Kikwete: Kutokana na utoaji hafifu wa Elimu nchini, kuna hatari ya nusu ya ajira zilizopo kutoweka ifikapo mwaka 2050

JK amesahau matumizi ya teknolojia hayabadilishi mitaala, usome kwa kutumia tablet au mwenzio aende kayumba at the end of the day wote watafanya mtihani mmoja.

Labda yule wa tablet atamzidi mwenzie topic alizo-cover in case ikitokea issue kama ya Corona, ila pasipokuwepo na Corona tofauti yao itakuwa ndogo sana.

Kitakachomyima mtoto wa masikini ajira hata akiwa na ufaulu mzuri bado ni kujuana (nafasi kutolewa kwa upendeleo) lakini sio kwasababu ya teknolojia, na ajira bado zitakuwepo pale pale haziwezi kuondoka.
Watanzanina bado tunachujuliwa kama watoto wadogo. Pia watu wana shindwa kutofautisha ajira na utumwa
 
Ukweli mchungu by 2050 kila kitu kitabaki kwenye technology

Hivyo wanaitajika watu ambao wapo tayari kujiajiri, Machine na operators wa machine

Maroobot vile vile yatakuwa yakifanya kazi sehemu kama shelli na super market

So kazi zitakuwa chache au kutokuwepo kabisa

Kikwete ana hoja tuchukue hatua.
Easily manupulated
 
Teknolojia pia inatengeneza kazi nyingi, cha muhimu ni kuhakikisha watoto watu wanapewa kipaumbele kwa masomo ya sayansi na teknolojia ili hizo ajira nyingi zibaki nchini, hakuna teknolojia inayo ondoa ajira bila kutengeneza ajira nyingine.
Lakini inategemea hizo kazi nyingi zinamnufaisha nani zaidi. Hata robot anafanya kazi kiwandani lakini anaefaidika ni nani
 
Anamaanisha kwamba ifikapo 2050 baadhi ya ajira zitakuwa zinafanywa na mashine na marobot. Kwa mfano kiwanda kinachoajiri watu 200 kwa sasa kitakuwa kinaajiri watu 25 tuu yaani 175 wanaobaki watakuwa hawana kazi.
Kama maroboti yanafanya kazi ya watu 200 si inatakiwa watu mia mbili wanufaike kwa kupunguza kazi ila mshahara ulele ule. Nini maana ya robot sasa. Si robot anarahisisha kazi
 
Mkuu mwanasiasa yeyote huwa ana akili ya utambuzi vizuri sana, yaani ana uelewa mkubwa kuhusu kipi kizuri na kipi kibaya, siyo kwamba hawa viongozi wa sasa hawaelewi hili alilolisema JK, wanaelewa sana ila tatizo ni wataendeleaje kula kama wakitoa siri kama hizi ilihali hata wao hiyo elimu iliwaumiza. So wao wanakuja kukuambia ujiajiri huku akitumia uwezo wake wa kujenga HOJA NADHARIA kuchambua na kukuambia yasiyowezekan katika uhalisia wa maisha.

Hawa viongozi wetu siyo kwamba madudu yote yanaoendelea kila sehemu hawayajui, la hasha! Wanayatambua vema sana, ila wanajifikiria wao kwanza na familia zao, maslahi ya taifa ni baadae na hayo maslahi ni yale yasiyoathiri maisha yao kiujumla.

Leo serikali ikae ianze kutengeneza syllabus mpya yenye kukidhi vigezo vyote, hao wataalamu wanao?? Tanesco leo luku mfumo unasumbua nchi nzima, mifumo yetu ya mitandao na teknolojia tunachukua nje kisha tunatumia kujifunzia halafu ndiyo tulete mfumo mpya.

Ukionekana unaleta mapinduzi hata yenye faida kwa maslahi ya nchi utawaiwa faster na kuulizwa swali dogo tu "tupe kibali cha wewe kufanya hili", mimi juzi ndiyo nimeanza hata mafanikio bado ila lengo ni kuifaidisha nchi yangu leo unakuja niuliza kibali tena ukiwa na sura ngumu na baadhi kujia na polisi na wanasheria juu wa kuanza kuchambua ibara.

Kiufupi hata hao tunaotaka wabadili mfumo wao wenyewe hawajui wataubadili vipi maana wataalamu kwanza hawapo na wanaoaminika kuwa wataalamu wanaishi kwa copy and paste, no creativity at all.

Kuna kozi unasoma Tanzania, practical unaeenda jifunzia nje tena baada ya kuitwa graduate.

Shida ni kwamba tunaishi kimazoea na tunafanya mambo yaleyale. Yaani mechanical engineer kashakaririwa kuwa kazi zake ni zilezile naye anaishi humohumo, yaani hakuna kujiongeza.

Wajanja wengi hata makazini ni wale waliojiongeza na kujifunza vingi nje ya masomo yao na hao huwa wengi wao wanatafuta sehemu zenye kujua na kuthamini thamani zao. Ukimnyima kazi hapa anatoka anaenda nje huko unasikia baada ya miaka kadhaa tuna mtanzania anafanya kitu fulani huko nje na anafanya vizuri sana.

Hii nchi ukiwa tajiri, ukiwa na uwezo mzuri wa kufikiri, ukiwa na msimamo kusimamia haki na ukijitambua sana unageuka kuwa ADUI. Maana wengi hawapendwi wanaharabu kazi za wanasiasa ambao hawajui chochote zaidi ya kukesha kukariri vifungu vya sheria na kufuata taratibu ambazo zipo outdated so unapokuja na kitu kipya unawachanganya na kuona una nia ya kuwaharibia.
Ukionekana unaleta mapinduzi hata yenye faida kwa maslahi ya nchi utawaiwa faster na kuulizwa swali dogo tu "tupe kibali cha wewe kufanya hili", mimi juzi ndiyo nimeanza hata mafanikio bado ila lengo ni kuifaidisha nchi yangu leo unakuja niuliza kibali tena ukiwa na sura ngumu na baadhi kujia na polisi na wanasheria juu wa kuanza kuchambua ibara.

KIBALI
SURA NGUMU
POLISI
KUCHAMBUA IBARA

HAKIKA UMEMALIZA KILA KITU KUHUSU JINSI MIFUMO YETU INAVYOFANYA KAZI
 
Lakini inategemea hizo kazi nyingi zinamnufaisha nani zaidi. Hata robot anafanya kazi kiwandani lakini anaefaidika ni nani
Robot mmoja anaweza ondoa kazi za watu 5 na kuongeza ufanisi ila huyo robot mmoja anatengezwa made watu 50, je hao watu 50 watakuwa Tz au hizo bidhaa zote zitakuwa imported, tusishindane na teknolojia ila tuwe sehemu ya teknolojia.
 
Kuzungumzia teknolojia leo wakati upatikanaji wa umeme tu bado ni shida ni mapema mno, mabadiliko ya teknolojia yatakuja pale ambapo tutajitosheleza kwa vitu vingine kama umeme, na wataalamu wa kutosha kufundisha.

Teknolojia itakapokuwa ndio itakuja kuathiri ajira za watu kama viwandani na kwingineko, lakini hapa kwetu bado wakati huo haujafika na sidhani kama tutafika 2050.
Technology pia inaweza Punguza matumizi ya umeme, wakati tunakua taa za bulb zile zilikuwa zinakula watts 100, Tena hata mwanga vizuri hazina, Sasa hivi unaweza kuwa na Taa mbili sebuleni, tv kubwa, na computer juu zisile huo umeme wa watts 100.

Na technology inakuwa Kwa kasi sana ukitegemea kuja kufundishwa utasubiri sana, watu wajengewe tabia ya kujiongeza wenyewe, elimu isio ya kukariri watu wajifunze kwa kuelewa.
 
Technology pia inaweza Punguza matumizi ya umeme, wakati tunakua taa za bulb zile zilikuwa zinakula watts 100, Tena hata mwanga vizuri hazina, Sasa hivi unaweza kuwa na Taa mbili sebuleni, tv kubwa, na computer juu zisile huo umeme wa watts 100.

Na technology inakuwa Kwa kasi sana ukitegemea kuja kufundishwa utasubiri sana, watu wajengewe tabia ya kujiongeza wenyewe, elimu isio ya kukariri watu wajifunze kwa kuelewa.
Kweli kabisaaaaa
 
Rais mstaafu wa awamu ya nne Dk Jakaya Mrisho Kikwete ameonya tusipobadilika namna tunavyofundisha watoto wetu basi ajira zote zitatoweka ifikapo mwaka 2050.

My take.
Hii elimu yetu ya kuwafanya chadema washangilie kila baya linaloipata nchi yetu ikiwemo kukamatwa ndege, miradi kukwama , tutashitakiwa MIGA etc bora ifutwe kabisa tuanzishe elimu mpya itakayowafanya chadema wajitambue.

====

Dar es Salaam. Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete amesema kutokana na utoaji hafifu wa elimu nchini kuna hatari ya nusu ya ajira zilizopo kutoweka ifikapo mwaka 2050.

Ameyasema hayo leo Jumanne Mei 18, 2021 wakati akizindua kongamano la elimu linalojadili ufadhili wa elimu lililoandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (Tenmet) jijini Dar es Salaam.

Akieleza utafiti uliofanywa na tume ya kimataifa ya elimu ambayo yeye ni mjumbe, amesema elimu inayotolewa barani Afrika ilitolewa miaka 50 hadi 70 iliyopita kwa nchi zilizoendelea.

"Sisi bado tunatumia chaki, wakati wenzetu wanatumia tablets. Tuliona kuwa kuna watu zaidi ya milioni 263 waliotakiwa kuwa shule lakini hawapo, kati yao milioni 100 wapo Afrika. Kwa waliopo shule wengi hawamalizi shule. Wengi wanaishia njiani. Asilimia 67 wamemaliza shule, asilimia 33 ni idadi kubwa," amesema Kikwete.

Amesema kutokana na utoaji hafifu wa elimu na maendeleo ya teknolojia kuna janga la ukosefu wa ajira linakuja.

"Ifikapo 2050 asilimia 50 ya kazi zitafutika, kwa sababu ya matumizi ya mashine. Kutakuwa na magari yasiyotumia dereva. Unataka usafiri, unaita Uba, unatumia simu yako inakuja inakupeleka sehemu husika labda Ubungo Plaza au Millennium Tower," amesema.

Amesema mbali na ukosefu wa ajira, idadi ya watu barani Afrika itafikia watu bilioni mbili, “kama watu hao hawana ujuzi unafanya nini? Sijui itakuwaje. Kutakuwa na athari kubwa za kiuchumi na kijamii."

Akisisitiza matumizi ya teknolojia, Kikwete ameshauri kuwepo na uwekezaji katika elimu ili vijana wa Afrika wasiwe watazamaji, wawe washiriki wa uchumi.

"Kunatakiwa kuwepo na matumizi ya sayansi na teknolojia katika ufundishaji. Kila shule inatakiwa kuunganishwa na intaneti," amesema.

Huku akitoa mfano wa janga la corona, Kikwete amesema limethibitisha jinsi ukosefu wa teknolojia unavyoathiri ufundishaji.

"Tumeona wakati wa corona, moja hatua zilizochukuliwa ni kufunga shule. Wanafunzi wetu hawakusoma, wanacheza rede, lakini nchi zilizoendelea shule zilifungwa na watoto wakaendelea kusoma.”

"Nilipokuwa Rais tulianzisha matumizi ya intaneti katika ufundishaji, tuliwekeza sana kwenye mkongo wa Taifa. Lengo langu lilikuwa ni kuhakikisha kila shule, hospitali ziunganishwe na intaneti. Mwalimu mmoja wa hisabati afundishe nchi nzima,” amesema.

Kuhusu Elimu jumuishi ameitaka Serikali na wadau kuhakikisha hakuna mtoto anayebaki nyuma kwa kukosa elimu.

"Wengine wanadhani msichana ni wa kubaki jikoni. Wengine wameachwa nyuma kutokana sababu za kisiasa.

Tunatakiwa kuhusisha mashirika yasiyo ya kiserikali kuchangia elimu," amesema.

Awali akimkaribisha Kikwete mwenyekiti wa Tenmet, Dk John Kalage ambaye pia ni mkurugenzi wa taasisi ya HaliElimu amesema kongamano hilo litajadili kwa kina njia za ufadhili wa elimu nchini.

Chanzo: Mwananchi
Kipindi cha utawala wake hakuliona Hili????????????????
 
Sifa kuu ya kiongozi ni kuonyesha njia kwa waliomtumainia......tunatakiwa kujua serikali imejiandaaje kukabiliana na mabadiliko hayo ya kiteknolojia kisera na kiutendaji.....au 2050 kutakuwa hakuna vijana wa kiTanzania watakaotaka ajira......??
Fact. Viongozi wengi wa Tanzania wana tabia ya kujishangaa wenyewe badala ya kuonesha mwarobaini wa tatizo.
 
Udumavu wa ubongo ni janga zaidi ya teknojia.
Watoto wengi kutokana na udumavu hawawezi kumudu maisha ya kawaida kwa sasa (kadiri ya umri wake), je atafundishwaje ili apambane hiyo 2050 kwenye soko la ajira?
Ajira zitakuwepo kutokana na utashi wa kisiasa. Kwa mfano kutoa motisha kwa wawekezaji wanaotumia nguvu kazi badala ya robot.
Tunahitaji teknolojia na ni muhimu katika elimu, ila tusikurupukie kichwa kichwa.
Tukumbuke hata umeme na maji tu bado vinatutoa jasho kwelikweli!
 
JK amesahau matumizi ya teknolojia hayabadilishi mitaala, usome kwa kutumia tablet au mwenzio aende kayumba at the end of the day wote watafanya mtihani mmoja.

Labda yule wa tablet atamzidi mwenzie topic alizo-cover in case ikitokea issue kama ya Corona, ila pasipokuwepo na Corona tofauti yao itakuwa ndogo sana.

Kitakachomyima mtoto wa masikini ajira hata akiwa na ufaulu mzuri bado ni kujuana (nafasi kutolewa kwa upendeleo) lakini sio kwasababu ya teknolojia, na ajira bado zitakuwepo pale pale haziwezi kuondoka.
Hujamuelewa mzee😂😂😂
Mzee anamaanisha ukuaji wa Elimu yetu Ni lazima uendane na ukuaji wa Teknolojia. Hivyo vyote vinategemea bajeti imara.

Kama kasi ya ukuaji wa elimu yetu iko nyuma Sana dhidi ya kasi ya ukuaji wa teknolojia Basi wahitimu wa wa kiafrika watapokonywa ajira zao.

Itakapofikia hatua watu walioendelea kutengeneza maroboti madereva, Tiketi kukatwa kwa kadi, huduma kwa wateja Ni roboti, na kila kitu. Sisi Waafrika tutakuwa watazamaji na wahitimu watashindwa kuajirika maana Teknolojia imewatupa mkono kwa sababu hatutaweza kuendesha roboti Wala kuzitengeneza.
 
Rais mstaafu wa awamu ya nne Dk Jakaya Mrisho Kikwete ameonya tusipobadilika namna tunavyofundisha watoto wetu basi ajira zote zitatoweka ifikapo mwaka 2050.

My take.
Hii elimu yetu ya kuwafanya chadema washangilie kila baya linaloipata nchi yetu ikiwemo kukamatwa ndege, miradi kukwama , tutashitakiwa MIGA etc bora ifutwe kabisa tuanzishe elimu mpya itakayowafanya chadema wajitambue.

====

Dar es Salaam. Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete amesema kutokana na utoaji hafifu wa elimu nchini kuna hatari ya nusu ya ajira zilizopo kutoweka ifikapo mwaka 2050.

Ameyasema hayo leo Jumanne Mei 18, 2021 wakati akizindua kongamano la elimu linalojadili ufadhili wa elimu lililoandaliwa na Mtandao wa Elimu Tanzania (Tenmet) jijini Dar es Salaam.

Akieleza utafiti uliofanywa na tume ya kimataifa ya elimu ambayo yeye ni mjumbe, amesema elimu inayotolewa barani Afrika ilitolewa miaka 50 hadi 70 iliyopita kwa nchi zilizoendelea.

"Sisi bado tunatumia chaki, wakati wenzetu wanatumia tablets. Tuliona kuwa kuna watu zaidi ya milioni 263 waliotakiwa kuwa shule lakini hawapo, kati yao milioni 100 wapo Afrika. Kwa waliopo shule wengi hawamalizi shule. Wengi wanaishia njiani. Asilimia 67 wamemaliza shule, asilimia 33 ni idadi kubwa," amesema Kikwete.

Amesema kutokana na utoaji hafifu wa elimu na maendeleo ya teknolojia kuna janga la ukosefu wa ajira linakuja.

"Ifikapo 2050 asilimia 50 ya kazi zitafutika, kwa sababu ya matumizi ya mashine. Kutakuwa na magari yasiyotumia dereva. Unataka usafiri, unaita Uba, unatumia simu yako inakuja inakupeleka sehemu husika labda Ubungo Plaza au Millennium Tower," amesema.

Amesema mbali na ukosefu wa ajira, idadi ya watu barani Afrika itafikia watu bilioni mbili, “kama watu hao hawana ujuzi unafanya nini? Sijui itakuwaje. Kutakuwa na athari kubwa za kiuchumi na kijamii."

Akisisitiza matumizi ya teknolojia, Kikwete ameshauri kuwepo na uwekezaji katika elimu ili vijana wa Afrika wasiwe watazamaji, wawe washiriki wa uchumi.

"Kunatakiwa kuwepo na matumizi ya sayansi na teknolojia katika ufundishaji. Kila shule inatakiwa kuunganishwa na intaneti," amesema.

Huku akitoa mfano wa janga la corona, Kikwete amesema limethibitisha jinsi ukosefu wa teknolojia unavyoathiri ufundishaji.

"Tumeona wakati wa corona, moja hatua zilizochukuliwa ni kufunga shule. Wanafunzi wetu hawakusoma, wanacheza rede, lakini nchi zilizoendelea shule zilifungwa na watoto wakaendelea kusoma.”

"Nilipokuwa Rais tulianzisha matumizi ya intaneti katika ufundishaji, tuliwekeza sana kwenye mkongo wa Taifa. Lengo langu lilikuwa ni kuhakikisha kila shule, hospitali ziunganishwe na intaneti. Mwalimu mmoja wa hisabati afundishe nchi nzima,” amesema.

Kuhusu Elimu jumuishi ameitaka Serikali na wadau kuhakikisha hakuna mtoto anayebaki nyuma kwa kukosa elimu.

"Wengine wanadhani msichana ni wa kubaki jikoni. Wengine wameachwa nyuma kutokana sababu za kisiasa.

Tunatakiwa kuhusisha mashirika yasiyo ya kiserikali kuchangia elimu," amesema.

Awali akimkaribisha Kikwete mwenyekiti wa Tenmet, Dk John Kalage ambaye pia ni mkurugenzi wa taasisi ya HaliElimu amesema kongamano hilo litajadili kwa kina njia za ufadhili wa elimu nchini.

Chanzo: Mwananchi
This is pumbav! Akili inayokuja baada ya kutoka madarakani ni pumbav kabisa! Kikwete angewezaje kuanzisha ufundishaji wa mtandao wakati pesa yote ilikuwa inaibiwa on his watch? Mradi pekee mkubwa ulikuwa ni Mloganzila kwa miaka 10 ya utawala, averaging a total budget of over TZS 170 trilioni in 10 years. Nchi ambayo watu walikuwa wanabeba pesa za escrow yeye anasema siyo za umma, ni za watu binfasi. Hopeless!

Shame upon his shameless face.
 
Hujamuelewa mzee😂😂😂
Mzee anamaanisha ukuaji wa Elimu yetu Ni lazima uendane na ukuaji wa Teknolojia. Hivyo vyote vinategemea bajeti imara.

Kama kasi ya ukuaji wa elimu yetu iko nyuma Sana dhidi ya kasi ya ukuaji wa teknolojia Basi wahitimu wa wa kiafrika watapokonywa ajira zao.

Itakapofikia hatua watu walioendelea kutengeneza maroboti madereva, Tiketi kukatwa kwa kadi, huduma kwa wateja Ni roboti, na kila kitu. Sisi Waafrika tutakuwa watazamaji na wahitimu watashindwa kuajirika maana Teknolojia imewatupa mkono kwa sababu hatutaweza kuendesha roboti Wala kuzitengeneza.
Hako ka mtu hakastahili hata kusikilizwa. Kama ni theory za uchumi tumeshazisikia sana madarasani kwa walio na uwezo kuliko yeye. Nini anachoweza kutuonesha kuwa ni matokeo ya utawala wake kwa miaka 10?
 
Hako ka mtu hakastahili hata kusikilizwa. Kama ni theory za uchumi tumeshazisikia sana madarasani kwa walio na uwezo kuliko yeye. Nini anachoweza kutuonesha kuwa ni matokeo ya utawala wake kwa miaka 10?
Sasa hivi kuna mabinti wengi sana wanafanya shughuli wasizostahili.

Halafu ukiwaangalia ni mabinti warembo kweli na wamesoma shule za gharama sana.

Mtaji wanaotumia kufanya hizo biashara ni ndogo kuliko hata hizo ADA walizopoteza huko shuleni.

Sasa mtu unabaki unajiuliza maswali tu! Watu kama hawa siwangeenda kusoma shule za kawaida.

Halafu hizo PESA walizopoteza huko wangezitunza kwa ajili ya manufaa ya baadae.
 
Utoaji wa elimu una gharama zake. Kama serikali haiwezi kucover gharama hizo, nchi inakuwa na majengo ya shule na wanafunzi bila kutoa elimu. Gharama kubwa ambayo serikali imejisahau kabisa ni mishahara ya waalimu, badala yake serikali imejaza malipo kwa wabunge na wanasiasa tu, halafu wanakuja kulalamikia elimu.

Mimi nilipokuwa darasa la kwanza Mwalimu mkuu wetu (alikuwa anavaa kaptula nyeupe au khaki, shati nyeupe, tai nyeusi, na stocking nyeupe) alikuwa na gari moja na pikipiki moja. Halafu mwalimu mkuu msaidizi na baadhi ya waalimu waandamizi walikuwa na pikipiki au vespa; vyote vikiwa vimetokana na mishahara yao tu. Leo hii sidhani kama kuna mwalimu anaweza kununua pikipiki ya mchina kwa kutumia mshahara wake tu bila kufanya misheni. Mwalimu anayeingia darasani akiwa na mawazo ya atakula wapi siyo tu kuwa hawezi kuandaa masomo yake vizuri bali pia hawezi kufundisha darasani ila atapiga blah blah ili muda uishe kusudi akafanye mambo yale yanayompa mlo.

Posho za wabunge zinatakiwa zifutwe kabisa zielekezwe kwa waalimu; mbunge akifanya kazi yake analipwa mshahara, siyo alipwe mshahara na posho huku mwalimu halipwi mshahara wa kutosha na wala hana posho yoyote.
 
Kuna wanafunzi wa St MARY GORETI wanauza MITUMBA pamoja na NGUO ZA NDANI [ 👙 ]

Na kuna wanafunzi wa MAUA wanachonga milango ya mbao [ 🚪]

Ukiangalia vyeti vyao ni vizuri kweli!

Lakini nenda TAMISEMI sasa! Ni madudu tupu 😆😆😆

Aah! Yaani hii NECTA ni KOMEDI 😂😂😂
Elimu haipo ku kufanya uwe Tajiri ama upate ajira nzuri tu,

Anaweza akachonga milango ndio, ila akachonga milango mizuri ambayo mwanzo haikuepo,

Elimu huondoa ujinga na kukupa maarifa mapya, huondoa wasiwasi usio na maana na kukupa maisha yenye Amani,
 
Back
Top Bottom