Kikwete apokea Ripoti ya EPA ajiandaa kuhutubia Taifa!

Waitttttttt! Haipandi na akili haikubali? Au Mkulu ameona aijumuishe kwenye hotuba yake wiki hii. Lets wait
 
Katika hali isiyotarajiwa, waandishi wa habari waliokuwa wamekwisha kuingia ndani ya viwanja vya IKULU kuhudhuria uwasilishwaji wa kile kinachoitwa "Taarifa ya EPA" walijikuta wakirudishwa na kuambiwa watajulishwa ni lini au muda gani wataitwa tena.

Wakati huo Mwenyekiti wa Task Force iliyoundwa na Rais Jakaya Kikwete kuchunguza na kuchukua hatua dhidi ya wahusika wa EPA, Mwanasheria Mkuu, Johnson Mwanyika, alikuwa ndani ya majengo ya IKULU.

MASWALI YAMEIBUKA:
1. Je, Rais alipata dharura ya kukosa muda wa kuipokea?
2.Je, Rais hakuridhishwa na maelezo ya kina Mwanyika kuhusu taarifa yao?
3. Je, Rais ameshitushwa na taarifa hiyo kutokana na kugusa wengi?
4. Je, Rais aliona ni bora aisome kwanza ili akiipokea awe na cha kusema?
5. Je, Rais ameona hakuna sababu ya kupokea mbele ya waandishi?
6.Je, Rais aliona ni bora wahusika wachukuliwe hatua badala ya taarifa?
7. Je, Kina Mwanyika wamemwambia kazi bado nzito?

Na mengine mengi waandishi wamejiuliza na wananchi watajiuliza pia, JF munasemaje?

Halisi

Hapo ipo kazi Mkuu, yawezekana jamaa kachungulia hiyo ripoti akaona, WATAMTOA NISHIA, AKJISEMEA FUNIKA KOMBE MWANAHARAMU.......
 
Hapo hapo kuna usanii unataka kufanyika kuwasafisha baadhi ya vibopa walio tajwa mara ya kwanza kwa hiyo wamesahau wakawaweka ndani sasa wanataka kurekebisha mambo nyie tulieni hakuna kipya hapo ni sanaa tu inafanyika.Walisema serikali ina mkono mrefu sasa kwa issue ya EPA naona serikali ina mkono mfupi sana inashindwa kuwafikia baadhi ya watu flani flani wanao zidi kuneemeka.
 
kama kweli

... kama kweli tume ya rais imefanya kitu ambacho wananchi tunataka ifanye, basi kamwe hiyo ripoti haitakuja kusomwa mbele ya waandishi wa habari au hadharani labda iwe edited.
 
Katika hali isiyotarajiwa, waandishi wa habari waliokuwa wamekwisha kuingia ndani ya viwanja vya IKULU kuhudhuria uwasilishwaji wa kile kinachoitwa "Taarifa ya EPA" walijikuta wakirudishwa na kuambiwa watajulishwa ni lini au muda gani wataitwa tena.

Wakati huo Mwenyekiti wa Task Force iliyoundwa na Rais Jakaya Kikwete kuchunguza na kuchukua hatua dhidi ya wahusika wa EPA, Mwanasheria Mkuu, Johnson Mwanyika, alikuwa ndani ya majengo ya IKULU.

MASWALI YAMEIBUKA:
1. Je, Rais alipata dharura ya kukosa muda wa kuipokea?
2.Je, Rais hakuridhishwa na maelezo ya kina Mwanyika kuhusu taarifa yao?
3. Je, Rais ameshitushwa na taarifa hiyo kutokana na kugusa wengi?
4. Je, Rais aliona ni bora aisome kwanza ili akiipokea awe na cha kusema?
5. Je, Rais ameona hakuna sababu ya kupokea mbele ya waandishi?
6.Je, Rais aliona ni bora wahusika wachukuliwe hatua badala ya taarifa?
7. Je, Kina Mwanyika wamemwambia kazi bado nzito?

Na mengine mengi waandishi wamejiuliza na wananchi watajiuliza pia, JF munasemaje?


Majibu jumatano......i hope so....

Tanzanianjema
 
Lakini ni kipi kinachopmfanya rais wetu aonekane ameshindwa? Ukisikiliza maneno yake na kusoma mikakati yake, inaonekana kuwa ni mizuri sana. Kwa nini utekelezaji unakwama? Ni tatizo la rais mwenyewe au wasaidizi wake? Nauliza hivi kwa sababu imefika wakati watu wengi wenye shida wanaamua kukimbilia wka rais mwenyewe kuomba msaada. kwangu mimi hii inamaanisha kuwa waliotakiwa kuyatatua matatizo hayo (wasaidizi wa rais) hawafanyi kazi yao sawasawa. Tuendelee kumlaumu kwa makosa ya wasaidizi wake pia? labda hapa kosa lake ni kutowabadilisha haraka iwezekanavyo na kuchagua timu itakayom,pa ushirikiano wa kutosha.
Lakini pia kuna uwezekano kuwa kuna kitu kinamfanya ashindwe kuyafanya hayo mabadiliko ambayo tunayatamani. Ukisikiliza maneno yake, anaonekana kuwa ni mtu anayependa kuifanyia kitu fulani nchi lakini inaonekana kuna kitu kinamkwamisha
 
Inahitajika imani ya hali ya juu (kama ya kumwezesha mtu kutembea juu ya maji) kuweza kuziona pumba za "mtalii/msanii no. 1" JK, kuwa mchele. Na wadanganyika ni watu wa imani kweli kweli. Tembelea nyumba za ibada utaelewa ninachoongelea.

Kwa kuwa bunge la Tz lina sehemu mbili: kichwa kikiwa ni raisi wa jamhuri, basi bunge letu la wawakilishi wa wananchi litapaswa kupiga makofi na magoti wakati wa hotuba ya bwana mkubwa.
 
Hivi bado mwanyika anataka kuwasilisha ripoti wakati yeye aliambiwa awachukul;ie hatua watakaobainika kuwaibia wananchi?!!!!!? Si ajabu rais amekataa, atakuwa amemwambia akatekeleze maagizo na si kuleta siasa
 
Halisi,


Kumbuka ilitakiwa wachukuliwe hatua na si kuwasilisha report kwa mbwembwe na kuwaita waandishi wa habari.

Muungwana kaona si vyema kufanya mbwembwe cha muhimu zaidi ni hatua za kuchukuliwa.

Safi sana Muungwana!
 
Waandishi; haya ndio maswali ambayo wananchi na wapiga kura wa TZ wangependa kuyauliza na kupatiwa majawabu; itakuwa ajabu kama wananchi hawataelimishwa na vyombo kuyajadili mapema ili rais ayatolee majibu tutaletewa ngonjera zisizo na tija za Zimbambwe oohh africa kusini, ooo ziara ya iringa nk. Tunaka pamoja na mambo mengine aje ajibu maswali yaliyo jikita kwa Richmond/EPA/IPTL kuvunjwa?/Zanzibar ( CCM/CUFG mwafaka pamoja na hadhi ya ZNZ),walimu na malipo, wafanyakazi na vitisho kukomeshwa dhidi ya wafanyakazi na kumtimua Waziri aliyetishia wafanyao kazi( HG), wasi wasi ni kuwa ataendelea kutoa ahadi tena, nK. Haya vyombo vya habari ni juu yenu kuelimisha sasa umma habari sio sahahi sio za kuzushi kwa mstakabali wa taifa letu ili kama rais hatatoa majibu tumhoji kulikoni; je bado anataka kuendelea au labda amechoka; isije kuwa anakuja kutangaza kujiuzuru maana baada ya ziara amegundua hakuna maisha bora na hivyo kamaa muungwana anataka aachie asije kulaumiwa baadaye; hilo nalo litakuwa jema kabisa
 
Nina wasiwasi kuwa atawatangaza watakaofilisiwa mali ,wahusika wa ufisadi watakaokamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria vile vile huenda akatangaza kamati mpya ya kuchunguza tuhuma anazoshutmiwa Mkapa , bila ya kukosea atalizungumza suala la Muungano na hapa itaonekana hekima zaidi akijaribu kutuliza mpira kwa kuzidisha hilo atawazungumzia wahusika waliojadiliana suala hili katika vita vya maneno aidha kwa kuwataja mmoja mmoja au kwa kuashiria kwa maelezo atakayotoa ,hekima itatumika katika kuwafahamisha ikiwa kila mmoja atamhusisha na kosa lake katika kuitetea au kuipinga Kauli ya Pinda. Hivyo atajaribu kuweka mambo droo.
 
Mbona Wengi Mmekuwamnamuandama Rais Kikwete Hapa Kunaoneka Kwa Uwazi Kuwa Wengi Wenu Mnataka Aonekane Kushindwa Kwa Sababu Ambazo Wengi Miongoni Mwetu Tunajuwa Hamkufurahi Huu Jamaa Awe Rais Ilikuwa Ni Mbinu Tu Zakumtumilia Ili Mfanikiwe Na Yenu Halafu Mpite Mkisema Kuwa Mmnaona Hawa Watu Wako Vile Na Hivi Tunaelewa Nini Kinafatia Katika Kumuangusha Kikwete Lakini Mungu Atampanguvu Imara
 
Kupokea ripoti kwa mbwembwe au kimya kimya yote si muhimu,la muhimu ni hatua kali za kisheria kuchukua mkondo wake na wezi wote kuadhibiwa.
 
“Kwa ajili hiyo Rais ameamua mambo yafuatayo. Rais amewaagiza; Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (PCCB), kuchunguza na kuchukua hatua zipasazo za kisheria kwa makampuni na watu waliohusika na uhalifu huu…
“Rais amewataka watumie ipasavyo mamlaka na madaraka waliyonayo kwa [/COLOR]mujibu wa sheria. Aidha, amewataka wakamilishe kazi hiyo katika kipindi cha miezi sita. Amemwagiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali awe kiongozi wa kazi hii…Amewataka wahakikishe kuwa fedha zilizolipwa isivyo halali zinarudishwa,” (Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo Januari 9, 2008.)
 
Back
Top Bottom