Kikwete for London Family Planning summit

anakereka nawale watoto wake wengi na jinsi wajukuu wanavyozidi ikulu so ameenda kujifunza njia mbadala
 
Mkuu Per diem,Show off,na mengine kama hayo yanahusika kwenye hili.Coz asipo safiri vijana wizara ya mambo ya nje wanazishughulikia.
 
Wakubwa, hivi hamjui rais wetu ni ******? Hata kikundi cha ngoma kikipita karibu na mageti ya magogoni kitamsomba mpaka kariakoo ati...leo ninyi mnashangaa safari ya maujiko majuu!
 
Kikwete amekwenda kujifunza kupanga uzazi bila shaka ukiachia mbali kuwa mbali na presha ya mgomo unaoendelea kuivua nguo serikali yake. Kesho utasikia kuna mkutano wa kusaidia watu kupanga jinsi ya kupanda miti kwa mistari atahudhuria. Hujakaa sawa utasikia kaenda umoja wa mataifa kuhudhuria kikao cha kumjadili osama bin laden ni upuuzi upuuzi mtupu.
 
Katika pita pita zangu nimeona ratiba ya mkutano huu na kugundua kuwa Mheshimiwa Rais anashiriki session ya Key Note panel ya heads of state saa 8:20 hadi saa 9:00 yas huko UK (rejea ratiba nimeambatanisha). Hata hivyo, kuna baadhi ya viongozi ambao hawakupata nafasi ya kuhudhuria na wame submit recorded statement (Mh Michael Bloomberg) au wataungwa kwa video conference (Rais Joyce Banda). Mambo ni kupanga ni kuchagua, waenda itika mwaliko na kwenda, waweza itika mwaliko na kushiriki kwa recorded statement / video conferencing au waweza kudecline mwaliko.
 

Attachments

  • Agenda - London Summit on Family Planning.pdf
    343.4 KB · Views: 42
Elimu haina mwisho, ajifunze tu kwani itamsaidia kutoendelea kuza* nje...
 
Hivi ana wake na watoto wangapi? na bado anaendelea kuoa na kuzaa? Itabidi aulizwe hilo swali na waandishi wa habari akirudi kama kutakuwa na press conference
 
I am sick to my styomach. Huyu ndiye rais wetu, Heri hata Matonya awe Rais kuliko Kikwete kuwa Rais. Matatizo lukuki nchini, bila aibu anaondoka kwenda kwenye family planning summit. This man is bogus. Mimi mwanamke lakini nadiriki kumuita Bogus. Mnyika alisema kweli. Huu ni udhaifu liopitiliza. Yaani bila aibu, huyu ni mtu wa aina gani jamani? Is this man normal?

JF Staffs, hii siyo sehemu ya masharti yenu?

1. Kumvunjia heshima, kumkejeli, kumtukana, mjumbe yeyote.


Wadau wengi wamekuwa wakiivunja kanuni hii ambayo tulikubaliana tangu 2006; haturuhusu kwa namna yoyote iwayo kuvunjiana heshima kwa makusudi wala matusi kwa namna yoyote iwayo. Mfano: Kuandika neno fvck kwa nia ya kukwepa censorship ni kutukana kwa kudhamiria kabisa, tumelishtukia hili na mara inapobainika hoja husika huondolewa na mhusika kufahamishwa juu ya kosa lake, anapothibitika kuendelea kukaidi basi hufungiwa kwa muda au kufutiwa uanachama kabisa!


2. Kuleta katika JAMII FORUMS maelezo yenye maudhui mabaya, au kuweza kuleta maudhi yoyote kwa wajumbe ama kwa wingi wake, ukubwa wake, au mfumo wake.
Hili nalo pia husababisha hoja za watu kufungwa, kufutwa au mhusika kupewa onyo.


3. Kuleta makala au kuendeleza mijadala yenye kuleta ugomvi, uchochezi na yenye muelekeo wa kutengenishana badala ya kuungana miongoni mwa wajumbe wa JAMII FORUMS na Watanzania wote kwa ujumla.
Nadhani maelezo yaliyo juu yanajieleza wazi, natamani wengi wangeelewa maana ya maneno hayo juu! JF si sehemu ya kuanzisha uchochezi aidha wa kidini, kisiasa n.k.


Endapo itabainika umeanzisha hoja kwa nia ya kuibua uchochezi au ugomvi na mtu basi tunasikitika hoja hiyo itakufa HARAKA SANA.


