Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Hiyo Richmond ina siri kubwa sana siku ukiijua hutaweza kuamini. Ushawahi jiuliza kwanini USA walinunua Dowans?

Swali ni kwamba ni nani anamiliki Mahakama, Serikali na vyombo vyote vya usalama? hayo Unayoyasema wewe ni mpaka upate/upewe nafasi ya kuyasema!
Serikali pmj na vyombo vyake wakishaamua kukufungulia mashtaka hakuna atakaye kusikiliza tena, hakuna gazeti litakalo kutetea, hakuna TV itakayokupa air time kwa maana wote hawa pia wamesajiliwa na serikali!
Unafikiri akina Mramba na Yona hawana ya moyoni? Lkn ni nani anawapa nafasi hata ya kuyasema?

Kama haumini ninayokwambia subiri uone sasa mziki wa Serikali dhidi ya Lowasa na CHADEMA kwanza akitangaza tu walinzi wote aliopewa kama Waziri Mkuu mstaafu wanarudi Serikalini pili mpaka sasa hivi anajulikana kama Waziri Mkuu mstaafu hilo litabadilika na mambo yataanzia hapo...
 
naanza kupata wasiwasi na hizo picha
mbona mood za watu ziko tofauti:what:

mbona slaa kavaa mashati mawili tofauti kwenye hzo picha mbili?:what:

jaribu kuzoom mkono wa kulia wa lowassa

 nitarudi

Nimeangalia tena nimeona kuna utofauti wa nguo hasa....................
 
Hii picha imepigwa kutumia spy camera za miwani au jino bandia. Inawezekana imepigwa na mmoja wa wapambe wa EL au Mlinzi wake ndo maana hapo haonekani.
 
CCM wanakwenda kupinduana wenyewe kwa wenyewe si ajabu unabii wa Nyerere aliyesema kuwa mpinzani wa kweli atatoka CCM ndio unakwenda kutumia.
 
Nasikia mbowe alimwambia lowasa atoe B10 apewe nafasi ya kugombea urais kupitia chadema!!!!!
 
CCM wanakwenda kupinduana wenyewe kwa wenyewe si ajabu unabii wa Nyerere aliyesema kuwa mpinzani wa kweli atatoka CCM ndio unakwenda kutumia.
 
Wadau amani iwe kwenu.

Kikao cha Kamati Kuu cha dharura cha Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilifanyika jana Kunduchi Beach Hotel kuanzia saa mbili hadi saa tisa usiku. Jumla ya wajumbe 36 walihudhuria kikao hicho akiwemo Mwenyekiti Freeman Mbowe, Katibu Mkuu, Dr Wilbroad Slaa nk. Aidha, Edward Lowasa alihudhuria kama mwalikwa ambapo aligharamia mkutano huo ikiwa ni pamoja na gharama za ukumbi, chakula, nauli na posho za wajumbe. Kiasi cha fedha alichotoa Lowasa ni milioni 500 ambazo zimetumika kwa matumizi niliyoyataja hapo juu.

Katika kikao hicho, mjadala mkubwa ulitawala juu ya ujio wa Edward Lowasa ndani ya CHADEMA na hatimaye kupeperusha bendera ya chama hicho. Kutokana na tishio alilotoa Mwasisi wa CHADEMA, Edwin Mtei juu ya kuwafukuza Slaa na Lissu ikiwa hawatakubali Lowasa awe mgombea Urais, wajumbe hao waliamua kuridhia kwa shingo upande maamuzi ya wenye CHAMA. Kutokana na hali hiyo, Wajumbe wote 36 kwa kauli moja waliridhia Lowasa kujiunga na CHADEMA na awe Mgombea Urais.

Taarifa hii inahitimisha minong'ono iliyotanda siku nyingi tangu Lowasa akatwe. Kutokana na maamuzi hayo, uongozi wa CHADEMA umepanga kumtambulisha rasmi Lowasa kesho Jumanne Julai 28 kwenye Hotel ya Kilimanjaro Kempisk iliyopo Dar es Salaam.

