Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 11,866
- 4,252
Hii imenishangaza sana. Ni miaka minne mfukulizo. Pengine inaweza kuwa zaidi kwa kuwa sikufuatilia kabla. Natumia usafiri wa pikipiki. Sasa nikishapata ajali au kuanguka na pikipiki, basi sipati tena ajali mwaka wote. Au kuanguka.
Sasa mwaka ulivyoanza hii hali au kumbukumbu ikanijia. Na mara nyingi huwa ni kati ya tar 1 hadi 10. Sasa nikiwa njiani nakumbuka na najitahidi sana kuwa makini, ila ikipangwa imepangwa tu.
Leo imetokea. Bajaj aliyekuwa anatoka kwenye foleni bila umakini aliiingiza njia ya upande wa kulia nikajikuta namparamia. Nilidondoka vibaya nikaumia sehemu kadhaa. Ajali hiyo ilisababisha pkpk nyingine iliyokuwa inakuja mbele yangu kuharibika taa ya mbele.
Wakati naanguka nikawa nacheka tu nikijua tayari January imejibu. Pamija na kwamba niliumia, sikutaka kuhangaishana na bajaj. Nilichukua chombo changu na kuondoka nikimuacha kabananishwa na aliyeharibiwa taa. Nilijua ya January yametimia hivyo sikuwa na sababu ya kulumbana.
Hofu yangu ni kuwa hii trend itanijenge hofu ya January
Sasa mwaka ulivyoanza hii hali au kumbukumbu ikanijia. Na mara nyingi huwa ni kati ya tar 1 hadi 10. Sasa nikiwa njiani nakumbuka na najitahidi sana kuwa makini, ila ikipangwa imepangwa tu.
Leo imetokea. Bajaj aliyekuwa anatoka kwenye foleni bila umakini aliiingiza njia ya upande wa kulia nikajikuta namparamia. Nilidondoka vibaya nikaumia sehemu kadhaa. Ajali hiyo ilisababisha pkpk nyingine iliyokuwa inakuja mbele yangu kuharibika taa ya mbele.
Wakati naanguka nikawa nacheka tu nikijua tayari January imejibu. Pamija na kwamba niliumia, sikutaka kuhangaishana na bajaj. Nilichukua chombo changu na kuondoka nikimuacha kabananishwa na aliyeharibiwa taa. Nilijua ya January yametimia hivyo sikuwa na sababu ya kulumbana.
Hofu yangu ni kuwa hii trend itanijenge hofu ya January