Kikwete kuondolewa uenyekiti CCM

Status
Not open for further replies.
The biggest ever mistake done by J.K was to chess away Pro. Mangula as CCM Chairman...hapo JK kajamb.ia jivu na lishatawanyika....let him go!!
Mangula hajawahi kuwa mwenyekiti labla umepitiwa kidogo. Ninachokifahamu huyu bwana aliwahi kuwa katibu mkuu wa magamba nafasi ambayo kwa sasa inashikiliwa na gamba lingine kwa jina la Mukama.
 
Mmh! hv hizi ccm movies hazijaisha,inayokuja cjui part ya ngapi ngoja tusubiri tuone labda watafanikiwa kimaudhui.
 
hata wakivuana wooote nyadhifa hadi selikalini ccm hakuna mwenye akili hata 1 angalia walivo feli kutatua mgogoro wa mgomo wa madaktari hii wiki ya 3 sasa hawajui hata wafanye nini, hivi kama ungekuwa ni uvamizi wa mipaka taifa lingekuwa mateka? Kikwete mwenyewe karudi badala ya kutatua tatiza yuko bize na kufungua benki. Ovyo kabisa
Wewe Hujui kuwa Kikwete naye Doctor! So Naye Yumo kwenye Mgomo...
 
Acheni kujadili ndoto. Hakuna mwenye ubavu wa kumtoa hata kujaribu kutoa wazo la mfano kikaoni. Unafiki tu 100%.
 
Sidhani kama Tanzania tume mature vya kutosha kisiasa kutuwezesha kuwa na kofia hizi mbili chini ya watu wawili tofauti bila ya kuleta migogoro ya uongozi. Binafasi nadhani litakuwa kosa kubwa sana kufanya hivyo kwani tofauti na nchi nyingine zilizoendelea ambako wenyeviti wa vyama husika mara nyingi (kama sio zote) huwa hawajihusishi na mbio za Urais, kwa Tanzania hali ni tofauti. Kumtoa Mwenyekiti wa sasa wa CCM katika nafasi hiyo kitatuletea vurugu nyingi sana kuelekea 2015. Sioni kama ujio wa mwenyekiti mpya utamaliza migogoro ya sasa kwani tatizo lililopo sasa ni pana sana. Hata hivyo kikao chenye mamlaka ya kumtoa mwenyekiti na makamu wake ni Mkutano Mkuu wa Taifa, na haujawahi kufanya hilo, na badala yake wenyeviti waliopita aidha waliondoka kwa hiari zao au baada ya kumaliza muda wao wa uongozi. Itakuwa ni maajabu ya kihistoria kama hilo litafanikiwa. Napinga hoja.
 
Wewe umeishiwa ya kuandika humu kauze Mananasi kwani ni msimu wake hilo unalolifikiria hata dalili haipo kwa sasa! JIPANGE Pumbavu
 
Ni tetesi za siku nyingi, inasemeka walionnusuru April, 2011 ni akina Dr Mwakyembe, sasa anaumwa sijui kajipanga vipi? siasa za CCM ni lafu na faul tu kwa kuwa sasa hakuna refa, baada ya Mzee kawawa kuondoka, mzee aliyebaki hawezi kuwa msimamizi maana na ni mchezaji wa timu nyingine, kazi ipo
 
1985 akina komba waliimba sana wimbo wa kutenganisha kofia mbili, nyerere akabaki na moja mwinyi akachukua nyingine......... wakaenda wakafika mahari wakashindwa fanya kazi kwa sababu ya kuto jiandaaa, maana Usalama wa Taifa walipoteza direction, walidhani bado wanatakiwa kuripoti kwa mwenyekiti wa CCM wakati bosi wao sasa ni rais....sasa baada ya vyama vingi kulikuwa na haja ya kuanda katiba mpya nchi ambayo ingeweka bayana hayooooo, sasa CCM wakadhani mambo yatakwenda kama wanavyotaka for life, sasa unefika wakati yanawatotkea puani sasa

Sidhani kama Tanzania tume mature vya kutosha kisiasa kutuwezesha kuwa na kofia hizi mbili chini ya watu wawili tofauti bila ya kuleta migogoro ya uongozi. Binafasi nadhani litakuwa kosa kubwa sana kufanya hivyo kwani tofauti na nchi nyingine zilizoendelea ambako wenyeviti wa vyama husika mara nyingi (kama sio zote) huwa hawajihusishi na mbio za Urais, kwa Tanzania hali ni tofauti. Kumtoa Mwenyekiti wa sasa wa CCM katika nafasi hiyo kitatuletea vurugu nyingi sana kuelekea 2015. Sioni kama ujio wa mwenyekiti mpya utamaliza migogoro ya sasa kwani tatizo lililopo sasa ni pana sana. Hata hivyo kikao chenye mamlaka ya kumtoa mwenyekiti na makamu wake ni Mkutano Mkuu wa Taifa, na haujawahi kufanya hilo, na badala yake wenyeviti waliopita aidha waliondoka kwa hiari zao au baada ya kumaliza muda wao wa uongozi. Itakuwa ni maajabu ya kihistoria kama hilo litafanikiwa. Napinga hoja.
 
Likifanyika hilo na parapanda za mwisho wa dunia zinaanza kulia, malaika wanakuja kuvuna ulimwengu. Hakuna mwenye ubavu huo.
 
Wakuu mpango huu nilisikia unaratibiwa na Lowasa. Hii NEC iliyopita ambapo EL alifunguka kuhusu Richmond ndo uitakiwa utekelezwe. Ambacho kingetokea ni pale baada a EL kufunguka, lazima wapinga ufisadi nao wangejibu mapigo wakiongozwa na 6. Ingetokea tafrani ya hoja humo ndani na ingeonekana M/Kiti ndo anakiharibu chama na EL alishandaa watu wake ili hoja ya kutokuwa na imani na JK ikianzishwa ipate kura nyngi za Ndiyo.
Mkapa aliliona hilo mapema ndo maana baada ya EL na Sumaye kuongea, akamwambia JK aifunge hiyo hoja na mambo ya kujivua gamba yarudi ngazi za chini.
Kama mnakumbuka, Nape alikuja kulalamika sana kuwa kuna watu wanataka kumpindua M/Kiti wake.

My take: Richmond lazima iondoke na mmoja btn JK and EL. Let wait and see hasa mwaka huu wa uchaguzi ndani ya CCM japo mabadiliko yoyote hayatakuwa na tija kwa taifa maan wote ni wezi. oh no ni majambazi.
 
Walishindwa NEC wataweza sasa? Kabla Kikwete hajaondolewa Ataanza Lowasa na Chenge,Kikwete hawezi kuvuliwa uenyekiti kwa mbinu chafu za mafisadi,,ingawa Lowasa amewanunua wajumbe wa NEC na wabunge wa CCM asilimia kubwa
 
Yetu macho ila kwa wanaccm na mfumo wao mwenyekiti wake anakua na taarifa au mikakati yoyote ile kabla ya mwingine yeyote hivyo si lahisi kushindwa kuchukua hatua kabla la kutokea alijatokea.Ila kwa wajasili na wenye roho ngumu wanaweza kujalibu.ila jibu lao analo mwenyekiti wao.Yatakayojili ni uondo kwetu.
 
Status
Not open for further replies.
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom