Kikwete na semina elekezi kwa Mawaziri - Dodoma 2011

Ni kweli kabisa hizi semina hazina tija. Jana saa 3 usiku TBC walirusha ufunguzi wa semina hiyo na nikashangaa kuona kwamba mambo ambayo viongozi hao wanafundwa niyale ambayo kila mtu anayeteuliwa kuwa Waziri au Katibu Mkuu anatakiwa awe anayafahamu. Vinginevyo hakuna haja ya mtu asiyefahamu mabo ya kawaida kuteuliwa kushika wadhifa huo. Kwa mfano kweli Waziri au Katibu Mkuu anahitaji kufanyiwa semina ili aelewe hali ya uchumi wa dunia au athari ya madawa ya kulevya? Hii ni kupoteza fedha zetu bure.
 
hii ni semina au mafunzo ya uongozi, sasa Rais kama anachagua watu kwa upendeleo wakati wengi ni mbumbu wa uongozi ati kwa kuwa alimwezesha kwa kuficha siri za uchaguzi au aliwazibiti wapinzani vilivyo na akampa ka cheo kama shukruni , si ndio hawa wanaofundishwa kuongoza sasa eti wanafundwa, mtu mzima alelekezwa utoa mamuzi ya busara yenye tija kufuatana na kazi aliyoiomba hapa ni kuaribu hela za walipa kodi tu. Mfano utambadilisha Hawa Ghasi aliyeshitaki kwa Rais kuwa "kuna watu wanakula njama na kubandika watumishi hewa alafu wanakula mishahara yao kifisadi" Rais akamuuliza, "Wewe Umefanyaje?, akamwambia "Nimepeleka Takukuru, (Rais) kama wewe umepeleka Takukuru haya mafile si yatachukua miaka nane? sasa mtu kama huyu semina elekezi itamsaidia vipi wakati ana maamuzi
 
Mimi sielewi kitu kimoja, anawambia mawaziri wasikae ofisini lakini kasahau ufinyu wa bajeti ya serikali, hii inaweza kupelekea fedha zote za wizara kubaki wizarani na wengine kula nyasi. Gharama za kusafiri kwa hiyo cabinet ni kubwa mno, labda swali la kujiuliza gharama hizo zinakuwa na tija inayokusudiwa?

Anachotaka umma ufahamu ni kwamba tatizo lipo kwa mawaziri wake na siyo yeye. Hiyo ndiyo mbinu ya huyu jamaa msanii. Anajua vizuri kwamba serikali yake hivi sasa haina hela lakini anataka mawaziri watembelee wananchi. Ndiye rais wetu huyo!!
 
...............Katika mji wa Dodoma kwasasa kuna tukio moja la msingi na la kutafakari kwa makini,limepewa jina kama semina elekezi wa viongozi wetu.Kabla ya kuidadavua hoja hii naomba nitoe maoni ya wanazuoni wa mambo ya utawala,ambao wanasema kwamba;utendaji wa kiongozi ni zao la elimu na vichocheo au motivation kwa lugha ya kigeni.Nakubalia na mawazo haya moja kwa moja.Tatizo langu lipo kwa hizi semina zetu hapa TZ,Je tathmini imefanyika kugundua zinatoa matokeo yaliyotegemewa? Tazameni semina elekezi kule Ngudoto 2009 ilitumia mamilioni ya pesa lakini mwishowe zikazalisha uwizi zaidi na ubadhirifu zaidi...Je baada ya semina hizi rushwa zitapungua? ubadhirifu utakwisha? Au ni semina za kugawana night na marupurupu mengine.........Tusidanganyane,bila utashi wa kweli wa kisiasa hata tuendeshe semina kila siku gamba halitatoka............
 
Wanapoteza pesa zetu na muda bure. Ni bora wangeenda Loliondo wakapata kikombe, labda watapona huo ugonjwa unaowasumbua. Mawaziri na watendaji wa JMT wanaugua ugonjwa aina ya ukosefu wa akili ya kufikiri, kuamua, na kutenda (UAKUKUKU).
 
Tafadhali naomba hotuba ya rais ya ufunguzi elekezi huko dodoma. Aliye nayo naomba anipe. Nitashukuru sana.
 
Kamaliza, alikuwa TBC
JK kawaambia watendaji wafanye kazi kwa biddi ili CCM ishinde tena 2015
 
Kamaliza, alikuwa TBC
JK kawaambia watendaji wafanye kazi kwa biddi ili CCM ishinde tena 2015
Mr. Presdent, we are tired with CCM, you said it in Dodoma on birthday of CCM, and that it is. After your presdence end on 2015 we want to see and taste others faces. Thank you.
 
ingekuwa vema kuwa na viashiria (indicators) vya kupima matokeo katika uborshaji utendaji kazi serikalini baada ya semina---- isije ikawa kama nyoka wa mdimu
 
juu ya nini mkuu..

Nadhani ni akina Mlengo wa kati! Lazima uwe na moyo wa kiwendawazimu kufikiria kuwa ccm watashinda kirahisi tu na cdm watapata wabunge 15 tu kwenye uchaguzi ujao! Kwa akili ya kawaida that is impossible.
 
Back
Top Bottom