Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Lowassa kashaibadilisha Chadema.

1. Kabadilisha ratiba yao ya uchaguzi.

2. Kabadilisha mgombea wao. Dr. Slaa anakatwa kwa sababu ya Lowassa.

3. Kabadilisha bajeti yao ya uchaguzi.

4. Kabadilisha kauli zao kuhusu ufisadi.

5. Kabadilisha ilani yao ya uchaguzi.

Sasa tujiulize, nani anayebadili mwenzie? Chadema itambadili Lowassa au Lowassa anaibadili Chadema?

Lowassa yuko kwenye siasa muda mrefu kuliko umri wa Chadema. Kuamini kuwa Lowassa atabadilika ghafla ni kujidanganya kulikopitiliza.

Mpaka sasa Chadema haijabadili chochote kwa Lowassa, yeye ndio anawabadili.

Chadema badala ya kuleta mabadiliko, yenyewe ndio inabadilishwa...
Huwezi kuamini huyu ndie Edward Lowassa mmiliki mpya wa
chadema unaambiwa hata Mzee Mtei aliyekuwa mwenye chama haongei.nguvu ya pesa inafanya kazi.
 
Lowassa kashaibadilisha Chadema.

1. Kabadilisha ratiba yao ya uchaguzi.

2. Kabadilisha mgombea wao. Dr. Slaa anakatwa kwa sababu ya Lowassa.

3. Kabadilisha bajeti yao ya uchaguzi.

4. Kabadilisha kauli zao kuhusu ufisadi.

5. Kabadilisha ilani yao ya uchaguzi.

Sasa tujiulize, nani anayebadili mwenzie? Chadema itambadili Lowassa au Lowassa anaibadili Chadema?

Lowassa yuko kwenye siasa muda mrefu kuliko umri wa Chadema. Kuamini kuwa Lowassa atabadilika ghafla ni kujidanganya kulikopitiliza.

Mpaka sasa Chadema haijabadili chochote kwa Lowassa, yeye ndio anawabadili.

Chadema badala ya kuleta mabadiliko, yenyewe ndio inabadilishwa...

aisee, nimeamini ukitaka kuona nyeti za kuku, subiri kaupepo upulize!! mambo yote hadharani -- CCM kwisha jeuri yenu!!
 
Yaani kama chelsea ilivonunuliwa yule mrusi.. Ndivyo lowassa alivofanya kainunua CDM ...
 
Mkuu ikandanganywa na ccm sawa ila ukindanganywa na chadema imekuwa nongwa!Mbona ccm ccm inakudanganya kila mwaka na kila uchaguzi hulalamiki?
Siasa ni mchezo wa wingi mwenye wengi ndo mshindi! Nchi hii bado watu wengi ni mbumbumbu ambao ni zaidi ya 60% hawa wako tayari kuchagua hata sura tu ukawa Rais wa nchi hii. kama tungekuwa wote tuna ufahamumtu ambaye anafaa ni Dr.Slaa, lakini kwa kuwa watanzania ni mbumbumbu, ukimweka kugombea mtashindwa wao wanataka LOWASA! wewe unasema ni fisadi wao ndo wanamtaka huyohuyo! Chadema wameamua nawao wazipate zile kura za mbumbumbu wa nchi hii ambazo ndo nyingi ili washinde mambo mengine mbele kwa mbele! kama na hapa utakuwa hujanielewa basi rudi darasani mkuu!

Hayo ya Lowassa fisadi au sio fisadi, hapa sio pake fungulia uzi mwingine. Mada iliyopo picha hizi ni za kugushi, kwamba Lowassa hakuwapo katika kikao hiki picha yake imebandikwa tu na wanjanja. Wewe unasemaje? Unachojaribu kuniambia Sababu CCM wamekuwa wakinidanganya basi Chadema au mwingine anapoiga mfumo wa udanganyifu nivumilie?
 
Kumbuka msemaji wa mwisho wa nani agombee ni wa kamati kuu. Hivyo matokeo ya kura za maoni yanaweza kubadilishwa kwa maslahi mapana ya chama na mustakabli wa taifa.
Kwahiyo kura zenu za maoni ni fix tu!
 
Mimi picha hiyo ya chini nilisema wazi ni edited lakini hiyo ya juu hakika ni halisi kabisa na ni wazi Chadema hawakutaka picha hii ivuje na Mbowe ana sema za kutengenezwa lakini kwa aliyo yasema mbele ya wahariri ni wazi picha hizo ni halisi kabisa sema imembidi azikane tuu!

Hata ziwe halisi au Edited ukweli unabaki palepale kuwa LOWASA AIKACHA CCM NA KUJIUNGA UKAWA(CHADEMA)
 
Jikumbushe

Lowassa Ngoyai Edward 2008.

