Kinachoendelea Zanzibar ni aibu kwa nchi

Kinachoendelea Zanzibar ni aibu kwa nchi

Mambo yanayohusu ulinzi na usalama ni classified, hayapaswi kupewa media attention, vifaru ni silaha za kivita na sio vifaa vya kutunzia usalama, hivyo ukiona vifaru, ujue tayari taarifa za kiintelijensia zimeishawafikia, na wanausalama makini kote dunia, hujipanga kukinga ni bora kuliko tiba, hivyo vifaru huko ni kwa ajili ya tahadhai kabla ya hatari, kuna mambo fulani kuna magaidi fulani wamepanga kufanya ugaidi fulani, hivyo kitendo tuu cha kuviona vifaru na ulinzi ulioimarishwa, hao magaidi, hawataendelea tena kutekeleza nia zao ovu!.

Kwa hayo yanayotokea kwa vile Wanzanzibari wenyewe wapo na wameyakubali, ulitaka wafanye nini?!. ....
Usalama kwanza, mengine yote baadae!.

Pasco
Je ugaidi unafanywa na nani?
Nani wamepanga ugaidi?
Wale wanaoitwa "mazombie" wanaingia katika kundi la magaidi au ni walinzi na watunza usalama?
Leo zipo habari hizi, kulikoni?
Link1. Zanzibar: Pemba hali ni tete, vurugu kati ya Polisi na raia
Link2. Breaking News: - Zanzibar: Bomu larushwa na kulipua nyumba ya Kamishna wa Polisi
Link3. Haya ndio yaliyotokea usiku wa kuamkia leo Pemba
Link4. Kisiwani Pemba hali yazidi kuchafuka: Polisi na Majeshi yazidi kumiminika
 
Mambo yanayohusu ulinzi na usalama ni classified, hayapaswi kupewa media attention, vifaru ni silaha za kivita na sio vifaa vya kutunzia usalama, hivyo ukiona vifaru, ujue tayari taarifa za kiintelijensia zimeishawafikia, na wanausalama makini kote dunia, hujipanga kukinga ni bora kuliko tiba, hivyo vifaru huko ni kwa ajili ya tahadhai kabla ya hatari, kuna mambo fulani kuna magaidi fulani wamepanga kufanya ugaidi fulani, hivyo kitendo tuu cha kuviona vifaru na ulinzi ulioimarishwa, hao magaidi, hawataendelea tena kutekeleza nia zao ovu!.

Kwa hayo yanayotokea kwa vile Wanzanzibari wenyewe wapo na wameyakubali, ulitaka wafanye nini?!. Viongozi sio ni kama hawapo, bali kiukweli hawapo kikatiba na kisheria, muda wao ulikwisha asmi November 4, sasa wapo wapo tuu kama hawapo!. Wana dini pia wapo kuwafikisha watu mbinguni na sio kuwaingiza magaidi ikulu!, taasisi za kiraia zipo kufanya kazi za kiaia na sio kuingilia mambo ya siasa!, taasisi za haki za binadamu zipo na zinasubiri malalamiko yoyote rasmi kuhusu ukiukwaji wa haki za binaadamu, na hakuna malalamiko yoyote so far!, hii inamaanisha watu wote wameridhika na yote yanayotendwa!. Taasisisi za kisheria pia zipo, taratibu za taasisi zozote za kisheria ni kwa watu wenye malalamiko yoyote ya kisheria kuzifuata kuomba msaada wa kisheria, lakini kwa yote yanayotokea Zanzibar, hakuna yoyote aliyechukua hatua yoyote kulalamika popote, hivyo ulitegemea taasisi hizo zifanye nini?!, yaani daktari atoke hospitalini aanze kutembelea majumbani kuulizia wagonjwa?!, kikawaida kama mahali kuna mgonjwa, mgonjwa huyo ndie atakwenda hospitali kufuata tiba na sii vinginevyo!. Vyama vya siasa ndio kabisa, vipo kama havipo kwa sababu wao ndio waathirika wakuu, sheria taratibu na kanuni wanazijua, hawakufanya lolote zaidi ya kuitisha press conference na kupiga mikelele tuu, unategemea nini?!.

Usalama kwanza, mengine yote baadae!.

