KILIMO FURSA KUBWA.
Chanzo cha binadamu ni uumbaji wa Mungu. ‘’Mungu akasema , Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi...Mwanzo 1:26. Na pia, Biblia inathibitisha kwamba ‘’Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai… Mwanzo 2:7.
Mungu pia, kabla ya kuumba binadamu aliandaa mazingira wezeshi kwa binadamu kuishi. Moja ya maandalizi aliyofanya Mungu ili kuwezesha wanadamu kuendesha maisha ya kila siku‘’Bwana Mungu akamtwa huyo mtu, akammweka katika bustani ya edeni, ailime na kuitunza’’….Mwanzo 2:15.
Binadamu tumewekwa katika mazingira yanayotuwezesha kuishi kwa mafanikio anayoyatumaii Bwana, Mungu. Kazi ya kwanza kwa binadamu kuifanya ilikuwa ni kulima na kuitunza bustani ya Edeni. Hili lilikuwa agizo la Mungu kwa wanadamu wa Kwanza na pia kwa vizazi vyote. Bwana, Mungu aliaanda mazingira wezeshi kwa kizazi kilichopita, cha leo na vizazi vingi vijavyo; ‘’Mungu akasema, Maji yaliyo chini ya Mbingu na yakusanyike mahali pamoja, ili pakavu paonekane ikawa hivyo.
Mungu akapaita pale pakavu Nchi; na makusanyiko ya maji akayaita Bahari; Mungu akaona ya kuwa ni vyema. Mungu akasema, Nchi na itoe majani, mche utoao mbegu, na mti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, ambao mbegu zake zimo ndani yake, juu ya nchi, ikawe hivyo. Nchi ikatoa majani, mche utoao mbegu, na mti wa matunda uzaao matunda kwa jinsi yake, ambao mbegu zake zimo ndani yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema’’……Mwanzo1:9-12.
Bwana, Mungu aliumba eneo la Nchi kubwa ili likidhi mahitaji ya Mwanadamu ya kulima na kuotesha mazao ya aina mbalimbali kwa ajili ya kuishi na alitunze kwa ajili kuhakikisha manufaa yanaendelea kudumu kwa ajili ya vizazi vyote vya nyakati zote katika dunia hii. Kwahiyo, tangu mwanzo Mungu aliandaa mazingira na kumwambia binadamu ajihusishe na Kilimo.
Hata kwa sasa kilimo kimekuwa sekta muhimu kwa uchumi wa mtu mojamoja na kwa Taifa. Mazao ya kilimo yanatumika kwa chakula kwa binadaamu na wanyama na malighafi kwa viwanda vingi hapa duniani. Mazao ya chakula, mafuta ya kula, ya nazi, mawese, alizeti, karanga, mzeituni, mahindi, matunda ya kila namna, mpira wa miguu…..nk, vyote hivi chanzo chake ni kilimo. Mazao ya kilimo na kilimo ni FURSA KUBWA SANA YA UCHUMI NA MAISHA YA BINADAMU kwa sababu ya uimara wake katika soko-ni mahitaji yasiyoepukika kwa maisha ya binadamu, viwanda na wanyama. Ikiwa vijana na watu wa rika zote wakijihusisha na biashara ya mazao ya kilimo au kilimo biashara hata vyote kwa pamoja itakuwa ni daraja muhimu kwa ukombozi wa kilio cha ajira na uchumi wa mtu binafsi na Taifa.
Pamoja, na sekta ya kilimo kuwa tegemeo kwa Watanzania kwa zaidi ya asilimia 80+, Nchi ya Tanzania ina Ardhi kubwa yenye rutuba na mito inayotiririka maji na inapatikana kwa gharama nafuu sana hata mtu wa kipato cha chini anaweza kununulia ardhi. Tarehe 6 Aprili, 2019, Aliko Dangote, Tajiri Na.1 Africa analikuwa na Mahojiano na Mo Ibrahim juu ya Africa na Biashara, Uongozi na mambo mengine aliuzwa na Mo Ibrahim kwamba ‘’nini wafanye vijana ili waweze kuwa milionea katika umri wa miaka 20” Aliko Dangote alisema, vijana wakitaka kupata utajiri au kuwa milionea katika umri wa miaka 20 wanatakiwa kujihusisha na KILIMO NA TEHAMA. Katika mazungumzo hayo, Aliko Dangote alisema Analima Mpunga nchini Nigeria. Aliko Dangote ameona pia fursa kwenye Kilimo, wewe je? Tafakari.
Sasa kwanini kilimo kina fursa nyingi sana ambazo kijana na mtu wa rika yeyote anaweza kunufaika nazo, lakini hapohapo vijana wengi hawataki kujihusisha nacho na huku wanalalamika na ajira na maisha magumu, na wakijihusisha nacho wanachana nacho kabla ya mafanikio wanayotaka hawajayafikia.
Zifuatavyo ni moja ya sababu zinazopelekea wengi wasifikie mafanikio au wasijihusishe na kilimo;
- Dhana ya kutaka kupata bila ya kufanya chochote.
Ukipanda vibaya utavuna matokeo mabaya, na ukipanda vizuri utavuna matokeo mazuri. Dhana hii imepelekea wengi wasijishughulishe na kilimo, kwani kilimo kinataka kuwekeza, uvumilivu, king’ang’anizi na muendelezo ili kufikia mafanikio ya kweli. Katika maisha halisi, Dhana ya kupata chochote bila kufanya chochote haipo. Kwa kitambo huonyesha kuna mafanikio lakini mwishowe ni anguko.
Biblia inasema, ‘’basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafanishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba….Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba. Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafanishwa na mtu mpumbavu,aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga…Mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguke; nalo anguko lake likawa kubwa…Mathayo 7: 24-27.
Maana yake ni kwamba maisha au jambo lolote lina Kanuni na ili kuweza kufanikiwa na kudumu lazima kufuata kanuni zake, na kuzipuuza kanuni ni kujihahakishia anguko-lenye hasara kubwa. Kwa nini anguko, kwa sababu hakuna kanuni ambazo zitasaidia kuhimili changamoto zinapojitokeza. Kumbuka changamoto zitaendelea kuwepo mpaka mwisho wa dunia, kukabiliana nazo ni kwa kufuata KANUNI TU. KANUNI zinahitajika kwa ajili kuanzisha, kuendeleza na kutunza. Mafanikio ni kufuata kanuni na kufeli au kushindwa ni kutofuata kanuni. Mafanikio endelevu na kweli na yana gharama, gharama ya muda, fedha, kushindwa na kuanza upya, kushinda vikwazo vyote au uvumilivu. Maisha ni vita, unapaswa kushindana ili kushinda. Weka mpango mkakati vyema, ushindi ni hakika
- Madai ya kusema hakuna mitaji.
Maana wapo wengi wana fedha lakini kwenye kilimo hawana mafanikio. Mafanikio katika sekta ya kilimo ufahamu unakuja namba moja, na rasilimali fedha au pembejeo vinafuata ili kufanikisha. Hatahivyo, mtaji ni kile ulichonacho ambacho unaweza kuanza nacho katika kilimo. Mfano, vijana wengi wana simu janja (smartphone) za gharama kuanzia 150,000.00 hadi 2,000,000.00 kwa ajili ya mawasiliano yasio na faida huko wanalalamika maisha magumu na hawana mitaji. Kumbe, fedha zinazotumika kununua simu na vocha zikitumika kama mtaji wa kilimo baada ya miaka 5,10,15 watakuwa mbali kimtaji na maendeleo.
Hii, ni sawa na Mungu alipomuuliza Musa, una nini mkononi?, wakati walipotaka kuvuka bahari ya Shamu kwenda Kanaan. Musa akasema fimbo, na Mungu akamwambia nyosha fimbo na njia ikapatikana, watu wakapita. Lakini kabla ya tukio hilo, watu walikuwa wanalalamika wasijue kuwa fimbo ya Musa ilikuwa mtaji kwao kutengeneza njia ya kwenda ng’ambo ya bahari ya Shamu. Ujumbe, sawa mtaji unahitajika lakini anza na ulicho nacho katika kilimo.
- Kusikiliza maneno ya kutatisha tamaa.
- Kutokuwa na mipango yakufanisha kilimo.
- Kutokuwa na taarifa sahihi za kilimo.
Ajabu kweli, dunia ya leo ina vyanzo vingi vya taarifa lakini kwa bahati mbaya wengi hawanufaiki navyo, tuna fursa ya kupata taarifa lakini muda mwingi tunapoteza kwenye vitu ambavyo havina manufaa katika maisha. Unaweza kupata taarifa za kilimo kupitia; vipindi vya TV, You Tube, Instagram, Google, Facebook, wazoefu na wakulima wenye mafanikio……nk. Hivi vyanzo ni mtaji mkubwa maana vinatoa ufahamu unaohitajika wa kuanzisha biashara ya kilimo na kilimo.
