GE2010 Kikwete aanguka ghafla Jangwani...!

GE2010 Kikwete aanguka ghafla Jangwani...!

Rais alipumzika kidogo na akaendelea na speech. Hali ni nzuri na mambo ni shwari.

Hata kama we ni patriot, lakini usiseme usicho na uhakika nacho. Raisi amerudi jukwaani akajaribu kuhutubia kwa dakika chache na kisha akaaga na kuondoka huku watu wakishangaa shangaa.

Unadhani mkutano wa kampeni wa ccm jangwani unheweza kuisha saa kumi kasoro robo?
 
Kila binadamu anaumwa kwa wakati wake. Tumtakie kheri pamoja na tofauti zetu za kiitikadi.

mkuu hakuna mwenye kumtakia shari.......

swali ni kwanini ukweli hausemwi????????????!!!!!!!!!!
 
Ni kweli amedondoka madodyguard wa bongo ni wa hovyo wqamemwacha hadi mzee mzima analamba mchanga badala ya kumwahi asidondoke jumla!

Hakuanguka jumla mabodyguard wake walimuwahi kabla hajafika chini.

Mbona hata Dr Slaa alianguka bafuni huko mwanza hadi kuvunjika mkono. Wote wameanguka tofauti mmoja kaanguka bafuni mwingine jukwaani. hii ni bahati mbaya inaweza ikamtokea mtu yoyoye wakati wowote.
 
Naomba mambumbumbu wa amani muache kuchochea chuki na hulka ya dharau katika nchi hii iliyojengwa kwa misingi ya heshima na upendo.

Ndio maana Dr. Slaa alipodondoka na kuteguka mkono hakuna aliyesema RIP. Badala yake watu wote tulimuombea apone haraka aendelee na kazi za ujenzi wa Taifa.

Muwe wastaarabu.
 
Inawezekana ikawa ni saumu kutokana na mazingira yaliyopo. Bila shaka tangu asubuhi alikuwa na kazi nzito za kichama katika kuhakikisha maandalizi yanaenda vizuri. Pole yake.
Swaumu? Hakuna lolote anatafuta public huruma ya wananchi! Ah siasa kazi kwelikweli!
 
Kuanguka sio yeye tu kumbuka Dr Slaa aliaguka majuzi bafuni Mwanza na kuvunjika mkono,ile ni ajali kama ajali nyingine
 
Pole Jk, sijui unatatizo gani jamani, mbona kila mara jangwani kwenye uzinduzi waanguka.


kikwete ameshaanguka mara 4[nne] hadharani...yaani mara mbili jangwani na mara mbili kirumba mwanza [ikiwemo aliyoanguka kwenye shughuli ya kanisa la AIC-hakuwa amefunga ].....na pia amewahi kuzirai mara kadhaa akiwa ndani,.....according to insiders......

there is a problem ...!

pia nime note kwenye hutuba yake kuwa anasoma sana mitandao....ametoa moja " siku hizi tanzania kuna mitandao ...kwenye mitandao wanaandika sana sana ...lakini nawaambia kuwa ..watanzania hawadanganyiki..."
 
hakuanguka jumla mabodyguard wake walimuwahi kabla hajafika chini. Mbona hata Dr Slaa alianguka bafuni huko mwanza hadi kuvunjika mkono. wote wameanguka tofauti mmoja kaanguka bafuni mwingine jukwaani. hii ni bahati mbaya inaweza ikamtokea mtu yoyoye wakati wowote.

Lakini pale jukwaani hakuna utelezi! Isitoshe huyu JK ni mara ya tatu au ya pili hivi anadondoka jukwaani. Usilete za luleta hapa!!!
 
Nawashangaa sana CCM! Kwa nini wasitwambie ukweli ? Asiumwe yeye ni nani kwa sababu ni Rais, tukumbuke Rais hakujiumba mwenyewe.

ukweli upi CCM inaficha na Je CHADEMA inaficha nini kuhusu kuanguka kwa Slaa?
 
watu gani waliochoka,ni mtu mmoja asiye na akili timamu kachafua hali ya hewa.
 
Waungwana inayosemana JK kaaanguguka Jukwaani leo wakati wa kuanza kampeni je mambo yakoje,kwa mlio hudhuria!!!!????
 
rais ana afya mbovu na hafai kuongoza taifa hili..hatutaki sababu za kitoto za kila siku hapa mara kafunga eti swaumu kali...mbona watu huku vikindu wanafunga na hawaanguki
 
Hivi katika fomu nza NEC hakuna mahala unaulizwa iwapo una afya nzuri -- na hilo kuhakikiwa na daktari?
 
Back
Top Bottom