Ikiwa ni kweli Lowasa akajiunga na CHADEMA kisha kuwa mgombea kupitia UKAWA, kuna maswali najiuliza.
1. Je, nini utakuwa msimamo wa Lowasa na kundi lake, dhidi ya yale ambayo UKAWA uliyapinga, na yeye ndani ya CCM waliyapitisha, hususan katiba pendekezwa? Je, katiba pendekezwa itaendelea na maoni ya Warioba au na yale ya CCM na timu ya Chenge?
2. Je, itakuwaje watu kama Chenge, "mzee wa vijisenti, joka la makengeza" akitaka kujiunga na CHADEMA au chama chochote ndani ya UKAWA, ilhali katika tuhuma karibu zote za rushwa na ufisadi alitajwa?
3. Je Lowasa atakuwa tayari kutekeleza yale yaliyopiganiwa na CHADEMA, au atatekeleza ndoto zake ambazo alikuwa nazo hata angepata urais kupitia CCM.
Mi naona kama vile mwisho wa UKAWA, hasa CHADEMA unakaribia, na mwanzo wa Lowasa na genge lake kupenyeza na kuinuka.
Mi naona kama kitazaliwa chama kingine ndani ya UKAWA hata kama hakitakuwa rasmi, yaani cha Lowasa na wapambe wake, ambacho ndicho kitakuwa na nguvu ya maamuzi, vingine vitabaki dhaifu, vikitazama tu, na labda vikilalamika tu.
Sitegemei Lowasa akiwa rais, azuiwe na mtu yoyote akitaka kumteua Chenge kuwa waziri wa sheria na katiba, na sitegemei Lowasa na genge lake linalohama kutoka CCM wakubali katiba ya warioba irudi.
Binafsi siombei hilo, lakini zaidi naombea kama kweli Lowasa atahamia, awe tayari kutekeleza kwanza kile kilichopiganiwa na UKAWA, ili kutupatia imani na matumaini sisi wananchi.