Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Kumkataa Lowassa ni uchanga wa kisiasa, dola inachuliwa kwa style yoyote ile inayowezekana. CCM wanaua ili kulinda madaraka nyie kumchukua mtu kutoka CCM atakayewaumiza mnaona ni njia haramu ya kupata madaraka, Nawaombeni tukasome Theory za Machiavelli kuhusu Politics (Power) itatupanua uelewa kidogo wale tunaopinga political move ya Chadema kuhusu Lowasa. Halafu political immaturity tusiitoe nje ya group tutakuwa tuna expose our extreme ignorance on politics! Yani kuna watu wanaona ni bora CCM iendelee kutawala kuliko Chadema kushinda dola kwa kumtumia Lowasa. Hawa watu wanawapenda watanzania kweli? Hivi tunavyokuwa tunasema tunataka kuing'oa ccm madarakani tulikuwa tunajua kweli what it takes kukiondoa chama tawala madarakani, tunadhani ni kazi nyepesi? tuiamini kamati kuu ya chadema kama ambavyo tuliiamini kuhusu kumuondoa Zitto Chadema, they know what they are doing, and I even know more of what they are doing. Nitatetea huu msimamo kwa nguvu zote. They have made the right move at the right time, only time will tell you how right we are with this move. Siasa ni science na sanaa at the same time.
 
Sidhani kama Lowassa ni mjinga kihivyo.Hivi unajua watu wengi wako implicated kwenye hiyo kesi?Kuna Waziri na Naibu wake,Katibu,mwanasheria mkuu wa serikali ambaye ni Chenge.duh! Sinema hii nzuri inabidi uongeze😛opcorn

acha hivyo ...Kuna Rais Pia....ndiye aliyesaini document zote za mwisho..Kikwete ndiye aliyemleta Gire...mmiliki wa kampuni ya Mfukoni Richmond.....kaka usidhani watu wanakurupuka
 
Mh EDWARD NGOYAI LOWASSA NI MSAFI.

Watu wengi wataishangaa kauli yangu, watakaa midomo wazi na kujiuliza maswali kibao moja ya maswali watakayojiuliza ni kama yafuatayo.

Anasema EL ni msafi wakati alithubutu kumuita Fisadi?

Usafi wake uko wapi au kwa kuwa kahamia Chadema?

Huyu anayesema haya ni mamluki au Chadema kweli?

Hayo ni baadhi tu ya maswali japo najua kuna maswali mengine mengi zaidi juu ya mh EL.

Wanapoendelea kujiuliza ni vyema na mm niwaulize maswali kadhaa kama ifuatavyo?

Kama EL ni mwizi au fisadi ni kwanini hadi leo hajakamatwa na kupelekwa Mahakamani?

Je hajakamatwa kwakuwa serikali ni dhaifu au haijui sheria inazosimamia yenyewe au iliogopa kuumbuliwa zaidi?

Toka 2008 hadi leo nini kimefanyika baada ya EL kwa kulinda heshima yake na kuamua kujiweka pembeni?

Tunadhani ni kwanini jina lake liliishia njiani? papo hapo jiulize kwanini Rizone alitweete akionesha hayupo tayari kuona Rais akitokea kaskazini kipindi cha Uhai wake?

Je ni kwanini Rais JK hajawahi kuthubutu kumsema EL hadharani?

Je ni kwanini Upinzani walimpiga sana mitandaoni na hata majukwaani lakini leo wapo meza moja?

Ni kwanini CCM walimuamini tena 2010 akapeperusha Bendera yao jimbo la Monduli? utamuaminije Mwizi?

Je ni nchi gani upinzani ilishawahi kuing'oa serikali bila kutumia watu waliokuwepo au waliopo Madarakani?

Je tunapenda kuendelea kuwa masikin kwa mfumo uliopo?

Bado nina maswali ambayo sitayamaliza sasa hivi ila endelea na ww kujihoji na kujipa majibu huku ukiangazia mfumo mzima wa chama cha mapinduzi na serikali yake ndipo utapata majibu.

Narudia kusema "EL si Mchafu hata kidogo" lakini katika yote Mfumo wa CCM ndio mchafu na ndio unaowafanya wachafuke hata wasio wachafu, yawezekana kabisa msielewe dhana yangu lakini pia mkanielewa dhana yangu.

Mimi kama mwanachama wa chadema sipo tayari kuendelea kuitwa mpinzani lakini nipo tayari kuona nchi hii ikiwa upinzani kwa masilahi mapana ya watz wote.

Nitaeleza kwa kina nikitulia sehemu yenye upepo mwanana

Jiunge na Team ya Ushindi
 
mh edward ngoyai lowassa ni msafi.

Watu wengi wataishangaa kauli yangu, watakaa midomo wazi na kujiuliza maswali kibao moja ya maswali watakayojiuliza ni kama yafuatayo.

Anasema el ni msafi wakati alithubutu kumuita fisadi?

Usafi wake uko wapi au kwa kuwa kahamia chadema?

Huyu anayesema haya ni mamluki au chadema kweli?

Hayo ni baadhi tu ya maswali japo najua kuna maswali mengine mengi zaidi juu ya mh el.

Wanapoendelea kujiuliza ni vyema na mm niwaulize maswali kadhaa kama ifuatavyo?

Kama el ni mwizi au fisadi ni kwanini hadi leo hajakamatwa na kupelekwa mahakamani?

Je hajakamatwa kwakuwa serikali ni dhaifu au haijui sheria inazosimamia yenyewe au iliogopa kuumbuliwa zaidi?

Toka 2008 hadi leo nini kimefanyika baada ya el kwa kulinda heshima yake na kuamua kujiweka pembeni?

Tunadhani ni kwanini jina lake liliishia njiani? Papo hapo jiulize kwanini rizone alitweete akionesha hayupo tayari kuona rais akitokea kaskazini kipindi cha uhai wake?

Je ni kwanini rais jk hajawahi kuthubutu kumsema el hadharani?

Je ni kwanini upinzani walimpiga sana mitandaoni na hata majukwaani lakini leo wapo meza moja?

Ni kwanini ccm walimuamini tena 2010 akapeperusha bendera yao jimbo la monduli? Utamuaminije mwizi?

Je ni nchi gani upinzani ilishawahi kuing'oa serikali bila kutumia watu waliokuwepo au waliopo madarakani?

Je tunapenda kuendelea kuwa masikin kwa mfumo uliopo?

Bado nina maswali ambayo sitayamaliza sasa hivi ila endelea na ww kujihoji na kujipa majibu huku ukiangazia mfumo mzima wa chama cha mapinduzi na serikali yake ndipo utapata majibu.

Narudia kusema "el si mchafu hata kidogo" lakini katika yote mfumo wa ccm ndio mchafu na ndio unaowafanya wachafuke hata wasio wachafu, yawezekana kabisa msielewe dhana yangu lakini pia mkanielewa dhana yangu.

Mimi kama mwanachama wa chadema sipo tayari kuendelea kuitwa mpinzani lakini nipo tayari kuona nchi hii ikiwa upinzani kwa masilahi mapana ya watz wote.

Nitaeleza kwa kina nikitulia sehemu yenye upepo mwanana

jiunge na team ya ushindi


usafi huo wa lowassa umejulikana lini
 
kuna watu politics imewapitia pembeni chama chochote cha siasa kinaundwa ili kishike dola kwa gharama yeyote ile ni kama chama tawala kinavyolinda utawala wake kwa gharama yeyote ..chadema kitashirikiana hata na shetani kuitoa ccm madarakani ili heshima iwepo nchi hii mambo mengine yatafuata baadae kama kweli wewe ni mpenda mageuzi huwez kataa ujio wa lowasa chadema labda ulitataka chadema wawe wapinzani foreva....kama hukubaliani unaruhusiwa kuhama chama tuacheni ambao tuna malengo ya kukamata dola na sio kua wapinzani foreva ...
 
Mbowe kakataa kabisa kuongea kwenye Mkutano na hata Waandishi waliomfata kuongea nao kakataa. Anapima Upepo
 
Ina maana Dr Slaa Ukikurupuka kumuita lowassa fisadi na kumjumuisha kwenye LIST OF SHAME.

Ulituaminisha wananchi kuwa lowassa ni fisadi na ile list of shame ni utapeli wa kisiasa.

Ulituambia kuwa usalama wa Taifa wanaripoti kwako iweje wasijue kuwa EL alikuwa msafi?

Ushauri wangu kwako ni mmoja tu jiuzulu kama uliudanganya umma wa watanzania.

Muombe msamaha EL kwa kumchafua kitu ambacho kilipelekea yeye kukatwa ndani ya ccm pamoja na ushawishi aliokuanao.
 
acha hivyo ...Kuna Rais Pia....ndiye aliyesaini document zote za mwisho..Kikwete ndiye aliyemleta Gire...mmiliki wa kampuni ya Mfukoni Richmond.....kaka usidhani watu wanakurupuka

Ah rafiki mie mdada bwana.Pole.Ninajua JK ndiyo mwenye deal ndiyo nimesema Edo siyo mjinga kihivyo.Kesi ya urais itaibua mengi.Si wengine wapiga kura tu....
 
Kanyaga twende Kamanda Lowassa anatosha. Ukitaka kuona nyeti za kuku subiri apulizwe na upepo. Kumekucha
 
Tuliza boli!!! Kumbuka hata Marekani ilimtumia Osama Bin Laden kuisambaratisha Urusi. Iwapo Lowassa ana uwezo wa kuisambaratisha CCM ni lazima CDM wamtumie! Lengo ni kuing'oa CCM madarakani! Siasa ni strategy na hii ni fursa nzuri ya CCM kufa hata kama ni kwa mbinu chafu! Mengine baadae!!
 
Lizaboni hapana, hizi picha ni za keli. Na je jumbe alizotuma Lowassa Kwa wanamtando uwa yupo UKAWA nazo ni za kutengeneza?

acha kudanganywa picha za kutengenezwa zoote, tena zchunguzen vzur background zlivyokaa na maumbile yao utagundua kuwa zmeungwaungwa tu kisanii, na hii waliyosimama, wamekata picha ya EL wakaiweka kwenye picha hiyo y viongoz wa cdm, angalia hata hawakuwa wanatazamana kila mtu alikuwa na time yake'
 
Last edited by a moderator:
Wewe mwanaharamu namuomba Mungu akulaani kwa kuhadaa maelfu kwa maelfu ya Watanzania na photoshops zako. Je umenufaika na kipi kwa hadaa hii? Dear admins, acheni kulala. Mpo bize kuhamisha mada za muhimu lakini mnashindwa kuchukua hatua dhidi ya uhuni huu. JF mna fedha ya kumlipa Lowassa au UKAWA mkichukuliwa hatua za kisheria kwa hiyo photoshopping?

dugu yangu umekuja juu kama moto wa kifuu.Haya twambia kosa la nani?Tumewabembeleza tutajieni Mgombea urais kimya,jamani tuambieni ni Lowassa kimya.Leo mbatia katangaza wanamkaribisha Lowassa na watampa nafasi hamkufafanua nafasi ipi.

Waacheni waweke uhuru wa habari.Mngetaka mngemtangaza mgombea mapema,lakini inaelekea huko hakuna mgombea ambaye yupo safi zaidi ya huyu makapi toka CCM....

Pole kwa hili wengine tumeshafanya uamuzi mgumu...No for Lowassa yes for JJMnyika.Bye bye....

Mkitufukuza twambieni wapi turudishe kadi zenu....
 
hana jipya. hao hao chadema kupitia katibu mkuu walimwita lowasa fisadi hakafu hao hao leo wanampokea. lowassa bora atulie tu akihamia chadema kaisha
ccm walimwita Lowasa Fisadi na kumtaka ajivua gamba sasa wanahaha nini ???
 
Back
Top Bottom