Mbunge wa Jimbo la Igunga aendelea na ziara Jimboni

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,900
944
đź“Ť Igunga, Tabora

❇️ MBUNGE NGASSA KUANZA ZIARA JIMBONI

❇️ KUHUTUBIA MIKUTANO SITINI (60)

❇️ KUFANYA ZIARA KATA KUMI (10), VIJIJI THELATHINI (30)

Mbunge wa Jimbo la Igunga Mhe. Nicholaus George Ngassa, anaanza ziara ya Kikazi Jimboni kwa ajili ya kutoa mrejesho wa Bunge la Bajeti kwa Wananchi, Kutatua kero za Wananchi na kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Mheshimiwa Ngassa (MB) anaanza ziara ikiwa ni utaratibu wake wa kutoa mrejesho kwa Wananchi mara baada ya Bunge la Bajeti kukamilika.

Mheshimiwa Ngassa (MB) ataambatana wa Watalaam wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga kwa ajili ya kutoa ufumbuzi wa kero za Wananchi.

"KAZI NA MAENDELEO"

Imetolewa na:
Ofisi ya Mbunge
Jimbo la Igunga
5 Julai, 2023

 

Similar Discussions

Back
Top Bottom