General Mangi
JF-Expert Member
- Dec 21, 2013
- 15,316
- 23,186
mkuu ushapoteza kibarua cha watu, huyo jamaa atafukuzwa kazi.Mimi nilikua hapo Kurasini wiki iliyopita na ninamshukuru Mungu mambo yalienda faster kuliko nilivyo fikiria mwanzo.
Ni kweli kigezo kimojawapo katika maombi ya Passport ni kua na kitambulisho cha Uraia.
Mimi sikua nacho na nilienda kumuona Commissioner wa Passort au tuseme Supervisor wao alinishauri niende NIDA nikapewe barua itakayothibitisha kua kweli nimeshafanya process zote za kitambulisho ila bado nasubiria kitambulisho. Kweli nilienda NIDA nikawaelezea na siku hiyo hiyo walinipa barua yenye namba yangu ya Kitambulisho cha Uraia na nikarudi kwa kamishina wa Passport (supervisor) akalipitisha ombi langu na ndani ya siku mbili Passport yangu ilikua tayari.
Pia kuna jamaa pia hakua na hicho Kitambulisho lakini alikua kapata safari ya haraka alimuona huyo Msimamizi akapitisha maombi yake na alipata Passport kesho yake.
Hivyo nakushauri nenda kamuone Kamishina wa Passport (Msimamizi mweleze hapo yote atakusaidia ni mtu mzuri sana hana longolongo. Usiishie kwa hawa wa mwanzoni wao wanafuata maelekezo kama Maroboti yaani sasa hv kama una vigezo vyote Passport ni ndani ya siku mbili mpaka tano yaani sio Issue tena.
Bora ungemfata PM