mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,076
- 4,113
Katika ziara ya Mwenezi wa CCM, Paul Makonda Wananchi jimbo la Same wameonesha kutokuwa na imani na mbunge wao, ambapo wamedai kuwa mbunge huyo amekuwa akirudisha nyuma maendeleo ya jimbo hilo hasa kwa kuwagawa vijana na watu. Wamemnukuu Hayati Nyerere kuwa ili maendeleo yawepo lazima kuwepo na SIASA SAFI, lakini mbunge huyo amekuwa chanzo cha kukwamisha maendeleo.
Raphael Mruta amesema...
"Nyerere alishawahi kusema ili maendeleo lazima tuwe na siasa safi tupo na mbunge ambaye anagawanya vijana, anagawanya watu hata lile soko kufeli ni kwa sababu ya sumu ya wakazi wa Same hilo lipo wazi kuwa hatuna mbunge,"
"Wanaokwamisha maendeleo ya Same ni kutokuwa na siasa safi tuna mbunge ambaye haonekani jimboni wala bungeni," amesema huku akishangiliwa na wananchi.''
Wananchi hao wameendelea kudai kuwa mbunge wao huyo amekuwa haonekani bungeni jambo ambalo linawapa wasiwasi wananchi hao. ''Hapa tuna Mkuu wa wilaya na Mkurugenzi hatuna Mbunge, Jimboni hayupo na Bungeni Hayupo anawagawa wananchi"
Raphael Mruta amesema...
"Nyerere alishawahi kusema ili maendeleo lazima tuwe na siasa safi tupo na mbunge ambaye anagawanya vijana, anagawanya watu hata lile soko kufeli ni kwa sababu ya sumu ya wakazi wa Same hilo lipo wazi kuwa hatuna mbunge,"
"Wanaokwamisha maendeleo ya Same ni kutokuwa na siasa safi tuna mbunge ambaye haonekani jimboni wala bungeni," amesema huku akishangiliwa na wananchi.''
Wananchi hao wameendelea kudai kuwa mbunge wao huyo amekuwa haonekani bungeni jambo ambalo linawapa wasiwasi wananchi hao. ''Hapa tuna Mkuu wa wilaya na Mkurugenzi hatuna Mbunge, Jimboni hayupo na Bungeni Hayupo anawagawa wananchi"