Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Kikao cha Kamati Kuu CHADEMA, Edward Lowassa ndani

Uhaini, Uhaini, Uhaini. Kwa zaidi ya miaka 7 Dr Slaa na wenzake wametuaminisha kuwa Lowassa ni fisadi na kwamba CHADEMA kinakataa usifadi, leo hii wanatumbia nini? What do CHADEMA stand for? Walioto wapi hadithi za Lowassa na ufisadi?

Mkuu NI kwa kuwa kwa miaka yote saba Ccm wameshindwa kumshitaki ili awe proved guilty.

So chadema tumejua kuwa kwenye Richmond yupo bado ccm
 
Lowassa: "Siwezi kuhama CCM, ambaye anaona hafai ahame yeye"

Mbowe: "Lowassa ni fisadi na yuko katika list of shame".

Slaa: "Hatupokei makapi ya CCM"

Leo hii they all have same mindset!?


Hahaha...Tanzania nchi yangu nakupenda sana, ila ukombozi wako bado sana!
Usijisahaulishe ... Alishawahi pia kusema asipopata ndani ya CCM atapata Nje ya CCM
 
BAVICHA karibuni uwanjani. Naona mambo yameiva.
Leo Lowassa sio ‘’fisadi‘’tena!
 
japo nilisikia hizi tetesi kwa muda mrefu ila nimepata mshtuko kuona hizi picha.

Sikujua tuna wanasiasa muflisi namna hii, kumbe Tanzania hakuna upinzani bali wasaka tonge.

Hakika <b>A WEEK IS VERY LONG IN POLITICS <b/>
Even a day is very long bro. Unakumbuka safari ya matumaini ilifutwa ndani ya masaa kadhaa.
 
Kama picha zinavyojieleza ni EL na wajumbe wengine katika mkutano
Siyo mkutano wa UKAWA acha kupotosha ni mkutano wa Chadema. CUF, NCCR MAgeuzi, NLD wapo wapi?

Teh teh teh teh.
 
Hizi habari za EL kwenda UKAWA zinavyosubiriwa kama ilivyokuwa inasubiriwa issue ya kukatwa, embu kina TOMASO tusubiri video kabisa vinginevyo tuwe mashuhuda tu
 
Baada ya kuwa kimya muda mrefu ''THE WHITE'' amesema wabunge zaidi ya 150,wakuu wa wilaya ,wa mikoa na viongozi mbalimbali wa serikali nao watanifuata,ndani ya siku mbili kuanzia leo.

''source:niko kwenye kikao''

Kikao kinafanyika wapi mkuu!
 
Mwalimu Kambarage Nyerere alisema atakayeiua ccm atatoka ccm,
sasa kumekucha kama ule wimbo wa marehemu komba
tuombe uzima oktoba 2015 itukute hai.

Aliyekiokoa chama na umauti mwaka 1995
sasa ni marehemu,nani atakiponya chama 2015?
je ni wale aliowazuia wasiuzwe benki wakauza?
je ni wale aliowasihi wasivunje azimio la Arusha wakavunja?
ni nani?
 
Picha mbilii tu hapana hebu kaongezeee mpaka ya kusalimia wajumbe
 
Adui wa Watanzania ni CCM wala si Mtu Mmoja Mmoja. Mbona Mijizi Mingi Ipo CCM au wewe Unamwona Lowassa tu Kwa Kuwa Amewabwaga Minyinyiem.
 
Lowassa: "Siwezi kuhama CCM, ambaye anaona hafai ahame yeye"

Mbowe: "Lowassa ni fisadi na yuko katika list of shame".

Slaa: "Hatupokei makapi ya CCM"

Leo hii they all have same mindset!?


Hahaha...Tanzania nchi yangu nakupenda sana, ila ukombozi wako bado sana!
Mkuu binadamu wote wako hivyo, usitegemee kupata binadamu atakayemaanisha anachokisema kwa 100%.
So Lowassa kuja ukawa na kubadilishwa status sitashangaa....na inawezekana walimsema fisadi kupata uungwaji mkono na watamsafisha kwa lengo lile lile la kuungwa mkono.
Binafsi nina imani na Lowassa, hakuna aliye msafi hapa duniani...huyu tajiri atatuibia huku anapuliza, huyu aliyetoka aliingia masikini ulizia hazina kama ina kitu.
 
For real sielewi hatma yangu chadema yaani naiangalia kadi yangu katiba yangu na bendera yangu ya chadema nafikilia mara mbili nivichome moto au!? Wakuu Lowassa simuamini kweli ndio uongozi umemtaka aje chadema!? Ngoja tuone!
 
Back
Top Bottom