Hata hivyo, ni lazima tujiulize kwa nini Lowasa anautaka sana urais kwa udi na uvumba? Je ni kweli ana uchungu wa kutatua kero zinazowakabili wananchi? Kama ndo hivyo, kwa nini akiwa Waziri Mkuu hakutumia nafasi hiyo na badala yake alitumia kufanya ufisadi hali iliyopelekea kujiuzulu kwake kutokana na kashfa za Richmond?

Ni vema tukatambua Watanzania kuwa Lowasa huyu huyu aliyekataliwa na Mwalimu Nyerere ndiye anayejiunga na CHADEMA. Ni Lowasa huyu huyu aliyekataliwa na CCM ndiye anayejiunga CHADEMA. Ni Lowasa huyu huyu aliyesimama kwa tambo nyingi akisema kuwa atakuwa wa mwisho kuondoka CCM na watakaomkataa waondoke wao ndiye anayejiunga na CHADEMA.

Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyataja mara kwa mara na kusisitiza kuwa ndiyo sifa za Edward Ngoyai Lowasa kutofaa kuwa kiongozi wa watu mambo yafuatayo;

  1. Ni mtu mpenda mali na kujilimbikiza mali kwa kiasi chochote na kwa hali yoyote anayoiweza. Lowasa anamiliki mali ambazo hazina maelezo ya jinsi alivyozipata. CCM waliliona hilo na wakamfungashia virago.
  2. Lowasa ni mtu dhaifu mbele ya mali na fedha kwa sababu hiyo njia na nafasi yoyote iliyo mbele yake anaweza kuitumia kupata fedha zaidi na kujilimbukiza mali.
  3. Ni mtu mwenye 'Pride' na kujitazama yeye tu na kupenda kutambulika kwa mali aliyonayo. Kwa sababu hiyo, anatumia muda na njia nyingi kujijazia mali badala ya kuongoza na kujali nchi yake (hii ndiyo sababu amekutwa na kashfa lukuki za ufisadi na kubwa zaidi ni ile ya Richmond iliyomfanya akaachia ngazi nafasi ya Waziri Mkuu).
  4. Lowasa anashindania zaidi kupata mali kwa njia zozote, ziwe za halali ama haramu. Kutokana na sababu hii ndio maana anajenga chuki na kulipiza visasi kwa watu anaoona kuwa vikwazo kwake katika kupata mali. Rejea jinsi alivyotuhumiwa kushiriki kumtesa Harrison Mwakyembe.
  5. Lowasa huwajali zaidi matajiri kuliko watu wa kipato cha chini. Hii ni kutokana na kulipa fadhila kwa watu wanaomsaidia katika harakati zake. Mathalan, wakati anatangaza safari ya matumaini, Lowasa alikuwa analazimisha wafanyabiashara kuchangia harakati zake kwa ahadi ya kufanya biashara na serikali akiwa Rais.

Kutokana na hoja hizi na nyingine nyingi bila kusahau ugonjwa unaoendelea kumsulubu, Lowasa hana sifa za hata kuteuliwa kugombea Udiwani. CHADEMA wamehadaika na tamaa ya fedha na wafuasi wa Lowasa. Bilioni 10 alizohongwa Mbowe zimefanya chama kitoke kwenye misingi yake na kuamua kumpokea fisadi.

Nawahurumia sana Dr Slaa, Godbless Lema, Tundu Lissu na wengineo ambao walijimaliza kutaja madhaifu ya Lowasa akiwa CCM. Je watafanya hivyo akiwa kwenye chama chao? Tusubiri tuone.

Ila jambo moja tu napenda kuwahakikishia wasomaji. Lowasa hana nafasi ya kushinda Urais. Nasema haya kwa kujiamini. Watanzania wamechoshwa na ufisadi. Watanzania wamechoshwa na viongozi wasiojali maslahi yao kama alivyo Lowasa. Watanzania si wepesi wa kusahau. Wameumizwa sana na hawa mafisadi na mwaka 2015 ni wa kukata mizizi yote ya ufisadi.
 
jaman haya mafuriko ya lowasa yanayokuja ni balaa hakuna cha tingatinga wala buldoza yanasomba kila kitu
 
11752506_957115111019150_7526639520180648076_n.jpg
 
Mkuu Lizaboni Chadema wamejizika rasmi...CCM njia nyeupe..
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom