Kijiji kilichomrushia mawe JK: "Zitto tuhutubie ama sivyo mawe"..

Nurujamii

JF-Expert Member
Jun 14, 2007
414
15
Na Maregesi Paul, Chunya

BAADHI ya wakazi wa Kijiji cha Kanga, wilayani Chunya, Mkoa wa Mbeya, ambacho baadhi ya wakazi wake walipiga kwa mawe baadhi ya magari yaliyokuwa katika msafara wa Rais Jakaya Kikwete hivi karibuni, wametishia kumshambulia kwa mawe Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Kabwe Zitto.

Wanakijiji hao walidai kuwa tayari kumshambuliwa kwa mawe Kabwe ambaye ni mbunge wa Kigoma Kaskazini kama asingewahutubia kwa mujibu wa ratiba iliyopangwa.

Walitoa onyo hilo juzi kijijini hapo, muda mfupi baada ya Kabwe kuwataarifu kuwa asingehutubia mkutano wa hadhara katika muda uliopangwa kwa kuwa alikuwa akisubiriwa katika Kijiji cha Mkwajuni, wilayani humo.

Pamoja na kuwaambia kuwa angerudi tena katika kijiji hicho kwa ajili ya kuwahutubia, wananchi hao walionyesha kutoridhishwa na ahadi hiyo na kumtahadharisha kuwa asije akawalaumu iwapo kama asingewahutubia baada ya kutoka Mkwajuni kwa vile wanahitaji kusikia sera za chama chake.

"Sisi tunakusubiri kama unavyotuahidi, lakini kama utajifanya mjanja, basi usije ukatulaumu kwani tutaishambulia gari yako kwa mawe," walisikika baadhi ya wakazi hao wakisema.

Ili kuwatoa hofu, Zitto aliwasisitizia kwamba asingeondoka wilayani humo bila kuwatuhutubia kwa vile lengo la chama chake ni kuzungumza na Watanzania wote ili wajue namna ya kuiondoa madarakani CCM.

"Jamani naomba msinipige mawe kwa sababu nitakaporudi kutoka Mkwajuni, lazima nitawahutubia kwani nisipofanya hivyo nitakuwa siwatendei haki kwani hata nyinyi ni wapiga kura," alisema Zitto.

Akihutubia kijijini hapo baada ya kurejea kutoka Kijiji cha Mkwajuni, Zitto alikemea vitendo vyovyote viovu vinavyofanywa na wananchi dhidi ya viongozi wa kitaifa.

Alisema kwamba, kitendo cha baadhi ya wakazi wa kijiji hicho kuupiga mawe msafara wa Rais Kikwete, kinafaa kukemewa kwa nguvu zote kwa vile historia ya Watanzania inaeleza jinsi wanavyopenda amani tofauti na nchi zingine duniani.

"Nilisikitika sana niliposikia kwamba, msafara wa Rais Kikwete ulipigwa mawe na baadhi yenu kwa sababu hiyo siyo historia ya taifa letu ambalo limekuwa mfano wa kuigwa duniani.

"Hata kama kiongozi amewachosha, njia sahihi siyo kumpiga mawe bali ni kutompigia kura wakati wa uchaguzi kwa sababu yeye anapatikana kwa kura," alisema Zitto.

Katika hatua nyingine, alimtaka Rais Kikwete kuwawajibisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile, Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Fatuma Kimario, Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Kanga na Ofisa Mtendaji wa Kata ya Kanga kwa madai kuwa wameshindwa kutatua kero zilizosababisha wananchi hao kushambulia msafara wa Rais.

Alisema kwamba, watumishi hao wanastahili kuchukuliwa hatua kwa vile chanzo cha wananchi kuurushia mawe msafara wa Rais kilikuwa kinajulikana ingawa viongozi hao kwa nyakati tofauti walishindwa kuwasikiliza wananchi hao.
 
Last edited by a moderator:
Duh!!!!...yaani kuhutubia watu ni lazima?Kweli hii siasa
inakoelekea kutakua na culture ya kihuni hivi karibuni.
 
Huu ndio uandishi unaolalamikiwa. Hiyo nusura ya kupigwa mawe haijakaa kwa namna ambayo ina-warrant aina ya headline iliyowekwa
 
Huu ndio uandishi unaolalamikiwa. Hiyo nusura ya kupigwa mawe haijakaa kwa namna ambayo ina-warrant aina ya headline iliyowekwa
si waandishi karibu kila fani imeingiliwa siku hizi lakini zaidi waandishi wetu bure hamna kitu
 
Nimesoma kichwa cha habari nikashikwa na hofu kusoma ndani nakuta duh!!! Jamani uandishi huu haufai kabisa elezeni kitu kilivyo
 
Kuhani akisema wahandisi wetu bomu mnamjia juu... haya sasa kituko hicho.
 
