GE2010 Kikwete aanguka ghafla Jangwani...!

GE2010 Kikwete aanguka ghafla Jangwani...!

Inawezekana raisi hamsikilizi daktari wake ! na daktari naye hajaamua kujiudhuru kwasababu decision algorithm yake haijafika mwisho...

Mkuu .... usiweke "dh" kwenye hili neno ...... ole wako Kiranga akusome...lol
 
Ushauri wangu kwa wanajukwaa wote, ukiweka mbali siasa za vyama sisi sote tu watanzania. Linapotokea jambo lisilo la furaha na tulipokee hivyo kama Watanzania, la Furaha nalo tulipokee kama Watanzania. Jambo la kuanguka Raisi wa Nchi si jambo dogo, linaweza hata kuathiri bei za Hisa za Makampuni yalijaindikisha DSE. Tucheke pale panapostahili kucheka, panapohitaji pole na tuseme pole, ushabiki mwingine haujengi!!!
 
Hakuna uchawi. Isipokuwa JK anapenda kusafiri mno. ndiyo maana anachoka. Rest & Restoration ni mojawapo ya vitu vinavyopima mafanikio ya mtu. Kwa hili JK hajafanikiwa kwa afya yake. Anafikiri ujiko kuzururazurura. Hata ziara zinazo hitaji wakuu wa wilaya tu, yeye yumo!!!!!!!

Hakuna la safari na wala baba yake safari: JK ni mgonjwa tu period. Kwani alipoanguka mwanza alikuwa amefunga???? Hivi kwa nini tusijiulize vipi daktari wake alipotoa riport alimtetea sana kuhusu afya yake. Sasa mbona leo mpaka sasa yuko kimya.... Watatunga sababu kibao lakini Mungu atawaumbua tu....!!! Waache walete mchezo tu siku ataanguka asiamke. Ndo wonder yeye mwenyewe anakwenda kupima akili USA, labda alifikiri ataambiwa yeye ni kipanga wa TZ..............!!!!
 
Ushauri wangu kwa wanajukwaa wote, ukiweka mbali siasa za vyama sisi sote tu watanzania. Linapotokea jambo lisilo la furaha na tulipokee hivyo kama Watanzania, la Furaha nalo tulipokee kama Watanzania. Jambo la kuanguka Raisi wa Nchi si jambo dogo, linaweza hata kuathiri bei za Hisa za Makampuni yalijaindikisha DSE. Tucheke pale panapostahili kucheka, panapohitaji pole na tuseme pole, ushabiki mwingine haujengi!!!
Mbona yeye huwa anacheka cheka tunapomwambia vitu serious kuwa maliasili zinakwisha lazima equilibrium iwepo, angekuwa rais serious na anaonekana kuwa na uchungu na wananchi wake na mali ya taifa sidhani kama kungekuwa na komenti unazoziona leo.
 
Hii inashangaza sana. Hebu sote tuwe makini na tujiulize maswali haya?

1. Huyu ni Rais wa nne Tanzania Bara, je wale watatu waliopita walianguka mara ngapi?
2. Kwani wao hawakuwa na kazi nzito kama yeye JK kwa sasa?
3. Awamu ya pili alikuwa ni his ex Mzee Mwinyi, na alikuwa ni moslem!! Je alianguka mara ngapi jukwaani au popote au hata kuzimia?
4. Huyu Rais wetu JK ameshaanguka mara nne public, na hatujui private ni mara ngapi?? Je hatujaweza kuona kuwa kuna hutilafu kubwa sana katika mwili wake na afya kwa ujumla?
5.Saumu ya masaa machache haiwezi kabisa kumwangusha mtu mwenye afya yake. Ninafahamu daku huliwa usiku, say kama hata amekula daku saa 2 mbili usiku, bado ana uwezo wa kushinda njaa kwa masaa mengi sana. Mbona wakristu wakifunga ni say kuanzia saa mbili usiku baada ya dinner na hakuna cha daku na bado hata hawasinzii ofisini? Tuwe tunajadili masuala kwa upana!! Afya ya huyu mheshimiwa ni zaidi ya ujuavyo!!
6. Ni kweli Dr. Slaa alianguka bafuni Mwanza na kuvunjika mkono, kumbuka kuwa mahoteli mengi yanatumia tiles za bafuni imara kiasi gani? Tena ukizingatia ni za China mara nyingi? Ile ilikuwa ni accident, hii ya JK si accident, ni madhaifu ya afya yake.

Watanzania wote, ni vema tufumbue macho na kuvaa kiona mbali kuhusu afya ya huyu mtukufu wetu!! Ifahamike kuwa ugonjwa hauombwi na kila mtu angefurahi kama asingeugua, ila basi unapoumwa ni vema ukaweka wazi, hata kama si details but tunajua kabisa huyu ndugu pengine ana low/High BP/Sugar and many other serious illiness!! Kulikoni kujitafutia visingizio lukuki, mara saumu kali, mara alisafiri mno hajapumzika ndiyo maana mwili umeishiwa nguvu, etc, etc. Hivi kweli kama unajua kuwa huna stamina ya kustahimili kazi nyingi ni kwa nini usi-delegate? (Hapa ni kwasafari zaidi).

Pole Rais, pole sana, weka wazi afya yako ilii tukuombee. Ugonjwa ni jambo la kawaida!!Hakuna atakayekunyang'anya hicho kitu eti kwa kuwa umeweka bayana afya yako. Mtasema pengine ugonjwa ni siri ya Dr. na Mgojwa, ni kweli ila magonjwa kama lilivyo general si siri, pengine details zake ndiyo siri. Kwani nini bwana!! Mimi nitasema tu, mbona hata wenye ukimwi wameamua kuvunja ukimya siku hizi na hawaogopi? Sembuse wewe mheshimiwa ambaye tatizo lako ni la kawaida si ukimwi??!!

Dr. wa Rais, tafadhali eleza report ya kiukweli, not propaganda!! Ugonjwa hauna propaganda!! Au ikiwezekana apumzike, bado ataendelea kupata maisha bora kama Rais mtaafu tu na aweze kuishi maisha marefu. Msimchoshe tafadhadhali. Mpeni ushauri wa ukweli.

Mkuu huwa tunajisahau sana kuwa hakuna Rais wa Tanzania bara!
 
Ushauri wangu kwa wanajukwaa wote, ukiweka mbali siasa za vyama sisi sote tu watanzania. Linapotokea jambo lisilo la furaha na tulipokee hivyo kama Watanzania, la Furaha nalo tulipokee kama Watanzania. Jambo la kuanguka Raisi wa Nchi si jambo dogo, linaweza hata kuathiri bei za Hisa za Makampuni yalijaindikisha DSE. Tucheke pale panapostahili kucheka, panapohitaji pole na tuseme pole, ushabiki mwingine haujengi!!!

Hizo hisa na zianguke tu! Kama ni mgonjwa na hataki kuwapisha wenye afya wasimame kugombea kumbe tusemeje? Kura hapati period!:mad2:
 
Guys lets be honesty on this issue...i ve never ever heard President fall down on stage in this world!!!Ni Tz tu nimeona,hivi kweli mtu kama Obama au David Cameroon usikie kaangua jukwaani sijui maelezo yangekua kama ya kwetu ya kujikanyaga!
I think we need to be more serious with president health..waseme ukweli kuna nini????
 
Form seven in taabu kwel kwel

hahaaaa eti yuko mwanza na jana kaonekana kapanda ndege saa 6 dakika 48 machana amekwenda nje kutibiwa..hahaaaa kumbe swaumu na glucose kushuka inatibiwaga ulaya.....
 
Ushauri wangu kwa wanajukwaa wote, ukiweka mbali siasa za vyama sisi sote tu watanzania. Linapotokea jambo lisilo la furaha na tulipokee hivyo kama Watanzania, la Furaha nalo tulipokee kama Watanzania. Jambo la kuanguka Raisi wa Nchi si jambo dogo, linaweza hata kuathiri bei za Hisa za Makampuni yalijaindikisha DSE. Tucheke pale panapostahili kucheka, panapohitaji pole na tuseme pole, ushabiki mwingine haujengi!!!

....ndio itaathiri bei ya hisa ...positivelly ....bei zitapanda....ikiwa na maana kuwa hata hiyo investors community haina confidence na kikwete......ukiniambia rais kama Obama akianguka bei zitashuka nitakubali.....au hata uganda na rwanda ....lakini sidhani kama kikwete wetu ana uwezo hata chembe..wa ku influence bei za hisa ..tusimvishe kofia isiyomkaa[who the cap fits ,let him weir it!!].......sana sana kikwete ana influence bei za bidhaa kupanda madukani....yaani hao wenye viwanda kila siku wanatupandishia bei za vyakula........kwa kuwa hawana uhakika na JK!!
 
