Kikwete: Lowassa ndiye mhusika wa Richmond

Kikwete: Lowassa ndiye mhusika wa Richmond

Status
Not open for further replies.
Katika pitapita yangu nimekutana na video ya kampeni katika uchaguzi wa mwaka juzi (2015) ambapo aliyekuwa akimaliza muda wake ndugu JK alisema pasipo kumung'unya maneno kwamba mwenye richmond si mwengine ila ni Bwana Lowassa.

Yawezekana kwa wakati ule tulikuwa na mihemuko ya vyama na joto la uchaguzi na kupelekea kwa namna moja ama nyingine watu kutopata wasaa wa kusikia hilo (Binafsi sikupata kusikia hotuba hii hapo kabla). Lakini leo tunaweza jadiliana kwa kina juu ya hili jambo.

Inakuwaje kitengo cha kampeni cha wakati huo cha CHADEMA hawakupata kujibu tuhuma hizo jukwaani kama ambavyo bwana JK alizitoa Jukwaani.? Kwa maana wengi walikuwa wanasuburi ama walidhani Lowassa angejibu ama kutoa maelezo iwapo tuu angeanza kushambuliwa.

CHADEMA wasitake kutuambia kwamba hawakusikia hizo tuhuma, kwani katika ushindani wa wakati ule naamini kabisa ni lazima kulikuwa na mtu/watu mahususi kwa ajili ya kufuatilia yanayofanywa na wapinzani wao (CCM) na isitoshe tuhuma zilitolewa public katika utambulisho wa kumnadi JPM,

Kwa hiyo naamini kabisa viongozi wa juu wa CHADEMA pamoja na Lowassa mwenyewe walisikia kupitia vyombo vya habari. Na pia wasije na hoja kwamba Bw. Lowassa alikuwa akilinda kiapo cha kutotoa siri alichokula wakati akiwa katika baraza la mawaziri, kwani kama ni kulinda kiapo hicho JK angekuwa wa kwanza na wala asingeanza kuyatamka hayo mambo ya Richmond katika jukwaa la kisiasa.

Tena JK hakuishia kutamka tuu, bali alitamka kwa lengo la kuvunja nguvu ya upinzani uliokuwa mbele yao na kujivunia wafuasi toka upande wa pili pamoja na kujipa nguvu upande wao.

Pia CHADEMA msije na majibu ya kuwa kama EL ni mtuhumiwa wa Richmond, basi apelekwe mahakamani ama ashitakiwe. Hii itakuwa si utetezi yakinifu, kwani yawezekana upande wa pili hawaoni sababu ya kumpeleka mahakamani either wanaona kwa kumpeleka mahakamani wataibua madudu yao yaliyojificha ama wameona kwa kumpeleka mahakamani watampa nguvu ya kisisa ama vyovyote vile.

Najua wengi mtakuja kwa kusema nimetumwa na CCM, Kwanza tuu niweke wazi kuwa mimi si mwanachama wa CCM wala CHADEMA (kwa maana sina kadi ya chama chochote kati ya hivyo). Ila tuu nimepata kuwa mkereketwa wa upinzani. So juu ya hili sijatumwa na mtu yeyote yule.

Nimeambatanisha video hiyo, Tuhuma hizo zimeanza kutolewa kuanzia dakika ya 5:10 na kuendelea.



yote hayo ni sawa, swali ni je mbona hakamatwi? Mbona ajafunguliwa kesi? Mbona yupo tu pale masaki?
 
Sipo hapa kusema kikwete anahusika ama laa. Nipo hapa kwa kuhoji ilikuwaje EL alishindwa kutumia his chance hata pale ambapo alishutumiwa direct na aliyekuwa boss wake. Kama angejibu jambo lenyewe aloshutumiwa nalo lilikuwa na uwezo wa kumbeba katika alichokuwa akikitaka zaidi ya alivyokaa kimya. Ndipo hapa inaibuka, was this man (EL) so serious na alichokuwa anakitaka.?
He was serious indeed ndio maana akahamia upinzani bila kuogopa kuwa ccm watamuandama na hata kumtupa jela.

Hilo la lowasa kutohusika kwa watanzania wengi walishaliona hasa baada ya kuona madili ni mengi serikalini wakajua kirusi kipo sehem sasa kma kila unapoenda watu wanakupokea kwa shangwe na kuonyesha kukuamini hadi kukupa kura zaidi ya million 6(NEC) una haja ya kujisafisha kweli?? Yye alishasema muende mahakamani simply ili yenyewe ndio ikamsafishe au ikamtuhumu huko......

So the answer is YES, he was serious ndio maana alikuwa tayari apandishwe kizimbani amwage mboga Kikwete akaogopa akaishia yeye na mwakyembe kuongea majukwaani tu shame on them.

By the way lowassa hanaga tabia za kujibu watu ametukanwa sana na kusemwa sana ila hajawahi kumjibu mtu yye as long as nafsi haimsuti wala kumhukumi na anajua yupo sahihi na anachokifanya basi kwake ITS ALL WELL AND GOOD ndio maana akajibu tu mwenye ushahidi apeleke mahakamani full stop mwisho wa siku watanzania wakapima wakaona mkweli mi nani ndio maana lowassa akapata kura mamilion ya watanzania na kma sio NEC leo hii tungeongea mengine
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom