Tumain
JF-Expert Member
- Jun 28, 2009
- 3,154
- 70
Ninalozungumzia la Zanzibar siyo suala la term tatu tu (hiyo ni hoja ya kupandia mgongonai). Kimsingi hoja ni kuwa Zanzibar watataka makubaliano ya Muungano yazungumzwe tena na vipengele vya muungano viangaliwe ama sivyo wao wataamua kutoka nje ya Muungano. Wakichukua msimamo huo Zanzibar nzima italipuka kwa shangwe.
Kitakachotokea watu wenye asili ya bara wataanza kunyanyaswa na kutakiwa kuridishwa "kwao" bara na watakapochelewa chelewa damu itaanza kumwagika. Na ndipo tutaona maelfu ya wale wanaoitwa "Watanganyika" wakitafuta mahali pa kukimbilia...
Na tuombee hoja iwe hiyo ya kisiasa tu; itakapoingizwa hoja ya dini tu kama ambavyo imejaribiwa mara kadhaa, tutashuhudia makanisa yakitakiwa kufungwa siku za Jumapili na hata watu kulazimishwa kuondoka.
Kikwete hatojua la kufanya.
Na wewe sasa umeshakuwa yahaya makanisa yalikuwepo zanzibar kabla ya muungano hakuna mauaji wala utabiri wako wa kijinga, ni uchochezi na pengine ni ukereketwa na udini wako (ukristo)
Wanzizabar wanachouliza na wanachotaka ni maelewano katika muungano na in fact ukoloni wa Tanganyika uishe huko, wachague viongozi wao bila dodoma thing ..naona ni sawa..
Waacheni wazanzibar waamue mambo yao, mnajidai mnawapenda sana wa tanganyika walioko zenj kuliko walioko musoma? mbona waliua hao sikuona maandamano? hivi wako wangapi huko zanzibar? wazanzibar wangapi wako bara..serikali gani ya kijinga itafanya hivyo..kweli wewe ni mchochezi na una agenda yako shame..
Huko zanzibar kuna watanganyika, wakenya, burundi, oman, wa norway mara ya mwisho kwenda...wapo hakuna aliyewahi kuwaua wala kuwabagua na wazee wetu wamekuwa wakienda huko miaka nenda rudi wakitokea bara bila shida wala problem
Shida ni ukoloni wenu sasa mnatafute visingizio oh dini ...grow up bana! waacheni wanzibar wakitaka muungano ok! wasipotaka ok! mnang'ang'ania nini? au ndio hizo agenda zenu za kina msekwa, makamba, always wanaopenda muungano ubaki kwa udi na uvumba ni wale wanaotoka ... wameshakununua uzieneze hapa
Wazanzibar only this time you can make "REJESHENI HESHIMA YENU" taifa lenu tutaungana kwa heshima si kwa ukoloni.