Katika kilimo tunapaswa kuwa na taarifa ya soko ya mazao unataka kulima, uhitaji wa mazao, udongo, aina ya mbolea, msimu sahihi na aina ya zao, mbegu bora kwa kila zao-inayovumilia magonjwa na mazao bora na mengi. Tafuta taarifa kabla hujaanza kilimo cha zao lolote, itakuwa na manufaa sana kwako.
- Kutokuwa na ufahamu na ujuzi sahihi wa kilimo.
Jambo jema kwa dunia ya leo, kama ilivyo kwa taarifa, ufahamu na ujuzi unapatikana kilahisi na kwa gharama wezeshi kwa mwenye nia ya kuzipata. Kupitia makala kwenye TV, You Tube, Google, wazoefu na wakulima wenye mafanikio, mafunzo ya kilimo…..nk.
- Kukosa imani na kilimo
Maana kama vile mwili pasipo roho umekufa, vivyo hivyo na imani pasipo matendo imekufa. Sasa turudi kwenye mfano wetu, ni kweli una imani ya kwamba umepata gunia 100 kwa ekari tano (imagination-cha kufikirika), ni jambo jema na hongera sana kwa hatua nzuri uliyofikia lakini kuhakikisha unapata gunia 100 kwa ekari tano (outcome-Matokeo halisi) unapaswa kufuata hatua zote (Kanuni) zote za kulima Mpunga; Andaa shamba kwa wakati, Lima kwa wakati, Panda mpunga kwa wakati na Tunza kama inavyotakiwa, Hakika utapata Mavuno uliyotarajia. Kuwa na imani kunafanya mkulima kuwa na uvumilivu au king’ang’anizi na kuwa na muendelezo wa kilimo. Hii, inachochea tena kuwa na tathmini ya kile kinachoendelea kwenye kilimo. Tathmini huonyesha mahali pa kuboresha.
Basi imani, chanzo chake ni kusikia….Warumi 10:17. Je unamsikia nani kuhusu kilimo?tahadhari, ukimsikia mtu anayekuvunja moyo kuhusu mambo ya kilimo huwezi kujihusisha nacho na ukihusisha nacho utafanya bora liende yaani upate usipate kwako ni sawa tu. Ndugu yangu Nakushauri tafuta watu watakaokushauri na kukutia moyo kuhusu kilimo. Kwa kufanya hivyo, utaongeza ari na imani kwenye kilimo.
Hapo juu nimeeleza sababu saba (7) ambazo zimekuwa kikwazo kwa wengi kuwa na mafanikio wanatarajia katika kilimo japokuwa kwenye kilimo kuna fursa ambazo zinaweza kummwezesha mtu yeyote anayejihusisha nacho kupata utajiri au mali. Japo katika sababu nilizoeleza hapo juu nimetoa kinachopaswa kufanyika. Hatahivyo, naomba nikupe hatua nne (4) ambazo zitakusaidia kufanikiwa kwa jambo lolote unalotaka kufanya pamoja na Kilimo;
- Lenga jambo ambalo unataka kufanya, kuwa na dhumuni.
Sasa, naomba nikwambie, hata wewe huwa unaliona na kusikia tatizo la uhaba wa chakula hapa duniani. Uhaba wa chakula ni tatizo lenye athari kwa maeneo mengi ya maisha ya binadamu, uhaba wa chakula kwa Taifa lolote unatishia usalama na amani, njaa na vifo, mfumuko wa bei ya bidhaa na kusababisha kupanda kwa gharama za maisha. Uhaba wa chakula husababishwa na uzalishaji mdogo wa chakula ambao pia husababishwa pengine na mvua chache ama kukosa pembejeo muhimu za kilimo. Umuhimu wa chakula kwa maisha ya binadamu unafanya kilimo kuwa fursa kubwa sana ya uchumi wa mtu mmoja mmoja, kaya na taifa. Dhumuni ni kuongeza uzalishaji ili kukabiliana na uhaba wa chakula. Kijana, baba, mama jihusishe na kilimo ili uwe sehemu ya suluhisho la uhaba wa chakula na vilevile uboreshe maisha yako kwa kujiongezea kipato cha fedha.
- Weka mpango.
- Jitenge na watu wenye maneno yanayokatisha tamaa, maneno Hasi.
- Kuwa na watu wa kujifunza kwao (Mentor).
Mwisho, nimatumaini yangu kuwa makala hii itakusaidia kuwa na mtazamo mpya wa kilimo na kujihusisha nacho na kuboresha kipato chako kubadilisha kabisa maisha yako ya kila siku. Hatahivyo, makala hii itakubadilisha kabisa mtazamo wako namna ya kufanya mambo yako. Naomba Mungu awe pamoja nawe unaposoma na kuchukua hatua.