Pasco
Eti gaidi akiona vifaru kuna uwezekano wa kuogopa!!!! Si magaid hao ni panya road kumbuka palipo na figusu za kivita ndipo ugaid unapochanua pia wale jamaa wauza silaha nifikir hiyo ni fursa kwao vyama vya siasa hata vingepiga kelele vp bado havina nguvu ya kuitoa ccm iliyojiimarisha ktk matumiz vyombo vya dola huko ndo msaada mkuu wa ccm ulipo unasema had walalamike ndo wasaidiwe ni kweli? Huu ni utani mkubwa
 
Toka tulipokaribisha balozi wa Mayahudi TZ hichi ndicho matakwa yao na mskuma yeye sasa ni bendera tu
 
Mambo yanayohusu ulinzi na usalama ni classified, hayapaswi kupewa media attention, vifaru ni silaha za kivita na sio vifaa vya kutunzia usalama, hivyo ukiona vifaru, ujue tayari taarifa za kiintelijensia zimeishawafikia, na wanausalama makini kote dunia, hujipanga kukinga ni bora kuliko tiba, hivyo vifaru huko ni kwa ajili ya tahadhai kabla ya hatari, kuna mambo fulani kuna magaidi fulani wamepanga kufanya ugaidi fulani, hivyo kitendo tuu cha kuviona vifaru na ulinzi ulioimarishwa, hao magaidi, hawataendelea tena kutekeleza nia zao ovu!.

Kwa hayo yanayotokea kwa vile Wanzanzibari wenyewe wapo na wameyakubali, ulitaka wafanye nini?!. Viongozi sio ni kama hawapo, bali kiukweli hawapo kikatiba na kisheria, muda wao ulikwisha asmi November 4, sasa wapo wapo tuu kama hawapo!. Wana dini pia wapo kuwafikisha watu mbinguni na sio kuwaingiza magaidi ikulu!, taasisi za kiraia zipo kufanya kazi za kiaia na sio kuingilia mambo ya siasa!, taasisi za haki za binadamu zipo na zinasubiri malalamiko yoyote rasmi kuhusu ukiukwaji wa haki za binaadamu, na hakuna malalamiko yoyote so far!, hii inamaanisha watu wote wameridhika na yote yanayotendwa!. Taasisisi za kisheria pia zipo, taratibu za taasisi zozote za kisheria ni kwa watu wenye malalamiko yoyote ya kisheria kuzifuata kuomba msaada wa kisheria, lakini kwa yote yanayotokea Zanzibar, hakuna yoyote aliyechukua hatua yoyote kulalamika popote, hivyo ulitegemea taasisi hizo zifanye nini?!, yaani daktari atoke hospitalini aanze kutembelea majumbani kuulizia wagonjwa?!, kikawaida kama mahali kuna mgonjwa, mgonjwa huyo ndie atakwenda hospitali kufuata tiba na sii vinginevyo!. Vyama vya siasa ndio kabisa, vipo kama havipo kwa sababu wao ndio waathirika wakuu, sheria taratibu na kanuni wanazijua, hawakufanya lolote zaidi ya kuitisha press conference na kupiga mikelele tuu, unategemea nini?!.

Usalama kwanza, mengine yote baadae!.

Pasco


Mbulula kabisa
 
Jamani tuwe wakweli. Hivi hili figisu kalianzisha nani? Hebu kwanza naomba mtafakari haya matokeo yaliyotolewa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar kutoka majimbo 31 kati ya 54 wakati wakiendelea kupokea mengine[Matokeo hayo yaliyokuwa yametangazwa kufikia saa mbili jioni Oktoba 27 ni kama ifuatavyo:
Matokeo ya uchaguzi wa Rais wa Zanzibar (Majimbo31/54)]

Jina Chama Kura Asilimia
Khamis Iddi Lila ACT-W 189 0.1
Juma Ali Khatib ADA-TADEA 93 0.0
Hamad Rashid Mohamed ADC 252 0.1
Said Soud Said AFP 223 0.1
Ali Khatib Ali CCK 240 0.1
Ali Mohamed Shein CCM 139,557 57.9
Mohammed Massoud Rashid CHAUMMA 257 0.1
Seif Sharif Hamad CUF 93,699 38.9
Taibu Mussa Juma DM 118 0.0
Abdalla Kombo Khamis DP 86 0.0
Kassim Bakar Aly JAHAZI 227 0.1
Seif Ali Iddi NRA 63 0.0
Issa Mohammed Zonga SAU 127 0.1
Hafidh Hassan Suleiman TLP 107 0.0
Zanzibar ina jumla ya wapiga kura 503,860 waliojiandikisha kupiga kura, kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar.

Halafu twendeni kwenye matokeo aliyotangaza maalim seif
Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, ameitisha mkutano wa waandishi wa habari na kusema kuwa baada ya chama chake kukusanya fomu zote za matokeo kutoka vituoni, yeye amepata kura 200,007 dhidi ya kura 178,363 za mgombea wa CCM anayetetea nafasi yake, Dk. Ali Mohammed Shein.


Sasa twendeni kwenye tafakuri
1 Tume ilitangaza kuwa wapiga kura wote waliojiandikisha walikuwa 503,860
2. Kwenye majimbo 31 kati ya 54 iliripotiwa kuwa Dr. Shein alipata kura 139,557[57.9%] na Maalim Seif
alipata kura 93,699[38.9]
3 Vyama vingine vidogo vilipata kwa pamoja chini ya asilimia 3 ya kura zote


Alipotangaza ushindi maalim alidai kuwa alipata kura 200,0007 na shein alipata 178,363 hizi hesabu ni kwa zanzibara na pemba.
Hakuna kura zilizoharibika wala kura za vyama vingine


Hivi ndugu zangu hapa ni nani wa kulaumiwa? Hivi mlitaka tume ikubaliane na hesabu za maalimi seif ambazo alidai ni za visiwa vyote 2?

Maoni yangu ni kuwa[naomba msitukane ila mtafakari maana hili ni jamvi la 'those who dare to speak'
Maalim baada ya kuona hali ya matokeo kutoka majimbo 31 hadi tarehe 27 yalionyesha dhahiri kuwa ulikuwepo uwezekano mkubwa kwa chama chake kushindwa na ili afe kiume alipreempt tume kwa kuanza kutangaza yeye wakati akifahamu kuwa kwa sheria zilivyosasa ni tume pekee ambayo inahaki ya kutangaza matokeo.
Kwa.haraka haraka nakupa jawabu mbili tu.

1 Ikiwa wapiga kura kutokana na maneno yako ni 500,000. Kura za Maalim + Dr Shein + Others ni kama 400,000. Kwa hiyo turn up ni 80% sio 100% kama unavyojidai.

2. Utambuwe kuwa matokeo ya Pemba yalikuwa bado hayajatngazwa ambapo Maalim anapata ushindi huko wa 75-85% ya kura zinazopigwa huko.

Nategemea kwa haya mawili yatakutosha
 
Jamani tuwe wakweli. Hivi hili figisu kalianzisha nani? Hebu kwanza naomba mtafakari haya matokeo yaliyotolewa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar kutoka majimbo 31 kati ya 54 wakati wakiendelea kupokea mengine[Matokeo hayo yaliyokuwa yametangazwa kufikia saa mbili jioni Oktoba 27 ni kama ifuatavyo:
Matokeo ya uchaguzi wa Rais wa Zanzibar (Majimbo31/54)]

Jina Chama Kura Asilimia
Khamis Iddi Lila ACT-W 189 0.1
Juma Ali Khatib ADA-TADEA 93 0.0
Hamad Rashid Mohamed ADC 252 0.1
Said Soud Said AFP 223 0.1
Ali Khatib Ali CCK 240 0.1
Ali Mohamed Shein CCM 139,557 57.9
Mohammed Massoud Rashid CHAUMMA 257 0.1
Seif Sharif Hamad CUF 93,699 38.9
Taibu Mussa Juma DM 118 0.0
Abdalla Kombo Khamis DP 86 0.0
Kassim Bakar Aly JAHAZI 227 0.1
Seif Ali Iddi NRA 63 0.0
Issa Mohammed Zonga SAU 127 0.1
Hafidh Hassan Suleiman TLP 107 0.0
Zanzibar ina jumla ya wapiga kura 503,860 waliojiandikisha kupiga kura, kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar.

Halafu twendeni kwenye matokeo aliyotangaza maalim seif
Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, ameitisha mkutano wa waandishi wa habari na kusema kuwa baada ya chama chake kukusanya fomu zote za matokeo kutoka vituoni, yeye amepata kura 200,007 dhidi ya kura 178,363 za mgombea wa CCM anayetetea nafasi yake, Dk. Ali Mohammed Shein.


Sasa twendeni kwenye tafakuri
1 Tume ilitangaza kuwa wapiga kura wote waliojiandikisha walikuwa 503,860
2. Kwenye majimbo 31 kati ya 54 iliripotiwa kuwa Dr. Shein alipata kura 139,557[57.9%] na Maalim Seif
alipata kura 93,699[38.9]
3 Vyama vingine vidogo vilipata kwa pamoja chini ya asilimia 3 ya kura zote


Alipotangaza ushindi maalim alidai kuwa alipata kura 200,0007 na shein alipata 178,363 hizi hesabu ni kwa zanzibara na pemba.
Hakuna kura zilizoharibika wala kura za vyama vingine


Hivi ndugu zangu hapa ni nani wa kulaumiwa? Hivi mlitaka tume ikubaliane na hesabu za maalimi seif ambazo alidai ni za visiwa vyote 2?

Maoni yangu ni kuwa[naomba msitukane ila mtafakari maana hili ni jamvi la 'those who dare to speak'
Maalim baada ya kuona hali ya matokeo kutoka majimbo 31 hadi tarehe 27 yalionyesha dhahiri kuwa ulikuwepo uwezekano mkubwa kwa chama chake kushindwa na ili afe kiume alipreempt tume kwa kuanza kutangaza yeye wakati akifahamu kuwa kwa sheria zilivyosasa ni tume pekee ambayo inahaki ya kutangaza matokeo.
Maalim kujitangazia matokeo yake haiwezi kuzuia Tume kutangaza matokeo halali na ya kweli. Kuna nchi nyingi tu upinzani huwa wanajitokeza na kujitangazia ushindi lakini bado Tume wanatangaza matokeo yao.

