Companero
Platinum Member
- Jul 12, 2008
- 5,609
- 1,731
Hoja kama hoja nimeipenda ila comment zako zinawalakini maana ukishaanza kutaja ukanda hapa maana yake unataka sasa tuingize rasimi kwenye katiba kuwa utawala wa nchi yetu niwakupokezana kikanda haijalishi sifa za mtu kiongozi mwenyewe, hii ni hatari sana.
Itakuwaje nyanda za juu kusini nao wakikomaa kuwa lazima rais ajaye atoke huko na kanda yenye neema ya ziwa victoria wakasema wanamtaka Magufuli, hapo si ndio mwanzo wa balaa! Take control of your comment mkuu
Ngoma tunaicheza kwa viuno na mabega, sii ujaona kijiwe kilivyo noga!...Lowassa ni maarufu kuliko Sitta ndani ya chama na nje ya chama hilo usijidanganye. Leo hii EL ikisimama na Sitta atamtoa nje kwa sababu Sitta hana mbinu za ushindi.. Kumbuka tu kwamba hata Uspika alipigwa changa la macho na EL..
Hivi unafikiri nguvu kubwa unayofanyika kumdhalilisha JK ina lengo gani? yaani leo EL ana uchungu sana na nchi yetu inakokwenda kuliko alivyokuwa waziri na waziri mkuu..tena watu wako radhi kumsamehe wengine wakidai arudi madarakani. Halafu JK amekaa kimya hata kujitetea hana moja isipokuwa wasizungumze CDM...Uchaguzi ulopita viongozi karibu wote walimkimbia JK akabakia nani? - EL na familia ya JK! EL ndiye aliyechakachua majina ya wagombea na kadhalika, hawa kweli maadui jamani au mnajichanganya...
Hapa ndipo tunapotofautiana Mkuu, yaani Lowassa maarufu kuliko Sitta!! Yes and No. Lowassa maarufu kwa uzuri kwa anaowalipa lakini si kwa umma, labda wale wanaotengenezwa kama wale wanafunzi wa UDSM waliomfuata awasaidie kutatua tatizo la mikopo. Nilishasema SI Unit ya ufisadi ni Lowassa, lakini huwezi kumfananisha na Sitta hasa katika umma unaopenda haki hata kama Sitta ana udhaifu wake. Kwa suala la mbinu, yes Lowassa ana mbinu na kubwa ya mbinu zake ni kutumia udhaifu wetu wa kupenda mno vya dezo bila kufanya kazi na hivyo kununua kila aliye mbele yake, ukiacha wachache wenye misimamo. Kwamba atashinda CCM, si ajabu maana CCM wengi wameingia katika siasa kwa rushwa na hadi sasa maisha yao yote bila rushwa hayaendi, hawasomeshi watoto bila rushwa na wengine hata kula yao ni kwa rushwa, hawana kazi na wenye kazi ni kubangaiza ama kujibanza kwenye vijiwe ama vijimigahawa kama Mwenyekiti wa UVCCM wa Arusha anayeishi kwa Mzungu. Huo ndio ukweli watu kama Hamisi Mgeja hana kazi kutwa hakai Shinyanga anazurura mara atumie timu ya Kahama kula fedha za Vodacom za ligi hadi timu ikashuka, mara sasa atumie uenyekiti na watu kama Millya na Mgeja ni wengi CCM. Wako vijana wazuri na wenye uwezo ktk kambi ya Lowassa, hao naamini akianguka watasonga mbele maana wana maono, si wadandiaji wana mikakati na wana akili, lakini si wengi ni wachache sana na hata EL hawaamini sana japo anawatumia.Lowassa ni maarufu kuliko Sitta ndani ya chama na nje ya chama hilo usijidanganye. Leo hii EL ikisimama na Sitta atamtoa nje kwa sababu Sitta hana mbinu za ushindi.. Kumbuka tu kwamba hata Uspika alipigwa changa la macho na EL..
Hapa ndipo tunapotofautiana Mkuu, yaani Lowassa maarufu kuliko Sitta!! Yes and No. Lowassa maarufu kwa uzuri kwa anaowalipa lakini si kwa umma, labda wale wanaotengenezwa kama wale wanafunzi wa UDSM waliomfuata awasaidie kutatua tatizo la mikopo. Nilishasema SI Unit ya ufisadi ni Lowassa, lakini huwezi kumfananisha na Sitta hasa katika umma unaopenda haki hata kama Sitta ana udhaifu wake. Kwa suala la mbinu, yes Lowassa ana mbinu na kubwa ya mbinu zake ni kutumia udhaifu wetu wa kupenda mno vya dezo bila kufanya kazi na hivyo kununua kila aliye mbele yake, ukiacha wachache wenye misimamo. Kwamba atashinda CCM, si ajabu maana CCM wengi wameingia katika siasa kwa rushwa na hadi sasa maisha yao yote bila rushwa hayaendi, hawasomeshi watoto bila rushwa na wengine hata kula yao ni kwa rushwa, hawana kazi na wenye kazi ni kubangaiza ama kujibanza kwenye vijiwe ama vijimigahawa kama Mwenyekiti wa UVCCM wa Arusha anayeishi kwa Mzungu. Huo ndio ukweli watu kama Hamisi Mgeja hana kazi kutwa hakai Shinyanga anazurura mara atumie timu ya Kahama kula fedha za Vodacom za ligi hadi timu ikashuka, mara sasa atumie uenyekiti na watu kama Millya na Mgeja ni wengi CCM. Wako vijana wazuri na wenye uwezo ktk kambi ya Lowassa, hao naamini akianguka watasonga mbele maana wana maono, si wadandiaji wana mikakati na wana akili, lakini si wengi ni wachache sana na hata EL hawaamini sana japo anawatumia.
Kwanini watu wanafikiri Lowassa ana clout ya kuwashawishi wananchi wa Tanzania kuwa hayuko jinsi anavyodhaniwa au kujulikana? Ni kweli wapo watu wanaoweza kuapa kwa Lowassa lakini kweli hivi akisimama na kuanza kampeni ataahidi nini Watanzania ambacho hakijawahi kuahidiwa na viongozi wenzake wa CCM waliopo au waliopita? Naombeni kitu japo kimoja tu ambacho EL anaweza kusema ambacho hakijawahi kusemwwa na CCM.
Kwanini watu wanafikiri Lowassa ana clout ya kuwashawishi wananchi wa Tanzania kuwa hayuko jinsi anavyodhaniwa au kujulikana? Ni kweli wapo watu wanaoweza kuapa kwa Lowassa lakini kweli hivi akisimama na kuanza kampeni ataahidi nini Watanzania ambacho hakijawahi kuahidiwa na viongozi wenzake wa CCM waliopo au waliopita? Naombeni kitu japo kimoja tu ambacho EL anaweza kusema ambacho hakijawahi kusemwwa na CCM.
leo wamekaa hivi kuna jipya hapo kweli
![]()
Kaitwa kaambiwa aachie ujumbe wa NEC abaki na ubunge kagoma.
wewe halisi unatoa coment zako kwa hisia za chuki huku ukweli unajua moyoni, tutawapiga pini hamtaamini tunarudi na ushindi wa ugenini toka dodoma na tunajiaandaa kuwapokea kwa kishindo hapa chuga town. tulifurahi pamoja, tulihuzika pamoja, tutafight pamoja na pamoja tutashinda. msipime kina cha bahari kwa kuingiza mguu