Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,252
- 113,645
View: https://youtu.be/ldflyzj-0S4?si=KSG3nRgnKOUhTRrM
CCM wenye akili kidogo ndo wanapenda mambo kama haya sasa - kuongoza watu walio wajinga na wapumbavu.
Ni vigumu sana kwa mtu mwenye akili zake timamu, mwenye busara na hekima tu za kawaida, kufanya upumbavu wa kugalagala chini mbele ya viongozi.
Na ithibati ya kuthibitisha kwamba hao viongozi wachache wa CCM walio na vijiakili kidogo kuwa wanapenda kuona mambo kama hayo toka kwa watu wanaowaongoza, ni ukimya wao dhidi ya huo upumbavu.
Mtu mwenye akili akiona watu wapumbavu na walio wajinga wakifanya mambo ya kipumbavu na kijinga, ana wajibu wa kimaadili wa kuyakemea na kuyapinga na kutoa fundisho kuwa hayo mambo si sawa.
Kwa vile haya mambo yanajirudia rudia sana, nashawishika kabisa kuamini kuwa viongozi wa CCM wanayapenda.
Wangekuwa wanayapinga, yasingekuwa yanajirudia rudia sehemu mbalimbali nchini.
CCM ni janga kwa mustakabali wa nchi.
Lakini janga kubwa zaidi ni idadi ya watu walio wajinga na walio wapumbavu.