Kili Music Awards 2011

Kili Music Awards 2011

tehe huo wimbo una uasili gani? zile nyimbo za saida kaloli si ndo za asili? mpoki kafanya bongo fleva kuna vikundi kibao vinafanya ngoma au mziki wa asili. ntaanzisha kikundi changu cha KAMBINDI halafu ntaimba huu wimbo SOKONI NILIPOKWENDA SOKONI NILIPOKWENDA NILIMKUTA DADA MMOJA EEH LIWAYA AMEPAKA WANJA EEH LIWAYA WANJA SIO WANJA EEH LIWAYA BALI NI MKAA EEH LIWAYAA
 
utadhani ni mashindano ya wanafunzi wa sekondari, hakuna mvuto na mpangilio ni hovyo hovyo
 
Hivi hii Kili music awards ina EVENT ORGANIZER? Ni kinyaa kitupu kwenye stage jamani. Watu hawawezi kujieleza, wanashukuru ukoo mzima, marafiki, maproduzer puh! Wengine wanagombea kupokea tuzo. Hao watoaji tuzo wenyewe wana maneno mengi, wewe umepewa kazi ya kumpa mwanamuziki tuzo unaleta story za nini? Mwishowe wanajiumauma na kuchemka kama Nsajigwa katia aibu alipokuwa anamtangaza mshindi.

Napendekeza kuwe na REHESAL kwa wanaowania tuzo wote, wagawa tuzo, na ma MC. Ikiwezekana umeze kabisa utakachosema ukifika pale stejini, na jinsi ya kuipoke tuzo yako. Loh! Halafu nani kasema huyo Milard Ayo anafaa ushereheshaji? Huyo ni presenter mzuri sana kwenye TV na radio but si MSHEREHESHAJI jamani! Anachemka kinoma. Mpoki amejitahidi, hajaongea utumbo, Mzee small na Bi Chau wamefurahisha, C Pwaa yuko presentable hata kwenye kupokea tuzo amejitahidi. Watu hawako serious, hawako presentable ni kichefuchefu.

Huyo Lina nae sijui kavaa nini, wacheza shoo wake wadada wamependeza kama nini na vigauni vyao vya silver , yeye hata sijuui kavaa nini. Duh! Bado tuko nyuma sana. Naona hata aibu jamani. Hivi huwa hawatizami Grammy, Emmy na tuzo zingine?
Najihisi kama mwanamke ambaye kajifungua bila kuwa na ujauzito - Mpoki
 
Keep me posted maana nimezima TV ili niboreshe uhusiano kati ya kichwa changu na mto. If you know what I mean.
 
Pengine walio ukumbini wanaenjoy zaidi/wanaona vitu bora zaidi! Kwa ss tunaoangalia tv itv wametuangusha...
 
Yap! Mkongwe Said Mabera ANANOGESHA KIUKWELI PALE!!!!
 
Tuwape moyo, tuwakosoe na tuseme wanatakiwa kufanya nn, sio kupoonda tu bana.....!
 
Pengine walio ukumbini wanaenjoy zaidi/wanaona vitu bora zaidi! Kwa ss tunaoangalia tv itv wametuangusha...
watu wanaweza kutofautisha kati ya itv na maandalizi mabovu
na kutuwekea nyimbo za mwaka juzi nayo ni itv:embarassed2:
 
Back
Top Bottom