....rudia hii habari ,hawajakusikia...

Kweli Mkuu, hii habari inahitaji kuongezewa nyama kidogo ili kitu kitoke mchicha. Vinginevyo utamu wake unapotea.

Hata hivyo, tukilinganisha JK na watu kama Mgabe, Kibaki na wengine wengi tu, nani alitegemewa kudondoka hadharani? Ni aibu kwa mkuu wetu wa nchi kuzimika zimika kama mshumaa halafu watu wanatuletea vijisababu vya kiswahili swahili. Inabidi tupewe maelezo ya kina kwa sababu Rais ni mtumishi wetu na tunalipa kodi ili aweze kutufanyia kazi. Jamani kuna mtu anaweza kuvumilia mfanyakazi wake ambaye afya ni mgogoro wakati kazi anayotakiwa kufanya ni ngumu sana?
 
ameanguka akisema..."tupeni ridhaa yenu, tutafanya zaidi..."
kudanganya umati wa masikini, mchana kweupe tena ukiwatazama machoni kuna ongeza stress na presha...
 
mungu amuweke hai ili ashuhudie kushindwa kwake na Dr. Slaa october
 
hakuanguka jumla mabodyguard wake walimuwahi kabla hajafika chini. Mbona hata Dr Slaa alianguka bafuni huko mwanza hadi kuvunjika mkono. wote wameanguka tofauti mmoja kaanguka bafuni mwingine jukwaani. hii ni bahati mbaya inaweza ikamtokea mtu yoyoye wakati wowote.

Kuna tofauti bana! JK kaanguka kwa kukosa fahamu, lakini Slaa alianguka wakati akiogea sabuni ya bamia!
 
Naomba mambumbumbu wa amani muache kuchochea chuki na hulka ya dharau katika nchi hii iliyojengwa kwa misingi ya heshima na upendo. Ndio maana Dr. Slaa alipodondoka na kuteguka mkono hakuna aliyesema RIP. Badala yake watu wote tulimuombea apone haraka aendelee na kazi za ujenzi wa Taifa. Muwe wastaarabu.

Jamani kusema ukweli ndo ustaarabu! au ustaarabu ni kunyenyekea upumbavu?
 
jamani hii video hapana..................imenibidi nimuonee huruma tu! sijamuonea huruma kama rais au ccm, ila kama mtu mzima, baba wa watoto, mwanamme, unaanguka kwa ugonjwa mbele ya watu, unabebwa kama mfu, kisha dunia nzima imekuona!

mmmh
 
Kweli nimetazama anavyoanguka kwenye hii video imeniuma sana na imenisikitisha. Katika hali ya ubinadamu, inasikitisha sana kuona binadamu mwenzio akizimika vile. Halafu alipoanza kusema 'aise' kabla hajaanguka, nadhani alikuwa anajisikia vibaya sana au maumivu lakini akajikaza aendelee na hotuba. Nimeumia pia jinsi sauti ilivyoanza kufifia kama anayetaka kutafuna ulimi, yaani kama ni ndugu yako yuko katika hali hiyo utatishika sana.

Kama kuna wanaofurahia kitendo cha binadamu mwenzao kuteseka vile mbele ya watu, hao ni makatili tu. Hakuna siasa hapa. Siasa ni kupingana kwa hoja na si kutakiana mabaya. Mimi napinga CCM kwa dhati, lakini nimesononeshwa sana na madhila yaliyompata JK pale jukwaani. Kama binadamu mwenye umri sawa na babangu, nimemtazama anavyoanguka kwa masikitiko makubwa, ikanijia picha kama babangu mzazi akianguka vile mbele ya umati, itakuwaje. Nimeumia sana.

Pole sana mheshimiwa, Mungu akujalie afya njema uwe salama, urudi kwenye mpambano. Tunahitaji mpambano baina ya watu walio wazima wa afya ndio maana napenda upone, tupate nafasi ya kukusikia katika kampeni, ujibu hoja zetu ukiwa mzima tufanye uchaguzi tukiwa tumesikia hoja za wagombea wote.
 
Back
Top Bottom