Killi Music Awards

Killi Music Awards

huyo Mo Music mshamba kwel anajidai ameshakua star wa kususia vitu wakati bado alfajiri kabisa. Nina uhakika ata angewekwa kwenye hicho kipengele angeburuzwa na Baraka Da Prince coz dogo yupo njema kuliko yeye.
Anawasikiliza XXL wale hawana cha kupoteza.

Asijilinganishe na Dully yule nguli long time kwenye game.

Huyo mtoto ni mjinga anashindwa kujua kuwa wananchi ndio wamependekeza majina na wao ndio walio mpigia kura chache ndio maana hayupo....
Na yeye aka anzishe za kwakwe kama H baba! Mimi mwenyewe si kumpendekeza na sikuweza kumpendekeza kwa ule wimbo mmoja!
 
Me pia namtia king kura yangu chap.

Huu mwaka ni wa kiba, nathubutu kusema hakuna wimbo bora tangu tumepata uhuru kama wimbo wa Mwana, huu wimbo utampa kiba tuzo nyingi, sema video ndiyo iliharibu kidogo ila na video ingekidhi matarajio ya wengi na hakika kiba angebeba hadi tuzo za Taarabu na zuku japo siyo nominee huko.
 
We nawe sijui umekula maharage ya wapi? Unaiaibisha JF, unaibisha members wote, hufai wewe, kalale mzee.

Hivi hujui kuwa Mo music ni msomi? Anachukua bachelor SAUT kwahiyo ana ufahamu na sio mtu wa kupelekeshwa kama wasanii wa Form2.

ulitaka atokee kwenye vipengele vyote ata vya taarabu kisa yeye msomi mkuu?
 
Mmmh...Ilo nalo n Wazo Zur pia. Ni kwel lakn Mimi stak kuamin kama Mo music hakupigiwa kura..

alipigiwa ndo manake yupo kipengele kingine ila utashi pia utumike. basata wajipange
 
Huu mwaka ni wa kiba, nathubutu kusema hakuna wimbo bora tangu tumepata uhuru kama wimbo wa Mwana, huu wimbo utampa kiba tuzo nyingi, sema video ndiyo iliharibu kidogo ila na video ingekidhi matarajio ya wengi na hakika kiba angebeba hadi tuzo za Taarabu na zuku japo siyo nominee huko.

Opinion evidence is not admissible
 
am glad wamemkumbuka Belle9.... jamani Jux naye yupo??? As far as i know, Vanessa Mdee bado ni chipukizi..
 
Huyu dogo anaanza kulewa sifa sasa.Hizi ndio tuzo za kwanza kwake tokea aanze mziki na hata hivyo kapata nomination moja sio mbaya.
Sasa Mavoko aseme vipi? Ameanza muziki siku nyingi na hajawahi kutoa nyimbo mbaya hata moja.Tena nyingine zimewahi kuwa kama nyimbo za taifa mf. Roho yangu.
Hapo sijasema kuhusu belle 9.

Kwanza huyo dogo hastahili hata hiyo tunzo na ni haki yake kutokuwepo...ali bahatisha wimbo mmoja na kila alio jaribu haukuwa hit song! Naona kakosa busara kabisa ni wazi ana jichimbia kaburi la kimziki kabisa! Alitakiwa kutununia sisi ambao hatukumpendekeza sio Kil au Basata!
Akamuulize H baba yuko wapi pamoja na kuchanganyikiwa hadi kuanzisha tunzo zake na familia yake? Huyu dogo si mvumilivu kabisa hivi Bell 9 asemeje....
 
Beka title anastahili kuwepo jamaa anajua sana, labda kwa hao wengine. Too bad wamemuacha Mo music

Hivi ulichukua muda wako kupendekeza jina lake au una laumu tuu..?Wananchi ndio wamewakataa sio Basata au Kil
 
Huyu dogo anaanza kulewa sifa sasa.Hizi ndio tuzo za kwanza kwake tokea aanze mziki na hata hivyo kapata nomination moja sio mbaya.
Sasa Mavoko aseme vipi? Ameanza muziki siku nyingi na hajawahi kutoa nyimbo mbaya hata mojao.Tena nyingine zimewahi kuwa kama nyimbo za taifa mf. Roho yangu.
Hapo sijasema kuhusu belle 9.

huyo mtoto kumbe mjinga hivo, nilikuwa namtetea ila hapa simsapoti, kususasusa ni ujinga, halafu yeye ndo kwanza anaianza safari, angesusa mtu kama Belle 9 au Mavoko sawa kwakuwa tushajua uwezo wao kwamba ni wakali hata wasipopewa tuzo, ila kawimbo kamoja ushapata bichwa na kuanza kususa? boya kweli huyu, hapo ndo kajitia gundu kabisa, sidhan kama atafanya vizuri tena
 
Huyo mtoto ni mjinga anashindwa kujua kuwa wananchi ndio wamependekeza majina na wao ndio walio mpigia kura chache ndio maana hayupo....
Na yeye aka anzishe za kwakwe kama H baba! Mimi mwenyewe si kumpendekeza na sikuweza kumpendekeza kwa ule wimbo mmoja!

Mjinga na kaniudhi kwelikweli.Hasira zote hizo kisa katoa hit moja tu? Na kapata nomination moja analalamika nini?

Hahahahahaa nilikua sijui hilo la H Baba!
 
huyo mtoto kumbe mjinga hivo, nilikuwa namtetea ila hapa simsapoti, kususasusa ni ujinga, halafu yeye ndo kwanza anaianza safari, angesusa mtu kama Belle 9 au Mavoko sawa kwakuwa tushajua uwezo wao kwamba ni wakali hata wasipopewa tuzo, ila kawimbo kamoja ushapata bichwa na kuanza kususa? boya kweli huyu, hapo ndo kajitia gundu kabisa, sidhan kama atafanya vizuri tena

Dogo kazingua sana.Sijui nani kamshauri huu uamuzi wa kijinga aliouchukua.Halafu huyo ni msomi sasa! Sijui kama wasomi wako hivi akina Juma Nature watakuwaje?
Wimbo wenyewe katoa mmoja tu na kapata category moja sio mbaya sana.Hata hivyo tukisema ukweli ni kua Baraka ana hit nyingi kuliko yeye na kapata nomination moja mbona hajalalamika?
Au nae alitaka apambane na akina Aki Kiba na Diamond nini? Wenzie wametoka mbali sana.
 
Mjinga na kaniudhi kwelikweli.Hasira zote hizo kisa katoa hit moja tu? Na kapata nomination moja analalamika nini?

Hahahahahaa nilikua sijui hilo la H Baba!

Teh Teh H Baba alipanic kabisa akaponda sana na kujitoa kabisa akaanzisha tunzo za familia yake..nilisikia kampa tunzo mtoto wake na mkewe na akajipa na yeye nilicheka sana..ngoja nifatilie zaidi!
Huyo Mo music kichwa kibovu sijui msukuma wa wapi huyu..yani anashindwa kuvumilia yeye ni nani kwenye muziki ?
 
Teh Teh H Baba alipanic kabisa akaponda sana na kujitoa kabisa akaanzisha tunzo za familia yake..nilisikia kampa tunzo mtoto wake na mkewe na akajipa na yeye nilicheka sana..ngoja nifatilie zaidi!
Huyo Mo music kichwa kibovu sijui msukuma wa wapi huyu..yani anashindwa kuvumilia yeye ni nani kwenye muziki ?

Ha ha ha ha ha! Sasa hizo tuzo zinaitwaje? Haki vile nimecheka sana.Fuatilia bwana upate japo na kapicha nizidi kuvunjika mbavu!

Hapo sasa.Huyo Kiba tu na umahiri/umashuhuri wake wote hadi leo hii ana tuzo chache tofauti na stahiki yake lakini mbona hasemi chochote?
Huyu bwana mdogo kanikera sana nimeshamtoa kwenye list ya ninaowakubali.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom