Kila January huwa napata ajali

Kila January huwa napata ajali

Inaonekana mkuu hata kufa utakuja kufa mwezi january ya mwaka wowote!, hapo cha msingi badili ratiba zako january yote uwe unajifungia ndani uanze kusafiri mwezi february.
Nyumba inaweza ungua moto, au pumzi ikabana tu
 
Sijui shida ni nini..
Mimi mke wangu alipojifungua mtoto wa kwanza, baada ya wiki 2 hivi nikapiga zinga la haja
Na huyu mtoto mwingine nae hivyo hivyo siku hiyo natoka home na hisia za ajali kabisa, nikaenda kupata ajali, ila zote nilitoka salama
hiyo ni kweli adui anakutafuta ufe, hawataki uoe/uwe na familia. Je! Kila baada ya kujifungua mke wako watu wa kwanza kuwapa taarifa ni akina nani?
 
Hii imenishangaza sana. Ni miaka minne mfukulizo. Pengine inaweza kuwa zaidi kwa kuwa sikufuatilia kabla. Natumia usafiri wa pikipiki. Sasa nikishapata ajali au kuanguka na pikipiki, basi sipati tena ajali mwaka wote. Au kuanguka.

Sasa mwaka ulivyoanza hii hali au kumbukumbu ikanijia. Na mara nyingi huwa ni kati ya tar 1 hadi 10. Sasa nikiwa njiani nakumbuka na najitahidi sana kuwa makini, ila ikipangwa imepangwa tu.

Leo imetokea. Bajaj aliyekuwa anatoka kwenye foleni bila umakini aliiingiza njia ya upande wa kulia nikajikuta namparamia. Nilidondoka vibaya nikaumia sehemu kadhaa. Ajali hiyo ilisababisha pkpk nyingine iliyokuwa inakuja mbele yangu kuharibika taa ya mbele.

Wakati naanguka nikawa nacheka tu nikijua tayari January imejibu. Pamija na kwamba niliumia, sikutaka kuhangaishana na bajaj. Nilichukua chombo changu na kuondoka nikimuacha kabananishwa na aliyeharibiwa taa. Nilijua ya January yametimia hivyo sikuwa na sababu ya kulumbana.
Hofu yangu ni kuwa hii trend itanijenge hofu ya January

View: https://youtu.be/LA8j13jWji8?si=nAJAweTFI2adD8ZC


View: https://youtu.be/EpuyQScCGa0?si=DbS456mLZa8Irn0y


View: https://youtu.be/4Xg0ByQok9I?si=fu0GJnx6mofjLRwY


View: https://youtu.be/p1FkCBuz3zI?si=uBqDUh7s3MWglo-R


View: https://youtu.be/GvrRGkEFlo8?si=O9Eni7psThyKD9Je
 
hiyo ni kweli adui anakutafuta ufe, hawataki uoe/uwe na familia. Je! Kila baada ya kujifungua mke wako watu wa kwanza kuwapa taarifa ni akina nani?
Sijui kwa kweli maana taarifa za mke wangu kujifungua huwa zinasambaa ngumu sana kuwaza wapi waliopqta taarifa na watu gani hawakupata
 
(Maombolezo 5:7)

Baba zetu walitenda dhambi na sasa hawako, na sisi tumeyachukua maovu yao.


....Mwisho wa kunukuu.....

Hiyo ni laana, ndugu zako ,babu Katika ukoo wenu walitoa sadaka Katika madhabahu za kiukoo Ili kupata ulinzi au msaada wa mizimu,

Sasa hiyo ni moja ya mashart ya kupokea msaada huo wa kimizimu. Magonjwa ya kujirudia yanayofanana, vifo vinavyofanana muda nk nk

SOLUTION.

Nenda kabomoe madhabahu ya ukoo wenu, Haribu Kila kitu Kisha umjengee Mungu mmoja, YESU KRISTO Madhabahu Katika ukoo wenu, Kisha uwe lango la ukoo wenu kuhakikisha ukoo nzima unamwabudu Mungu mmoja YESU Kristo.

Ufalme hutekwa na wenye nguvu, nenda pia kwa nguvu ewe mtu hodari..

NB: Hata nchimin petu, kiongozi kufia mamlakani baada ya awamu moja ni kitu kinachokwenda kujirudia
 
Acha kutumia Pikipiki mwezi January.. jibu unalo
SI solution hiyo,

Pkpk itamfuata hata nyumbani imgonge.

Hizo mambo huwa zimekuwa set, ni kama kutega alarm ikuamshe sasa Saba usiku,

Unadhani ukifika muda huo itaacha?

Muhimu ni atafute chanzo Kisha akiondoe ndipo kujirudia huko Kutakoma.
 
SI solution hiyo,

Pkpk itamfuata hata nyumbani imgonge.

Hizo mambo huwa zimekuwa set, ni kama kutega alarm ikuamshe sasa Saba usiku,

Unadhani ukifika muda huo itaacha?

Muhimu ni atafute chanzo Kisha akiondoe ndipo kujirudia huko Kutakoma.
January ajipe likizo asipande wala kusogelea Pikipiki.. aangalie February vipi yatajirudia asitupange.. mfano mimi hua naugua mafua makali kila mwaka mwezi wa 9 kwenda wa 10 na mwezi wa 12 mpaka hua nahisi hio hali ndivyo nilivyo tu ila mwaka jana mwezi wa 12 na mwezi wa 9 kwenda wa 10 nimeshangaa sijaugua mafua kabisa nimekuja kuugua mafua hii January ndio hali ya mafua kunibana imeanza.. hapo pia unasemaje?
 
January ajipe likizo asipande wala kusogelea Pikipiki.. aangalie February vipi yatajirudia asitupange.. mfano mimi hua naugua mafua makali kila mwaka mwezi wa 9 kwenda wa 10 na mwezi wa 12 mpaka hua nahisi hio hali ndivyo nilivyo tu ila mwaka jana mwezi wa 12 na mwezi wa 9 kwenda wa 10 nimeshangaa sijaugua mafua kabisa nimekuja kuugua mafua hii January ndio hali ya mafua kunibana imeanza.. hapo pia unasemaje?
Mimi pia nilikuwa naugua mafua Kila msimu wa mvua unapoisha kwenda kiangazi na pale kiangazi kinapoisha kwenda masika,

Nilidhani ni vumbi la kawaida,

Nilipokuja kustuka ni pando la mwovu, nikaikataa Hali hiyo ya kuugua mafua kwa kujirudia majira.

Saizi Nina miaka mitatu nadhani hakuna kitu hiyo.

Usiku watu walalapo, waovu hupanda magonjwa.

Stuka.
 
Mimi pia nilikuwa naugua mafua Kila msimu wa mvua unapoisha kwenda kiangazi na pale kiangazi kinapoisha kwenda masika,

Nilidhani ni vumbi la kawaida,

Nilipokuja kustuka ni pando la mwovu, nikaikataa Hali hiyo ya kuugua mafua kwa kujirudia majira.

Saizi Nina miaka mitatu nadhani hakuna kitu hiyo.

Usiku watu walalapo, waovu hupanda magonjwa.

Stuka.
Sijakuelewa
 
Back
Top Bottom