4. Kuleta maongezi binafsi baina ya mwanachama na mwanachama (waliojisajili) waliyoongea kwa kuaminiana kutoka katika Private Messages (PM) au barua pepe (Emails) na kuyaanika hadharani kwa nia ya kuchafuana.
Kuna wadau walikuwa na kawaida ya kuwasiliana na wenzao kwa mapenzi yao wenyewe au hata bila wao kuhitaji, namna pekee ya kuwasilisha PM au email ambayo unaona inaleta tatizo kwako si kuibwaga katika hadhara bali kuituma kwetu na sisi tukaifanyia uchunguzi na kubaini ubovu wa PM wenyewe au Email husika ili mhusika achukuliwe hatua za kinidhamu. Tunalichukulia suala la PM na Emails kuwa private, kulileta hadharani ni kutafuta magomvi na kudhalilishana.


5. Kusambaza kwa makusudi au kwa uzembe barua zenye virusi vya kompyuta.


Kwa bahati hili halijatokea sana JF, threads ambazo zinakuwa zinaonekana kuwa na links ambazo si salama huwa zinaondolewa haraka, aidha waanzishaji wa hoja husika hufahamishwa lakini wakionekana kukaidi hatuna sababu za kuendelea kuwasiliana nao badala ya kuwafungia kwa muda (kutokana na kukaidi) na kisha kuanza kuwa-monitor kadiri siku zinavyokwenda.


6. Kutoa maelezo au shutuma dhidi ya mwanachama mwenzako, kiongozi wa au watu wenye hadhi kijamii bila kuwa na ushahidi wa kutosha kwa lengo la kuchafua rekodi safi ya mhusika kijamii.
Wahusika mnaovunja sheria hii mnajua athari yake; tunaweza kuwa tunachukizwa na kitu flani kilichofanywa na kiongozi flani ndani ya serikali au kidini, kuanzisha shutma ambazo zinalenga kumchafua mtu bila kuwa na ushahidi ni kutaka kumchafulia jina mhusika. JF si sehemu ya kuchafuliana majina, hatua za kinidhamu huchukuliwa kwa wale wenye nia ya kuitumia JF kwa maslahi yao binafsi.


7. Ni sharti kwa kila mwanachama kutoa maelezo au mchango wake kwa uwazi na ukweli na kutomuogopa yeyote wala kumpendelea yeyote bali kuweka mbele maslahi ya taifa.
Tunaheshimu SANA hoja za kila mmoja, kuna wadau walikuwa wanadhani huenda wao si mali kitu hapa JF, tunatambua kuwa Mwenyezi Mungu katujalia karama tofauti, lakini wakati huohuo tunaamini kila mmoja anaweza kubadilika kadiri siku zinavyokwenda. Hakuna mwanachama wetu ambaye tunamwona "mbabe" dhidi ya wenzake, wote ni sawa mbele zetu na tunawapa heshima sawa.
 
Muuaji mwache aende zake! siye tupige maombi tu hiyo ndege isimrudishe hapa! afie huko huko!
 
naomba mtuambie hii ni safari ya ngapi? Hivi hakuna mtu anayaweza kutupa gharama ya safari hizi kisha tulinganishe na tija yake. Watu wanakufa rais yuko londone. Only in tanzania.

mjumbe aweda ni london siyo londone, (mji mkuu wa united kingdom -uk) karibu na great britain kule england nchini uingereza. Upo mjumbe?
 
Kwanza inanishangaza Rais wa nchi kwenda kujadili mambo ya uzazi wa mpango na kuacha mambo mengine ya muhimu zaidi, ikiwemo kutafuta suluhisho la madaktari. Kwani alikosa mwakilishi yeyote kutoka hata wizara ya afya au kwenye taasisi na wanaharakati kama TGNP na kadhalika? Hata mke wake mama Salma angeweza enda. Yaelekea huyu baba anapenda safari sana. Inaniuma kwa kweli kumuona Rais wa nchi yangu akiwa so silly...hiyo miaka ilobaki iishe tu aondoke madarakani.
 
Ni aibu aibu aibu na aibu kwa kiongozi wa nchi kusafiri kwa kiwango hicho. Huyu bwana hata mkutano usio na maana kabisa anahudhuria, aibu gani hiii jamaniiii!!!!
 
Back
Top Bottom