well articulatedna ukweli wa lowassa kutofaa kuwa mkuu wa nchi haubadili ukweli wa ccm kutofaa kuendelea kuwa chama tawala baada ya kushindwa kabisa kutawala kwa zaidi ya nusu karne.
Ukisema lowassa hafai kuwa mkuu wa nchi na ukasema ccm nayo haifai kuendelea kutawala, basi hapo tutakuwa kwenye ukurasa mmoja.
Lakini usije na habari za eti lowassa hafai halafu ccm wanafaa kuendelea kutawala kwa miaka mingine 5!
Nitakuona mwendawazimu!!
Acha basi kumung'unya maneno.
Jibu hili swali, sawa?
Kwa hiyo kesho wewe unaipigia kura CCM na Magufuli, siyo?
Wote hawafai ....lakini nimeamua kumchagua Magufuli bila kujali matokeo yake kuliko kuwapa nchi wanamtandao waliogombana na Mkuu wa kaya na kuamua kwenda upinzani kutimiza haja zao .....
Akiongea leo Mwanza kwenye kufunga kampeni za ccm Mh.Jk amesema ni kweli alishiriki kwenye makubaliano ya kutafuta kampuni ya kufua umeme baada ya Mabwawa kukauka nchi, lakini hakushiriki kutafuta kampuni gani ilete umeme, hivyo hahusiki kwa namna yoyote kwa ujio wa Richmond.
Hivyo waziri Mkuu ndio mhusika mkuu wa Richmond!
Wewe hujielewi kabisa!
Huwezi kusema Lowassa na Magufuli wote hawafai halafu ukaamua kumchagua Magufuli.
Kwa nini umpe kura yako mtu ambaye tayari ushakiri kuwa hafai?
Kama kura yako ni 'protest vote' kwa nini usimpe mama Mghwira wa ACT?
Wewe siyo sehemu ya ufumbuzi wa tatizo bali ni sehemu ya mwendelezo wa tatizo.
Na usije hapa kulialia siku huyo utakayempa kura yako atakapoendeleza yale yale ya miaka 54 iliyopita.
Mkuu kulalamika kupo hata Lowasa akiwa mkuu wa nchi (God forbid)
Tulijua atasema hivyo,but amechelewa tulishafanya maamuzi.
Tarehe 25/10/2015 kuna nini?