ukiangalia hiyo picha utaona makosa mengi mno ya hawa jamaa zetu wa UWT,
1) wote wamejitofautisha kabisa na Target (raisi), dress code yao inatoa mwanya mkubwa kwa snipers kujua nani ni nani, na hapo maana halisi ya bodyguard inapotea, ingekuwa busara kwa baadhi ya hao jamaa kuvaa nguo zinazofanana na Target,
2) ukiangalia hiyo picha, hicho kijiji chote cha UWT kimeconcentrate kwa Mgonjwa, na hakuna hata mmoja anaeangalia upende mwingine wowote, zaidi ya kuangaika kumbeba
3) Afya ya rais nadhani inajulikana zaidi na watu wa UWT, hivi kweli wanaweza kuja hapo au kutembea na raisi bila kuwa na kikosi cha Paramedics?, as far as i know hao jamaa wako trained kumguard huyo Rais, kwa hiyo palipaswa kuwa na kikosi kingine cha UWT ambacho kingefanya kazi hiyo ya kumzoa na kumshughulikia Mgonjwa wakati hao Bodguards wakiendelea na zoezi lao la ulinzi kama kawaida
4) nasema hao jamaa hawako trained kwa first aid, maana kwa ugonjwa wa kuanguka na hicho kiwingu kiasi hata huyo mgonjwa anakosa hata pa kupumulia
4) kunakuwaga na askari mwenye kitambi kikubwa nyuma ya raisi mara nyingi, vipi kwenye hii tukio hakwepo?, maana nadhani yeye ndio angekuwa wa kwanza kumdaka kabla hajafika chini, au yeye ni wa mapambo tu?