Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

maana yake ni kwamba
1.upinzani unataka ushike dola kwa njia yoyote ile.na ni lazima kua lowasa amesha pewa taratibu na sheria za kuwa kama mpinzani
2.lowasa ameamua kumwaga ugali baada ya ccm kumwaga mboga.na hamna sehem anapo fit tena kwenye ccm.yaanihamna cheo chochote kinacho mfaa zaidi ya uraisi akiwa ccm,hata kama walimuahidi cheo chochote kile hamna kinacho mfaa.
3.cdm na ukawa kwa ujumla wanajua idadi ya wabunge wa ccm wanano muunga mkono el hivyo wana uhakika wa kupata viti vingi vya ubunge(takriban wabunge 80 wanasadikiwa kuhama na lowasa)kwa sababu inabidi walipe fadhila kwa el
4.upinzani wana mtaji wao wa wapiga kura na ukiongeza na mtaji wa wapiga kura mafuriko wa el basi ina maanisha kua upinzani chini ya el wataweza kuchukua nchi
5.kuna watu kama nchimbi etal,hao wana hasira na ccm na wapo tayari kuibomoa.
6.ukawa wamesha fanya mazungumzo na el ambyo ni win win situation kwa kila upande,kwa el na kwao.maana lazima wawe wamejiridhisha kua el hata jitoa kugombea uraisi pindi atakapo teuliwa na ukawa na baada ya kuidhinishwa na tz nec.maana kama akijitoa maana yake n8 kua ccm itapita bila kypingwa,maana itagombea na mgombea wa act pekee.
6.lowasa alikua ana gombewa na act na ukawa.ukawa ndio ikaibukabkidedea.hivyo kwa upinzani kummiliki el ni fursa ya kupatia kura kwa wananchi.ni mjinga peke yake ndio ataiacha fursa kama hii ipotee.

cha msingi ni chadema wawe wana mminitor el kula sekynde maana ccm walijaribu kum monitor el kila sekunde ili asifanye anything stupid aka waponyoka.

mkutano wa jana wa ukawa wa buguruni na waandishi wa habari ni makybaluano kua ukawa wamuombe lowasa aje ajiunge nao na wamsafishe kwanza hadharani.maana el huwa anapenda kuonyesha kua ameombwa na watu ajiunge nao. na pia ni mbinu ya kuonyesha kua sio mpenda madaraka kama watu wanavyo dhani ispokua watu ndio ndio wanataka awaongoze
 
Hakika Lowassa ana kazi rahisi sana kushinda urais.Anachotakiwa kufanya ni kuwatupia CCM zingo lao la Richmond.Maana doa lake ni hilo tu.Hapa sasa aseme ukweli maana hana wa kumpepesia macho na asimlinde mtu yeyote.

Kwa mujibu wa nafasi yake lazima hilo zigo alitupe kwa yule aliye kuwa anawajibika kwake.Je aliingilia mchakato,je alipopewa taarifa kuhusu richmond hakuwajibika?.

Ni kazi rahisi sana Lowassa kujisafisha kisha atabaki katika ubora wake.........

Lowassa wewe ni mtaalamu wa art sasa tumia taaluma yako sawa sawa.

 
Raia wa kawaida huku mtaani wanafurahia sana lowasa kua mwana chadema ni lazima tuelewe lowasa kwa sasa sio mwana ccm tena kila atakachokifanya itakua kuhusu chadema na si ccm atafanya kila kitu kwa muongozo wa chadema hili naamini amelikubali hadi kujiunga chadema naamini ametoka na ameiaga ccm na chuki juu yake ndani ya chama cha ccm kitamfanya kua mwana chadema imara kama mbowe na slaa na bahati nzuri pesa anayo nawapongeza slaa na mbowe kwa kukomaa kisiasa kwa kuonyesha si wapenda madaraka tutakua pamoja mpaka chadema itakapoingia ikulu +ukawa hongera CUF NCCR na NLD kua kitu kimoja na chadema kwa sasa ni mwanachadema na yeyote atakayemtuhumu ni fisadi basi atuambie ni kwa nini hukumpeleka mahakamani
 
Wanamtandao sasa wapo Chadema. SIASA ni Maigizo
Ni zaidi ya pwagu na pwaguzi. Lakini nafikiri inakuwa maagizo hasa inapoingiliwa na wigizaji. Focus kubwa ya mbowe ni kupata viti vingi vya ubunge na hatimaye ruzuku kubwa, ni biashara. Lakini ni kujitia upofu kufikiria kwamba watashinda.
 
Mafuriko ukiyazuia yanatafuta njia nyingine ninyi tulieni muone mwelekeo wa hayo Mafuriko
 
Una kachembe ka utaalamu wa picha?kubali usikubali hizo ni za kutengeneza.hako ni kautalamu ka kawaida.au nikusetie yako ukicharazwa bakora na mh mbowe kwa kumkashifu?
 
Mtatukana matusi yote, lakini haitasaidia, kila mtanzania yuko Huru kwenda chama chochote cha siasa anachokipenda!

Lowassa ni Chaguo la Mungu!
 
Ni vigumu kupendwa na mtu mpumbavu

Na wasema maisha ni safari ndefu ishi upendandavyo

Na furaha ya maisha sio lazima upendwe na kila mtu
 
mlimkata sasa mbona mnalalamika baaada ya kujiondokea na kuwaachia chama chenu?

Sahihisha,siyo kila mwenye mawazo tofauti na wewe ni CCM,kuna wanaCDM wenzako pia tunamawazo tofauti na viongozi wetu.

Simkatalii Lowassa kuwa Mwanachama wa CDM ila nakataa Lowassa kupeperusha Bendera ya CDM kwenye ngazi ya URAIS.

Ninasababu kubwa moja ua mbili,kwanza huyu Mtu amepoteza pesa nyingi sana wakati anataka kuteuliwa kuwa mgombea wa CCM,leo tujiulize mimi na wewe atazirudishaje?Je hii haitakuwa mwanzo wa kuingia unajisi CDM ?Unadhani aliyezoea kula nyama ya mtu ukimbadilisha dini ataacha?

Pili huyu njia aliyotumia kusaka URAIS ndiyo njia aliyotumia kumasaidia RAFIKIYE mpendwa kuingia magogoni,tumeona jinsi maliasili zetu zilivyokuwa zinachotwa bila hata kukemewa na kiumbe yeyote.Rais alishika UTAMU wote hakuna mbunge wala nani kumkemea,jamani mnataka turudi miaka mingine kumi ya aina ile ile?

Tatu na mwisho inamaana miaka yote hii ishirini CDM imeshindwa kumrecruit KIONGOZI BORA wa kupeperusha Bendera ya CDM?

Je,viongozi wanawatendea HAKI watanzania waliojiaminisha kwao?

Hakika sina shida na Mbunge wangu JJMnyika Kura yake ipo wazi hana haja ya kuifuata kama alivyosema Mpoto nitampelekea mwenyewe lakini URAIS kama ni LOWASSA HAPANA na wala MAGUFULI pia hapati kura yangu wote hawa ni walewale tu.

Hizo ndizo sababu zangu mimi siyo CCM pole,ila ninamawazo tofauti na wewe.
 
CCM waliyataka wenyewe mi simo vijana Nape na Makonda wanamdharau Lowasa dawa yao Watz tuwatie adabu.Goli la Mkono Watz tuamke tuamke!
 
Back
Top Bottom