Mwanza ni jiji la pili kwa ukubwa ukiacha na Dar es Salaam ambalo limeshika namba moja.
Lakini;
WATU
Ushamba wa watu hii ni pie 22/7 inajulikana
MISOSI
Hapa ndpo shida ilipo, aisee watu wa huku hawajui kupika yani hapa nawapa zero.
Watu wa huku kwenye kuandaa misosi wako rafu na hawajui kabisa yaani wanachojua ni kuchemsha tu vyakula karibia vyote ila ndiyo waandaji ndiyo shida hiki kimeniuzi sana.
Wao wenyeji hawaoni tofauti. Sasa kwa watu ambao wameishi mikoa tofauti tofauti lazima wamind kama ushaishi Pwani, Tanga, Dar hata Dodoma, Iringa, Mbeya, Morogoro wapo vizuri ila siyo huku.
Uzuri ni samaki tu! Unaagiza wali samaki unaletewa samaki aliyechemshwa na wali mkavu hapo washamaliza. Yaani unajiuliza ungeagiza mchemsho tu! Unless uende kula mahotel makubwa sana ila siyo restaurant au migahawa.
BIASHARA
Biashara na mzunguko wa hela unaonekana. Upo
yaani kama misosi inachemshwa ili mradi tu na bei juu bado watu wananunua, pesa ipo
na biashara nyingne naona zinaenda.
Ila kama we mpenda kula usije huku labda ujie samaki tu.