Hivi unafikiri kama Tume ingendelea na kumtangaza Shein hili figisu si lingeshakuwa history. Tatizo wamelikoza kwa Mkaa wa Ruvu.

Just imagine, Lowasa alipojaribu kulalamika matokeo baada ya January kutangaza kuwa CCM inashinda kwa 67 % mbona Lubuva alikata kusikiliza na baada ya hapo matokeo yakatangazwa faster faster!!
 
Jamani tuwe wakweli. Hivi hili figisu kalianzisha nani? Hebu kwanza naomba mtafakari haya matokeo yaliyotolewa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar kutoka majimbo 31 kati ya 54 wakati wakiendelea kupokea mengine[Matokeo hayo yaliyokuwa yametangazwa kufikia saa mbili jioni Oktoba 27 ni kama ifuatavyo:
Matokeo ya uchaguzi wa Rais wa Zanzibar (Majimbo31/54)]

Jina Chama Kura Asilimia
Khamis Iddi Lila ACT-W 189 0.1
Juma Ali Khatib ADA-TADEA 93 0.0
Hamad Rashid Mohamed ADC 252 0.1
Said Soud Said AFP 223 0.1
Ali Khatib Ali CCK 240 0.1
Ali Mohamed Shein CCM 139,557 57.9
Mohammed Massoud Rashid CHAUMMA 257 0.1
Seif Sharif Hamad CUF 93,699 38.9
Taibu Mussa Juma DM 118 0.0
Abdalla Kombo Khamis DP 86 0.0
Kassim Bakar Aly JAHAZI 227 0.1
Seif Ali Iddi NRA 63 0.0
Issa Mohammed Zonga SAU 127 0.1
Hafidh Hassan Suleiman TLP 107 0.0
Zanzibar ina jumla ya wapiga kura 503,860 waliojiandikisha kupiga kura, kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar.

Halafu twendeni kwenye matokeo aliyotangaza maalim seif
Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, ameitisha mkutano wa waandishi wa habari na kusema kuwa baada ya chama chake kukusanya fomu zote za matokeo kutoka vituoni, yeye amepata kura 200,007 dhidi ya kura 178,363 za mgombea wa CCM anayetetea nafasi yake, Dk. Ali Mohammed Shein.

Sasa twendeni kwenye tafakuri
1 Tume ilitangaza kuwa wapiga kura wote waliojiandikisha walikuwa 503,860
2. Kwenye majimbo 31 kati ya 54 iliripotiwa kuwa Dr. Shein alipata kura 139,557[57.9%] na Maalim Seif
alipata kura 93,699[38.9]
3 Vyama vingine vidogo vilipata kwa pamoja chini ya asilimia 3 ya kura zote

Alipotangaza ushindi maalim alidai kuwa alipata kura 200,0007 na shein alipata 178,363 hizi hesabu ni kwa zanzibara na pemba.
Hakuna kura zilizoharibika wala kura za vyama vingine

Hivi ndugu zangu hapa ni nani wa kulaumiwa? Hivi mlitaka tume ikubaliane na hesabu za maalimi seif ambazo alidai ni za visiwa vyote 2?

Maoni yangu ni kuwa[naomba msitukane ila mtafakari maana hili ni jamvi la 'those who dare to speak'
Maalim baada ya kuona hali ya matokeo kutoka majimbo 31 hadi tarehe 27 yalionyesha dhahiri kuwa ulikuwepo uwezekano mkubwa kwa chama chake kushindwa na ili afe kiume alipreempt tume kwa kuanza kutangaza yeye wakati akifahamu kuwa kwa sheria zilivyosasa ni tume pekee ambayo inahaki ya kutangaza matokeo.
Mkuu hizo hesabu sio sahihi. Maalim ametangaza kipata kura 200077 na dr shein kupata 178363. Kwa pamoja jumla ni kwenye laki tatu hivi. Hakikisha tena hesabu zako
 
Mambo yanayohusu ulinzi na usalama ni classified, hayapaswi kupewa media attention, vifaru ni silaha za kivita na sio vifaa vya kutunzia usalama, hivyo ukiona vifaru, ujue tayari taarifa za kiintelijensia zimeishawafikia, na wanausalama makini kote dunia, hujipanga kukinga ni bora kuliko tiba, hivyo vifaru huko ni kwa ajili ya tahadhai kabla ya hatari, kuna mambo fulani kuna magaidi fulani wamepanga kufanya ugaidi fulani, hivyo kitendo tuu cha kuviona vifaru na ulinzi ulioimarishwa, hao magaidi, hawataendelea tena kutekeleza nia zao ovu!.

Kwa hayo yanayotokea kwa vile Wanzanzibari wenyewe wapo na wameyakubali, ulitaka wafanye nini?!. Viongozi sio ni kama hawapo, bali kiukweli hawapo kikatiba na kisheria, muda wao ulikwisha asmi November 4, sasa wapo wapo tuu kama hawapo!. Wana dini pia wapo kuwafikisha watu mbinguni na sio kuwaingiza magaidi ikulu!, taasisi za kiraia zipo kufanya kazi za kiaia na sio kuingilia mambo ya siasa!, taasisi za haki za binadamu zipo na zinasubiri malalamiko yoyote rasmi kuhusu ukiukwaji wa haki za binaadamu, na hakuna malalamiko yoyote so far!, hii inamaanisha watu wote wameridhika na yote yanayotendwa!. Taasisisi za kisheria pia zipo, taratibu za taasisi zozote za kisheria ni kwa watu wenye malalamiko yoyote ya kisheria kuzifuata kuomba msaada wa kisheria, lakini kwa yote yanayotokea Zanzibar, hakuna yoyote aliyechukua hatua yoyote kulalamika popote, hivyo ulitegemea taasisi hizo zifanye nini?!, yaani daktari atoke hospitalini aanze kutembelea majumbani kuulizia wagonjwa?!, kikawaida kama mahali kuna mgonjwa, mgonjwa huyo ndie atakwenda hospitali kufuata tiba na sii vinginevyo!. Vyama vya siasa ndio kabisa, vipo kama havipo kwa sababu wao ndio waathirika wakuu, sheria taratibu na kanuni wanazijua, hawakufanya lolote zaidi ya kuitisha press conference na kupiga mikelele tuu, unategemea nini?!.

Usalama kwanza, mengine yote baadae!.

Pasco


cuf magaidi, ccm malaika nimekuelewa pasco aka ....
 
Wakuu mna uhuru wa kuendesha mjadala kuhusu Zanzibar tani yenu. Lakini ukweli unabaki palepale: uchaguzi utafanyika, CCM watashinda kiti cha urais na maisha yataendelea kama kawaida. Kama falsafa inavyozidi kuthibitisha: watu hupata serikali wanayoistahili. Hakuna kitu kama "bahati mbaya".
 
Mwaka 1984 hali ya kuchafuka Znz ilipo tokea ..hali a,bayo rais wa Znz JUmbe alihusika kabisa kutaka kujaribu kujitoa ndani ya Muungano...alikua na kundi lake la kiroboto. Vijana wengi humu hawakumbuki ila hali znz ilikua mbaya watu walichukia sana utawala na muungano. Na kampeni ile ya kuuchukia muungano ilikua ikuungwa mkono na Rais mwenyewe na baadhi ya mawaziri aliwemo Waziri Kiongozi Ramadhan Haji na mwanasheria wa Znz Wolfang Dourado....

Znz hali ilikua very tense na isio tabirika...hali ya kuwa na rais ambaye ameasi katiba ....lakini Mwalimu hakuwahi kuwapelekea wapemba na wazanzibari vifaru , askari au mabunduki....
Mimi nakumbuka kabisa nikiwa National service znz jku wakati ule kama service man hatukuwahi kutika kwenda uraiani . Majeshi yote yulikua kambini zaidi ya kuwa na full alert basi ...
Na mjini hakukuwa na majeshi wala bifaru na haikutumika bitisho vyovyote..
Alitumia siasa akamuaondoa jumbe na wengine basi hali ikarudi na kutulia kabisa znz kwani mwalimu alijua siasa akwapelekea znz Mwinyi na Maaalim Seif na hao wakaiyuliza znz wakasahau yote ya kiroboto..

Mwalimu alikua kiongozi ..sasa nikiangalia hali ya majeshi kutolewa kambini na kupelekwa na kutembea uraiani kama kuna mapinduzi ya kijeshi...naamini nchi imekosa uongozi ...tuna tibu maradhi yetu kwa nguvu zaidi badala ya busara na hekima....tuna kasoro...kubwa sana na nchi imekosa kabisa mtu wa kumrithi mwalimu ..Naamini angekua hai kwa hili...angewapigavbakora wote hawa watu ccm..kabisa kabisa...yaani utie jeshi utembeze mitaani uraiani ?

Baada ya mutiny ile ya 1964...Mwalimu aliona aibu san kuona baada ya uhuru amuombe Malkia aje tena amsaidie kuzima uasi..hili lilimsononesha sana..
Aliamua kulipika upya jeshi la wananchi na likawa na miiko yake na likawa kazi yake kuu ni kulinda mipaka ya nchi na usalam wa raia.
Ccm sasa hawafati miiko ya kuasisiwa JWTZ...imeligeuza mali ya chama ...
Moja ya sifa kuu ya mwalimu nii hii ya kutolitumia jeshi kwa mambo haya ya kiraia.....viongozi wetu hawana
 
Mambo yanayohusu ulinzi na usalama ni classified, hayapaswi kupewa media attention, vifaru ni silaha za kivita na sio vifaa vya kutunzia usalama, hivyo ukiona vifaru, ujue tayari taarifa za kiintelijensia zimeishawafikia, na wanausalama makini kote dunia, hujipanga kukinga ni bora kuliko tiba, hivyo vifaru huko ni kwa ajili ya tahadhai kabla ya hatari, kuna mambo fulani kuna magaidi fulani wamepanga kufanya ugaidi fulani, hivyo kitendo tuu cha kuviona vifaru na ulinzi ulioimarishwa, hao magaidi, hawataendelea tena kutekeleza nia zao ovu!.

Kwa hayo yanayotokea kwa vile Wanzanzibari wenyewe wapo na wameyakubali, ulitaka wafanye nini?!. Viongozi sio ni kama hawapo, bali kiukweli hawapo kikatiba na kisheria, muda wao ulikwisha asmi November 4, sasa wapo wapo tuu kama hawapo!. Wana dini pia wapo kuwafikisha watu mbinguni na sio kuwaingiza magaidi ikulu!, taasisi za kiraia zipo kufanya kazi za kiaia na sio kuingilia mambo ya siasa!, taasisi za haki za binadamu zipo na zinasubiri malalamiko yoyote rasmi kuhusu ukiukwaji wa haki za binaadamu, na hakuna malalamiko yoyote so far!, hii inamaanisha watu wote wameridhika na yote yanayotendwa!. Taasisisi za kisheria pia zipo, taratibu za taasisi zozote za kisheria ni kwa watu wenye malalamiko yoyote ya kisheria kuzifuata kuomba msaada wa kisheria, lakini kwa yote yanayotokea Zanzibar, hakuna yoyote aliyechukua hatua yoyote kulalamika popote, hivyo ulitegemea taasisi hizo zifanye nini?!, yaani daktari atoke hospitalini aanze kutembelea majumbani kuulizia wagonjwa?!, kikawaida kama mahali kuna mgonjwa, mgonjwa huyo ndie atakwenda hospitali kufuata tiba na sii vinginevyo!. Vyama vya siasa ndio kabisa, vipo kama havipo kwa sababu wao ndio waathirika wakuu, sheria taratibu na kanuni wanazijua, hawakufanya lolote zaidi ya kuitisha press conference na kupiga mikelele tuu, unategemea nini?!.

Usalama kwanza, mengine yote baadae!.

Pasco
Itelenjensia hipi nyie mnahamu na vita kama mnahuwezo peleka Somalia jeshi lenu uone kama awajafa kama kuku we unapeka vifuru kwa watu amabao hawana siraha
 
Mambo yanayohusu ulinzi na usalama ni classified, hayapaswi kupewa media attention, vifaru ni silaha za kivita na sio vifaa vya kutunzia usalama, hivyo ukiona vifaru, ujue tayari taarifa za kiintelijensia zimeishawafikia, na wanausalama makini kote dunia, hujipanga kukinga ni bora kuliko tiba, hivyo vifaru huko ni kwa ajili ya tahadhai kabla ya hatari, kuna mambo fulani kuna magaidi fulani wamepanga kufanya ugaidi fulani, hivyo kitendo tuu cha kuviona vifaru na ulinzi ulioimarishwa, hao magaidi, hawataendelea tena kutekeleza nia zao ovu!.

Kwa hayo yanayotokea kwa vile Wanzanzibari wenyewe wapo na wameyakubali, ulitaka wafanye nini?!. Viongozi sio ni kama hawapo, bali kiukweli hawapo kikatiba na kisheria, muda wao ulikwisha asmi November 4, sasa wapo wapo tuu kama hawapo!. Wana dini pia wapo kuwafikisha watu mbinguni na sio kuwaingiza magaidi ikulu!, taasisi za kiraia zipo kufanya kazi za kiaia na sio kuingilia mambo ya siasa!, taasisi za haki za binadamu zipo na zinasubiri malalamiko yoyote rasmi kuhusu ukiukwaji wa haki za binaadamu, na hakuna malalamiko yoyote so far!, hii inamaanisha watu wote wameridhika na yote yanayotendwa!. Taasisisi za kisheria pia zipo, taratibu za taasisi zozote za kisheria ni kwa watu wenye malalamiko yoyote ya kisheria kuzifuata kuomba msaada wa kisheria, lakini kwa yote yanayotokea Zanzibar, hakuna yoyote aliyechukua hatua yoyote kulalamika popote, hivyo ulitegemea taasisi hizo zifanye nini?!, yaani daktari atoke hospitalini aanze kutembelea majumbani kuulizia wagonjwa?!, kikawaida kama mahali kuna mgonjwa, mgonjwa huyo ndie atakwenda hospitali kufuata tiba na sii vinginevyo!. Vyama vya siasa ndio kabisa, vipo kama havipo kwa sababu wao ndio waathirika wakuu, sheria taratibu na kanuni wanazijua, hawakufanya lolote zaidi ya kuitisha press conference na kupiga mikelele tuu, unategemea nini?!.

Usalama kwanza, mengine yote baadae!.

Pasco
Kutafata usalama sehemu ambayo watu hawana amani ni huendawazimu
 
Kwanza kuna matukio hayapati nafasi katika vyombo vya habari vingi kuhusu kile kinachoendelea Zanzibar. Zikiwa zimebaki siku sita tu kufanyika kile kinaitwa uchaguzi wa marudio hali ya Zanzibar ni Aibu.

Kwa sasa kumepelekwa vyombo vya ulinzi kwa wingi wakiwemo wanajeshi hasa kisiwani pemba na tayari vyombo hivyo vinaonekana wazi wazi kuleta athari. Kumeripotiwa taarifa za vifaru vya jeshi kuonekana vikitembea barabarani mchana kweupe na wananchi kuingiwa hofu.

Hali hii hujitokeza Zanzibar pekee katika Tanzania hii. Lengo lake halijulikani kama ni huu uchaguzi wa marudio au kuna zaidi ya uchaguzi.

Kuna mpasuko mkubwa wa kijamii. Imefika wakati hasa kisiwani Pemba watu wameshaanza kususiana mambo mbali mbali.

Mifano.

i. Kususiwa baadhi ya wananchi kusafirishwa kwa kivuko kutoka kisiwa kidogo (Kisiwa Panza) kwenda chokocho. Ifahamike mgogoro huu unafukuta na unahusishwa na siasa za uchaguzi wa marudio.

ii Kususiwa kwa baadhi ya mambo ya kijamii ikiwemo maziko na shughuli ya harusi. Maeneo mbali mbali yamejitokeza kwa njia baridi huko Pemba.

iii. Kuna taarifa za viongozi wa kitaifa Zanzibar (Sitaji Majina) kususiwa misikiti zaidi ya mara mbili pale inapopatikana habari kuwa wanakwenda kuswali jamii inasusa kwenda na kuwaachia viongozi wa serikali peke yao. Zipo taarifa ni hapa majuzi kiongozi mmoja alisusiwa ufunguzi wa msikiti hali iliyolazimu kuletwa askari wa kikosi fulani kuongeza idadi ya watu.

iv Kuzomewa baadhi ya viongozi wa kitaifa huko kisiwani Pemba na kususiwa kwenye shughuli za
maendeleo

Kwa ufupi kuna hali mbaya Zanzibar imeanza kujitokeza na inatarajiwa kukua na kuongeza uhasama zaidi. Watu wameanza kuchoma nyumba moto na baraza za vyama vya siasa.

Kuna hali ya kutiliana mashaka na ukimya wa kutisha unaoashiria shari, kuna kutishana kwa kutumia vyombo vya dola. Kumeanza kupigwa marufuku mikusanyiko katika baadhi ya maeneo Zanzibar.

Kuna masuali ya kujiuliza Nini hatima ya Zanzibar ikiwa hali iko hivi sasa kabla ya kufanyika uchaguzi wa marudio uliosusiwa na wadau wakubwa wa Zanzibar? jee Kutakuwa na suluhu yoyote?

Haya yanatokea viongozi ni kama hawapo, wana dini ni kama hawapo, taasisi za kiraia ni kama hazipo, taasisi za haki za binadamu ni kama hazipo, taasisisi za kisheria ni kama hazipo, vyama vya siasa ni kama havipo na wengineo.

Tutegemee nini? hii aibu kwa nchi
  1. PEMBA: THE FIRE NEXT TIME
    220px-FireNextTime.JPG


    Wakati James Baldwin anaandika maneno haya ambayo ndiyo jina la kitabu chake hiki mashuhuri kuhusu ubaguzi Marekani, nchi ile ilikuwa ikipitia kipindi kigumu sana katika historia yake. Jamii moja ilikuwa ikibaguliwa na kufanyiwa kila aina ya madhila kuanzia kupigwa na polisi, kusakasiwa mbwa, kumwagiwa maji ya washawasha nk. Nilipoziona picha hizo hapo chini kutoka Pemba fikra yangu ya kwanza ilikwenda kwa kasi ya ajabu kwa mwandishi huyu nguli James Baldwin na kitabu chake hicho - The Fire Next Time...

    2016%2B-%2B1


    upload_2016-3-15_20-58-55.gif


    upload_2016-3-15_20-58-55.gif



    upload_2016-3-15_20-58-55.gif


    upload_2016-3-15_20-58-55.gif


    upload_2016-3-15_20-58-55.gif


    2016%2B-%2B1

    Posted 7 hours ago by Mohamed Said
    Labels: makala
Loading
 
Mi siogopi jina lako hata kidogo,kwa kukujibu,kama hoja ni kutawala tu,Tanzania iliitawala kwa muda Uganda mara baada ya Vita ya ukombozi. Pia Tanzania ilitawala Anjuani kabla hawamuweka Rais wanayemtaka na pote huko palitawaliwa na maafisa wa jwtz wenye vyeo vya kanali. Sheli sheli pia ilishawahi kushikwa na Tanzania kwa miezi kama mitatu,kwahiyo sioni la ajabu as long kwamba Zanzibar ina undergo security unrest kuelekea uchaguzi wa marudio[emoji4]

Unaonaje ikitokea nchi nyingne ikaja kuitwala Tanzania utafurahi?
 
Mambo yanayohusu ulinzi na usalama ni classified, hayapaswi kupewa media attention, vifaru ni silaha za kivita na sio vifaa vya kutunzia usalama, hivyo ukiona vifaru, ujue tayari taarifa za kiintelijensia zimeishawafikia, na wanausalama makini kote dunia, hujipanga kukinga ni bora kuliko tiba, hivyo vifaru huko ni kwa ajili ya tahadhai kabla ya hatari, kuna mambo fulani kuna magaidi fulani wamepanga kufanya ugaidi fulani, hivyo kitendo tuu cha kuviona vifaru na ulinzi ulioimarishwa, hao magaidi, hawataendelea tena kutekeleza nia zao ovu!.

Kwa hayo yanayotokea kwa vile Wanzanzibari wenyewe wapo na wameyakubali, ulitaka wafanye nini?!. Viongozi sio ni kama hawapo, bali kiukweli hawapo kikatiba na kisheria, muda wao ulikwisha asmi November 4, sasa wapo wapo tuu kama hawapo!. Wana dini pia wapo kuwafikisha watu mbinguni na sio kuwaingiza magaidi ikulu!, taasisi za kiraia zipo kufanya kazi za kiaia na sio kuingilia mambo ya siasa!, taasisi za haki za binadamu zipo na zinasubiri malalamiko yoyote rasmi kuhusu ukiukwaji wa haki za binaadamu, na hakuna malalamiko yoyote so far!, hii inamaanisha watu wote wameridhika na yote yanayotendwa!. Taasisisi za kisheria pia zipo, taratibu za taasisi zozote za kisheria ni kwa watu wenye malalamiko yoyote ya kisheria kuzifuata kuomba msaada wa kisheria, lakini kwa yote yanayotokea Zanzibar, hakuna yoyote aliyechukua hatua yoyote kulalamika popote, hivyo ulitegemea taasisi hizo zifanye nini?!, yaani daktari atoke hospitalini aanze kutembelea majumbani kuulizia wagonjwa?!, kikawaida kama mahali kuna mgonjwa, mgonjwa huyo ndie atakwenda hospitali kufuata tiba na sii vinginevyo!. Vyama vya siasa ndio kabisa, vipo kama havipo kwa sababu wao ndio waathirika wakuu, sheria taratibu na kanuni wanazijua, hawakufanya lolote zaidi ya kuitisha press conference na kupiga mikelele tuu, unategemea nini?!.

Usalama kwanza, mengine yote baadae!.

Pasco
Hongera mkuu Pasco kwa ufafanuzi mzuri na wa kizalendo
 
POLENI sana kwa yote hayo. Lakini kwa kiwango kikubwa uwepo wa TPDF huko Zanzibar ni jambo jema kabisa tena basi msiwe na wasiwasi kabisa. Ni waovu tu wataogopa TPDF, watu wema kamwe hawawezi kuogopa jeshi hilo na ambalo ni la ulinzi wa wananchi. Wale wanaoweka X na kuchoma nyumba za wenzao ndio wataogopa lakini sio wale raia wema.
Hata raia wa Central Africa Republic waliambiwa hivyo hivyo kuhusu majeshi yakulinda amani ya Umoja wa Mataifa, ulizia kilichotekea? Mamia ya watoto kubakwa na wengine kulawatiwa huku UN ikijitutumua kuchukua hatua za kisiasa. Ulizia kilichotokea ZNZ 2001, raia waliambiwa hivyo hivyo kuhusu hao hao wanaoitwa TPDF walinda amani, nenda sehemu inaitwa Kisiwani (hili ni jina la kijiji) Pemba, achilia mbali wizi uliofanywa na hao unaowaita TPDF, waliwazini watoto wa watu wengine kufanyia vitendo vya unyanyasaji mbele ya familia zao. Unasemaje apo? Binafsi nlishakutana na member mmoja wa TPDF akiomba apangiwe kazi ZNZ huku akisema atapata nafasi ya kufanya mapenzi na watoto wa Kiarabu kwa sababu anaishia kuwaona tu, unasemaje apo? Ni kweli TPDF wanatakiwa kufanya hivyo ambavyo wewe unafikiria, lakini swali ni Je! Wanafanya hivyo au wanaishia kufanya kazi za kisiasa kwa mgongo wa TPDF. Tutafakari pamoja.
 
Back
Top Bottom