"Mheshimiwa Spika, kwanza napenda. kuchukua
nafasi hii kukushukuru sana kwa kunifanya
msemaji wa kwanza katika hoja hii.
Lakini la pili, nimpongeze Dk. Harrison
Mkwakyembe, Mwenyekiti wa kamati Teule kwa
kuwasilisha kwa mbwembwe nyingi sana taarifa
yake, mbwembwe zilikuwa nzuri kweli.
Kwa kazi nzuri kwa maoni yao, wamewasilisha
vizuri. Lakini nimesimama kuweka kwenye
kumbukumbu kutoridhika kwangu na jinsi kazi
hiyo ilivyofanywa. Mheshimiwa Dk. Mwakyembe
ni Mwanasheria, tena Daktari alikuwa anafundisha
Chuo Kikuu. Moja ya vitu alivyokuwa anafundisha
ni "Natural Justice".

Mheshimiwa Spika, wewe ni Mwanasheria
unafahamu suala la Natural Justice. Kwamba
Kamati Teule imesikiliza watu wengine wote
pamoja na wanaoita minong'ono ya mitaani,
wamesafiri mpaka Marekani kutafuta mashahidi,
lakini mimi ambaye ni mmoja kati ya
watuhumiwa mle hawakunihoji hata siku moja.

Mheshimiwa Spika, nimesimama kueleza
masikitiko yangu. Ofisi ya Bunge mpaka ofisini
kwangu hata kama wangeniita ningekwenda kwa
miguu kama hamna gari na nilikuwa tayari
kufanya hivyo.
Hawa ni watu makini sana siwezi kuamini
kwamba wanaweza wakafanya oversite kama
hiyo. Kwa sababu katika kila hoja walizojenga
wamesema Waziri Mkuu ilikuwa hivi. Kulikuwa na
shida gani kuja kuniuliza Waziri Mkuu wanasema
uliotoa dokezo hili ni sawa sawa kweli? Kulikuwa
na shida gani kwa mfano kufuata utaratibu wa
Westminster kuthibitisha hapo unaposema
mwenye Richmond ni fulani uka-lay on the table
records na ushahidi kuwa ni fulani.

Mheshimiwa Spika, Taifa letu ni Taifa changa,
lakini chombo hiki ndiyo mahali pa demokrasia
pakubwa katika nchi pote, hapa ndipo penyewe.
Kama katika chombo hiki haki haitaonekana
kutendeka nchi yetu haitakwenda vizuri. Hapa
ndipo tunategemea tuwaonyeshe umakini wetu,
umahiri wetu katika mambo ya demokrasia. Kwa
nhiyo nilichofanyiwa napenda kuweka
kumbukumbu sawa kwamba naona si sahihi,
nimefadhaika sana, nimedhalilishwa sana,
nimeonewa sana katika hili.
Maana zimechukuliwa tuhuma zikaelezwa hapa
kwamba hivi ndivyo ilivyo. Mimi sijauliza.
Kulikuwa na shida gani kuniuliza, kwa nini
muamini minong'ono ya mitaani kuliko maelezo
yangu. Sisi wote hapa ni wanasiasa tukianza
kuamini minong'ono ya mitaani niambieni
mwanasiasa atakayesimama. Hatuwezi, Tume
imepewa muda wa kutosha lakini inashindwa
kumuona mtu ambaye wanamtuhumu na
wanamsema kwa kirefu sana.

Mheshimiwa Spika, lakini hata pale
uliponinong'oneza ukaniambia una ushahidi
wowote? Nilikupa ushahidi huo wa maandishi.
Katika taarifa yao hakuna hata moja ya ushahidi
ambao umetoka Waziri Mkuu. Kile kitabu cha
majedwali kimejaa majedwali mengi pamoja na
magazeti mpaka ya Udaku lakini maelezo ya
Waziri Mkuu hakuna hata moja.

Mheshimiwa Spika, naamini ingekuwa ni heshima
wangeiweka halafu wakasema tunakataa
kitambulisho hiki kwa sababu hii na hii, hiyo
ndiyo imejengwa hoja. Lakini kujenga hoja na
kuja hapa Bungeni tunahutubia nchi nzima na
kusema Waziri Mkuu amefanya hiki, amefanya
hiki bila ya kumsikiliza nachelea kuuliza hivi mtu
wa chini itakuwaje?

Mheshimiwa Spika, lakini nimetafakari kwa
makini sana jambo hili nikajiuliza hivi kulikoni
mpaka watu wazima wenye uwezo wao, watu
maarufu wenye heshima zao, mpaka wafike
mahali waache jambo la msingi kama hilo
kulikoni? Mimi nadhani there is a wish which I
am going to grant, ni Uwaziri Mkuu. Nadhani
tatizo ni Uwaziri Mkuu. Kwamba ionekane Waziri
Mkuu ndio amefanya haya, tumuondolee heshima
au tumwajibishe.

Mheshimiwa Spika, nimetafakari kwa niaba ya
chama changu, kwa niaba ya Serikali yangu
nimeamua kumwandikia Rais barua ya
kumwomba niachie ngazi. Nafanya hivyo kwa
moyo mweupe kabisa ili kuonyesha dhana ya
uwajibikaji lakini kutokubaliana na utaratibu
uliotumika kusema uongo ndani ya Bunge wa
kumsingizia mtu.

Mheshimiwa Spika, nitumie nafasi hii
kumshukuru sana Rais kwa heshima aliyonipa ya
kutumikia nchi hii kwa Uwaziri Mkuu kwa miaka
miwili. Namshukuru sana Mheshimiwa Rais.
Nakushukuru wewe, nawashukuru Mawaziri na
Manaibu Waziri, nawshukuru Waheshimiwa
Wabunge na wanachama wa CCM tuliyosimamia
Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi.
Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo
nashukuru".
 
Tuwaulize huyo wanayemkaribisha amewaambia ana malengo gani na Nchi Yetu?

unajua siasa za Tz sasa zinajidhirisha waz kuwa ni biashara tu-hapo UKAWA wamebadili butcher la ng'ombe kuwa KITIMOTO baada ya kuona soko la ng'ombe linasuasua lakin awali walituaminisha kuwa KITIMOTO ni haramu
 
Hata jambazi sugu la kupora watu kwa silaha ukikutana nalo ukaliuliza lina malengo gani kwenye familia yake litakwambia lina malengo kujenga nyumba nzuri ya familia na kusomesha watoto shule nzuri.

juzi Mtangazaji wa Mpira wakati akielezea sababu ya watamaji kuwa wachache uwanja wa Taifa ktk mashindano makubwa na ya msimu ya Kagame Cup, alisema WaTz tunapenda timu sio mpira-hali hiyo inajionesha kwny siasa pia
 
El apewa Othman Masoud kuwa mgombea mwenza.
Masoud ni mwanasheria mkuu wa Zanzibar aliefukuzwa kwa kukataa katiba ya chenge.
Ni kijana msomi na makini
Timu imetimia na mechi imenogaa
 
hiyo ndio hali ilivyo sasa kwny siasa za Tz.
mwalimu(isomeke Upinzani) ulitufundisha maovu na hatari ya ufisadi na sisi tukaelewa na kuamini vilivyo na tukashika silaha kupambana na mafisadi( isomeke fisi) na wakati sasa tumeshachoma moto kuwadhiti fisi-anatokeza fisi Mkuu aliyekuwa akitusumbua , mwalimu anasema huyu ni mwenzetu (isomeke mbuzi).

ndg zangu Watz, tunarudishwa kuanza vita nyuma kabisa wakati tayar mafisad walikuwa hoi-leo hii yale mafisi yote (Chenge, Karamagi, Rostam, Tibaijuka, etl) wanashangilia kuona sasa kizazi chao kinarejea upya.

hongereni UKAWA kwa miaka 20 mmetuaminisha imani ambayo kwa masilah yenu ya kifedha leo mmetugeuka
Sikuamini masikio na macho yangu jana kile akina Lipumba walichokuwa wanakisema,wananchi tumegeuzwa matahira kisa pesa na mafanikio yao binafsi na familia zao kwa kupitia mgongo wa walalahoi lakini Mungu ni mkubwa waovu watashindwa na uovu wao,tutashikizana adabu Octoba.Pia ni wakati wa Slaa kuwakimbia mafisi.
 
hiyo ndio hali ilivyo sasa kwny siasa za Tz.
mwalimu(isomeke Upinzani) ulitufundisha maovu na hatari ya ufisadi na sisi tukaelewa na kuamini vilivyo na tukashika silaha kupambana na mafisadi( isomeke fisi) na wakati sasa tumeshachoma moto kuwadhiti fisi-anatokeza fisi Mkuu aliyekuwa akitusumbua , mwalimu anasema huyu ni mwenzetu (isomeke mbuzi).

ndg zangu Watz, tunarudishwa kuanza vita nyuma kabisa wakati tayar mafisad walikuwa hoi-leo hii yale mafisi yote (Chenge, Karamagi, Rostam, Tibaijuka, etl) wanashangilia kuona sasa kizazi chao kinarejea upya.

hongereni UKAWA kwa miaka 20 mmetuaminisha imani ambayo kwa masilah yenu ya kifedha leo mmetugeuka
kWELI NI FULL AIBU....najiuliza kwa imani niliyonayo kwa DK Slaa na niliyokuwa nayo kwa Mwanasheria Tindu Lissu ...hakika navuta muda kulelekea uchaguzi huku nikipiga picha kampeni za Lowasa..kupitia ukawa...FID+SADI
 
Unabadilisha vipi mfumo wakati chama chako kimeshaanza kubadilishwa na mgeni?
Mgeni anakuja, sera za chama ziko pale, anatekeleza hizo. UKAWA si ushirika wa kitoto ati! Kwani Lowassa bado mnamhitaji? Kama ndivo atabaki tu, tusiwe na haraka.
 
Back
Top Bottom