaza kuwa wapiga kura wote waliojiandikisha walikuwa 503,860
2. Kwenye majimbo 31 kati ya 54 iliripotiwa kuwa Dr. Shein alipata kura 139,557[57.9%] na Maalim Seif
alipata kura 93,699[38.9]
3 Vyama vingine vidogo vilipata kwa pamoja chini ya asilimia 3 ya kura zote


Alipotangaza ushindi maalim alidai kuwa alipata kura 200,0007 na shein alipata 178,363 hizi hesabu ni kwa zanzibara na pemba.
Hakuna kura zilizoharibika wala kura za vyama vingine


Hivi ndugu zangu hapa ni nani wa kulaumiwa? Hivi mlitaka tume ikubaliane na hesabu za maalimi seif ambazo alidai ni za visiwa vyote 2?

Maoni yangu ni kuwa[naomba msitukane ila mtafakari maana hili ni jamvi la 'those who dare to speak'
Maalim baada ya kuona hali ya matokeo kutoka majimbo 31 hadi tarehe 27 yalionyesha dhahiri kuwa ulikuwepo uwezekano mkubwa kwa chama chake kushindwa na ili afe kiume alipreempt tume kwa kuanza kutangaza yeye wakati akifahamu kuwa kwa sheria zilivyosasa ni tume pekee ambayo inahaki ya kutangaza matokeo.
Ndugu yangu usijitowe fahamu hio ni hatua ya nne katika process ya zoezi la uchaguzi yaani kuhakikiwa na kutangazwa na mwenyekiti.

Matokeo kupitia majimboni yalishatiwa saini na mawakala wote na yalishabandikwa na kuwekwa saini na tume kupitia RO (Returning Officer ) kwa majimbo yote 54 ya Zanzibar.

Wewe unatambuwa Tume kuwa ni Mwenyekiti huo ni ufahamu wako.

Kwa hili bado naiona aibu kwa nchi
 
Ndugu yangu usijitowe fahamu hio ni hatua ya nne katika process ya zoezi la uchaguzi yaani kuhakikiwa na kutangazwa na mwenyekiti.

Matokeo kupitia majimboni yalishatiwa saini na mawakala wote na yalishabandikwa na kuwekwa saini na tume kupitia RO (Returning Officer ) kwa majimbo yote 54 ya Zanzibar.

Wewe unatambuwa Tume kuwa ni Mwenyekiti huo ni ufahamu wako.

Kwa hili bado naiona aibu kwa nchi
Jee unakubali hesabu za maalim seif kuwa amemshinda dr. shein kwa kura 17,000??? Halafu hayo matokeo ya tume ni yale ambayo yalikuwa yanatangazwa kila yanapofika kwenye tume na kuhakikiwa. Hivi inawezekana kuwa tarehe 27 kulitangazwa kura nyingi kuliko matokeo aliyatangaza maalim seif mnamo tarehe 28???? tafakari
 
Huwezi kuiona mpaka uwe na uwezo na uwe tayari kukubali kwamba hiki kinachoendelea ni aibu. Ukiacha ukereketwa unaweza ukaelewa.
labda nikufahamishe mkuu, kua ukiacha ushabiki basi unaweza kuona namna gani uchaguzi ulikua na kasoro na kua kufanya uchaguzi upya liilikua suluhisho sahihi kabisa binafsi nampongeza jecha kwa hatua aliyochukua, na tume kuhakikisha kua uchaguzi wa marudio unafanyika kama ilivyopangwa..
 
Jee unakubali hesabu za maalim seif kuwa amemshinda dr. shein kwa kura 17,000??? Halafu hayo matokeo ya tume ni yale ambayo yalikuwa yanatangazwa kila yanapofika kwenye tume na kuhakikiwa. Hivi inawezekana kuwa tarehe 27 kulitangazwa kura nyingi kuliko matokeo aliyatangaza maalim seif mnamo tarehe 28???? tafakari
Kwanza kampita kwa kura 25,000. Wewe unazungumzia yaliyotangazwa na jecha pale bwawani hujuwi kuwa uchaguzi ulikwisha tokea tarehe 25 Oktoba saa kumi na moja za jioni na matokeo yote yalikwishapatikana tarehe 26 oktoba 2015.

Uliza uambiwe nini kilikuwa kinaendelea pale kisiwandui. Baada ya kupata taarifa KUWA UPINZANI KWA MUJIBU WA MATOKEO YA NCHI NZIMA MAJIMBONI ulishashinda ulizia kama una vyanzo vya kutosha.

Hii ni aibu kwa nchi
 
labda nikufahamishe mkuu, kua ukiacha ushabiki basi unaweza kuona namna gani uchaguzi ulikua na kasoro na kua kufanya uchaguzi upya liilikua suluhisho sahihi kabisa binafsi nampongeza jecha kwa hatua aliyochukua, na tume kuhakikisha kua uchaguzi wa marudio unafanyika kama ilivyopangwa..

Yaani kasoro za uchaguzi na criteria za kuharibika anazijuwa jecha peke yake dunia nzima akuisaidiwa na vuai Ali Vuai Naibu Katimbu Mkuu wa CC....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom