Usipofanya haya, utabaki unalalamika kila siku na kila mwaka

Objective football

JF-Expert Member
Oct 21, 2023
1,196
2,758
Mwaka 2023 umekuwa mwaka wenye neema na baraka maishani mwangu.

Ni muda mrefu nilikua nikiamini mafanikio iwe ya kiuchumi,kiafya ,ndoa na kadhalika inatokana na juhudi binafsi na kujituma pekee.

Kumbe nilikua niko tofauti ndugu zangu, leo nakupa siri jaribu kuifanyia kazi,mwenzenu imenisaidia imenipa unafuu wa maisha hakika mpaka sasa ninaweza msaidia mama nyumbani na jamii kwa ujumla.

Siri ni hii , tafuta karatasi nyeupe andika vipaumbele vyako mkiri mwenyezi MUNGU akusaidie. unavyo anza kuomba kwa mwenyezi MUNGU mshukuru kwanza yeye kwa kukupa pumzi na vitu alivyo viumba.

Kisha endelea kwa kumuomba MUNGU asamehe dhambi , maagano na laana za ukoo wako(generational curses) ,mizigo ya wazazi wako iwe fitna,uchawi,dhuluma nk uwataje majina ya wazazi wako wote wawili pamoja na bibi na babu yako.

Unajua dunia hii wengi tumebeshwa matatizo,balaa na mikosi kutokana na dhambi za wazazi wetu ,roho za kukosa,ajali,kukataliwa zinawasumbua wengi sana.

Kisha fuata na kukiri dhambi zako zote zitaje mfano"eeh MUNGU wangu mimi dismass ignas nisamehe dhambi ya ulevi, zinaa, Ushoga,punyeto,usagaji,dhuluma, niliyomtendea fulani na hata ambazo siku kusudia iwe kwa fikra nisamehe MUNGU"

Then, chukua sadaka yako kaitoe kwa wenye uhitaji mfano yatima,walemavu, wajane . hakikisha unapo mpatia sadaka una chuchumaa kwa muhusika tamka hivi mbele yake ili uongee na MUNGU wako moja kwa moja" ewe Mama yangu, mzee wangu naitoa hii sadaka kwako sababu naomba na mimi MUNGU Anikumbuke anipatie mtoto, ajira, biashara yangu ya vinywaji isonge, amani katika ndoa yangu,masomo kwa wanangu "

Sadaka hii inaenda kufukuza kila aina ya vikwazo vya kiroho vinavyo kurudisha nyuma,sababu wachawi ama madui zetu pia wanatumia gharama kubwa katika madhabahu yao kukurudisha nyuma wewe na familia yako.

Hakika hakuna roho chafu itakayo kusumbua,umasikini utauaga kwa kipindi kifupi kwenye hiyo shughuli yako unayoifanya, ndugu zangu nayatoa hapa kwenu kama ushuhuda nafahamu MUNGU alikonitoa,hata wewe kijana unaesumbuka na haya maisha ukurasa wako utabadilika.
 
Kuna rafiki yangu mmoja aliwahi kusema kuwa hawa ombaomba unaowaona mtaani ni malaika hivyo wanapokufuata uwasaidie usisite kutoa chochote ulichojaariwa, ingawa ombaomba wengine ni matapeli tu hawataki kufanya kazi kazi kuombaomba mtaani kwa kisongizio cha kutaka nauli.
 
Kuna rafiki yangu mmoja aliwahi kusema kuwa hawa ombaomba unaowaona mtaani ni malaika hivyo wanapokufuata uwasaidie usisite kutoa chochote ulichojaariwa, ingawa ombaomba wengine ni matapeli tu hawataki kufanya kazi kazi kuombaomba mtaani kwa kisongizio cha kutaka nauli.
yawezekana ndugu yangu, wengi wao wana nguvu sana ya kubadili maisha yako
 
Back
Top Bottom