Walnut Creek
JF-Expert Member
- Mar 17, 2009
- 5,717
- 6,053
Sikiliza hiyo nchi haijawahi kuwa na demokrasia la sivyo Seif angekuwa Rais wa Zanzibar. Mtu anashinda zaidi ya asimilia 70 hapewi ushindi halafu unaniambia viti vichache vya ubunge. Halafu ukiwa Rais wa Tanzania hamna mtu anaweza kukuzia kufanya jambo lako.Demokrasia ilikua na kufurahisha. Ktk kipindi cha Kikwete uchaguzi ulikuwa na maana walau kwa wananchi. Wakati wa Kikwete tulishudia Chadema na CCM vikiingia ktk uchaguzi wa mbunge wa marudio kule Arumeru mashariki Rais Mstaafu B. Mkapa na vigogo kibao wa CCM wakiwemo mawaziri walipiga kambi kumnadi mgombea wa CCM. Lakini matokeo yaliyo tangazwa ni kuwa kijana Joshua Nasari wa CHADEMA aliibuka mshindi.
Kikwete aliona mapungufu mengi aliyo kumbana nayo yalitoka na mfumo mbovu wa Kikatiba. Akaanzisha mchakato wa Kupata katiba mpya na Jaji warioba akatuletea katiba pendekezwa ya wanachi.
Wenzake wakaogopa Katiba mpya na kuivuruga hapo huwezi mlaumu Kikwete alisha onesha njia.
Kwa hiyo wewe hukuona hayo ya ndani ya Uzi siyo?.