Von Bismarck
JF-Expert Member
- Jul 11, 2018
- 3,074
- 6,254
Habari Watanzania?
Moja kwa moja kwenye mada!
Nimekuwa nachangia damu mara kwa mara kadiri ninapojisikia bila hata shinikizo au ushawishi wowote.
Hii tabia niliianza nikiwa nasoma kidato cha nne mpaka leo.
Ukweli ni kwamba kila ninapochangia Damu, moyo wangu unapata amani achilia mbali amani naona nimeokoa maisha ya mama zetu wakiwa leba, ndugu zetu waliopata ajali, wagonjwa wanaohitaji kuongezewa damu.
Kwangu najiona nimetoa Sadaka isiyo ya kinafiki kwa Mungu, sadaka yenye upendo, huruma na thamani sana.
NB: Mungu azidi kuwafanyia wepesi watu wanaopitia mateso na maumivu ya magonjwa au ajali.
Ndugu zangu uhai ni zawadi tunayopewa na mwenyezi Mungu, leo tupo lakini kesho yetu ni fumbo kubwa sana hatuwezi kulifumbua.
Tulio na nafasi yakufanya jambo hili( kuchangia damu) Tafadhari sana tujitoe kwa upendo wa ndugu zetu.
Jamii yetu inahitaji kusaidiana, hivyo tunaweza tusiwe na pesa ya kusaidia, au chakula lakini tukachangia damu zetu kama Sadaka.
Damu ni uhai unapochangia umejitoa uhai wako kwa ajili ya mtu mwingine. Mungu hawezi kukuacha kamwe.
Moja kwa moja kwenye mada!
Nimekuwa nachangia damu mara kwa mara kadiri ninapojisikia bila hata shinikizo au ushawishi wowote.
Hii tabia niliianza nikiwa nasoma kidato cha nne mpaka leo.
Ukweli ni kwamba kila ninapochangia Damu, moyo wangu unapata amani achilia mbali amani naona nimeokoa maisha ya mama zetu wakiwa leba, ndugu zetu waliopata ajali, wagonjwa wanaohitaji kuongezewa damu.
Kwangu najiona nimetoa Sadaka isiyo ya kinafiki kwa Mungu, sadaka yenye upendo, huruma na thamani sana.
NB: Mungu azidi kuwafanyia wepesi watu wanaopitia mateso na maumivu ya magonjwa au ajali.
Ndugu zangu uhai ni zawadi tunayopewa na mwenyezi Mungu, leo tupo lakini kesho yetu ni fumbo kubwa sana hatuwezi kulifumbua.
Tulio na nafasi yakufanya jambo hili( kuchangia damu) Tafadhari sana tujitoe kwa upendo wa ndugu zetu.
Jamii yetu inahitaji kusaidiana, hivyo tunaweza tusiwe na pesa ya kusaidia, au chakula lakini tukachangia damu zetu kama Sadaka.
Damu ni uhai unapochangia umejitoa uhai wako kwa ajili ya mtu mwingine. Mungu hawezi kukuacha kamwe.