Kiongozi wa kitaifa Utishiwapo kupigwa mawe na wananchi sababu ni kwamba umewaudhi.

Unaweza kuudhi wananchi kwa mambo yako mabaya unayofanya kama kiongozi, mambo yanayoleta kero na kila aina ya uchuro kwa wananchi. Unaweza tishiwa kupigwa mawe kwa kuamua kwa makusudi kushirikiana na watu ulioahidi kuwapiga vita. Pia kushindwa kutimiza ahadi nyingi ulizo ahidi wakati wa uchaguzi.

Kwa upande mwingine unaweza kuudhi watu kiasi cha kutishiwa kupigwa mawe kwa kushindwa kupata wasaa wa kuelezea kinaga ubaga mambo yako mazuri unayofanya yanayo leta mvuto hamu na ari miongoni mwa wananchi.

Ukitaka kuelewa namna kiongozi mzuri unavyoudhi watu kwa mvuto wako, rejea Hadithi ya Sungura kitabu cha Darasa la 3 enzi zile za miaka ya 70.

"Sizitaki mbichi hizi"

Ndizi zimeiva, njano ina Meremeta kama Kamapuni Mazabe ya kuuza Dhahabu ya CCM na wakoloni wake.
Unarukia weee! Wapi Huzifikii.
Unajivuta na kukaa pembeni, huku ukizichungulia kwa jicho la uchungu na tamaa.

Kwa sababu tu huwezi kuzifikia unaamua kuzipaka rangi ya Deep Green na kuziita mbichi, kwa hasira.
Lakini kama akitokea mtu akakupa "Ngwarigo"( Bishop Stick) ukaweza kuzifikia na kuzitia mikononi mwako hulazi damu kuzichangamkia.
 
Kiongozi wa kitaifa Utishiwapo kupigwa mawe na wananchi sababu ni kwamba umewaudhi.

Unaweza kuudhi wananchi kwa mambo yako mabaya unayofanya kama kiongozi, mambo yanayoleta kero na kila aina ya uchuro kwa wananchi. Unaweza tishiwa kupigwa mawe kwa kuamua kwa makusudi kushirikiana na watu ulioahidi kuwapiga vita. Pia kushindwa kutimiza ahadi nyingi ulizo ahidi wakati wa uchaguzi.

Kwa upande mwingine unaweza kuudhi watu kiasi cha kutishiwa kupigwa mawe kwa kushindwa kupata wasaa wa kuelezea kinaga ubaga mambo yako mazuri unayofanya yanayo leta mvuto hamu na ari miongoni mwa wananchi.

Ukitaka kuelewa namna kiongozi mzuri unavyoudhi watu kwa mvuto wako, rejea Hadithi ya Sungura kitabu cha Darasa la 3 enzi zile za miaka ya 70.

"Sizitaki mbichi hizi"

Ndizi zimeiva, njano ina Meremeta kama Kamapuni Mazabe ya kuuza Dhahabu ya CCM na wakoloni wake.
Unarukia weee! Wapi Huzifikii.
Unajivuta na kukaa pembeni, huku ukizichungulia kwa jicho la uchungu na tamaa.

Kwa sababu tu huwezi kuzifikia unaamua kuzipaka rangi ya Deep Green na kuziita mbichi, kwa hasira.
Lakini kama akitokea mtu akakupa "Ngwarigo"( Bishop Stick) ukaweza kuzifikia na kuzitia mikononi mwako hulazi damu kuzichangamkia.

Hii inanikumbusha maneno yaliyotolewa na waziri wa mambo ya nje wa uingereza kwa Mheshimiwa Robati Mugabe pale Zimbabwe miaka minane iliyopita:

FORMER British Foreign Secretary Robin Cook told a Zimbabwean minister that his people would suffer “until they stone you in the streets” if land was not returned to white commercial farmers, according to a new book by Reserve Bank Governor Gideon Gono.

....................

“After an hour and a half in which we were trying to find how we can resolve the question of the land acquisition that was the basis of our conversation, we discovered that the differences were so wide.
...................

“We decided it was necessary to change the topic and discuss other issues. Before we finished, Cook said, and he did not say Honourable Mudenge, he said 'Stan, you have just condemned your people to suffering’. These were his exact words: “They will suffer until they stone you in the streets.'”
 
Hapa kuna kitu kinavundikwa, siku kikiiva tusilie.

Kutishia kumpiga mtu mawe kwa hawa wanakijiji ni kulazimisha matakwa yao yafuatwe...hawataki excuse. Ndio utawala wa sheria unavyotaka hivi, wajichukulie sheria mkononi kama watakavyo ?

Wasiyemtaka wamrushie mawe na wanayemtaka pia? Sio kawaida...nahofia muendelezo wa hii tabia.
 
Hii inanikumbusha maneno yaliyotolewa na waziri wa mambo ya nje wa uingereza kwa Mheshimiwa Robati Mugabe pale Zimbabwe miaka minane iliyopita:


Kichuguu:

Ningependa wananchi waseme kama hatupati maendeleo mawe. Kuhutubiwa na kiongozi kwangu mimi hakuna na tofauti na disco. Disco linapokwisha kila kitu kinasahuliwa.
 
Kichuguu:

Ningependa wananchi waseme kama hatupati maendeleo mawe. Kuhutubiwa na kiongozi kwangu mimi hakuna na tofauti na disco. Disco linapokwisha kila kitu kinasahuliwa.


Ni kweli tunataka maendeleo, lakini pia tunahitaji watu wenye upeo na maono ili kuratibu maendeleo. Mahali pa wali tuwezapo kuwatambuwa viongozi hao ni katika hotuba zao katika hadhara mbali mbali.

Hotuba kutoka kwa kiongozi ni sehemu muhimu katika uwanja mzima wa kupiga hatua katika maendeleo. Katika hotuba kiongozi hujidhihirisha wazi kwa kukusudia au kwa kuto kukusudia. Neno zuri linaweza semwa na kiongozi, lakini ndani ya juhudi za kuhoji maana aua utekelezaji wa neno hilo umadhubuti au udhaifu wa kiongozi hujitokeza wazi. Viongozi wote wababaishaji, kamwe hawawezi kutetea na kusimama imara juu ya maneno waliyoyasema dakika chahche zilizo pita. Mara nyingi hukimbilia kujificha chini ya nukuu" Hamkunielewa, Mnenikuu vibaya, Sikuwa na maana hiyo". Kiongozi yeyote mbababishaji hupenda sana kukaa chini ya kivuli cha mwavuli wa maneno haya ya kibabaishaji.
Kiongozi anaweza toa hotuba nzuri yenye mvuto kwa wananchi kwa sababu tu amejifunza kuongea yale tu wananchi wanapenda kusikia. katika juhudi hizo za kuongea kile wananchi wanapenda kusikia kiongozi huyu hakawii kujipiga ngwala mwenyewe kwa kutoa kauri zinazo pingana au kutoa ahadi zisizo weza kutekelezeka.

Mfululizo wa hotuba za kiongozi yeyote ni dirisha au mlango wa utambuzi wa nia na makusudi ya ndani ya kiongozi yeyote yule duniani. Huhitaji na nabii kumjua kiongozi mwongo mwizi mbabaishaji au kiongazi asiye na dira au agenda ya kubadiri hali za kiuchumi za wananchi.

Hotuba za viongozi wetu wengi zimejaa ujanja wenye unafiki mwingi, aidha zimejaa hila za kifisi fisi zenye wingi wa kuvizia udhaifu wa wananchi.

Tunahitaji hotuba au aina fulani ya uweza wa kiongozi kusikika akinukuu jambo au mambo kutoka katikati ya hisia zake na mwelekeo.

Hotuba za viongozi wetu wengi zina mvuto wa kisiasa lakini zikitazamwa kiuchumi ni sawa na Uharo wa Fisi alo vimbiwa.
 
Na Maregesi Paul, Chunya

"Sisi tunakusubiri kama unavyotuahidi, lakini kama utajifanya mjanja, basi usije ukatulaumu kwani tutaishambulia gari yako kwa mawe," walisikika baadhi ya wakazi hao wakisema.

Mwandishi kaandika story based on some crazy statement shouted out by an anonymous member of the audience!!

Haha hahhahahhaha

Safari tunayo!
 
Waandishi mnawalaumu bure, anaeandika headline ni editor. From time to time naona jinsi wanaJF mnavyowalaumu waandishi. Uandishi wa habari ni wito, kipaji na uwezo. Kama mnavyochangia mada humu JF kuna vichwa, vipaji na uwezo na kuna wasindikizaji.
Waandishi wa Bongo kwa kweli ni kazi ya kujitolea kama kazi ya kanisa, hata wasio na wito, vipaji wala uwezo wamo. Tuwaunge mkono na kuwapongeza kwa jinsi wanavvyojitolea hata kwa hicho kidogo kinachiopatikana.
 
Waandishi mnawalaumu bure, anaeandika headline ni editor. From time to time naona jinsi wanaJF mnavyowalaumu waandishi. Uandishi wa habari ni wito, kipaji na uwezo. Kama mnavyochangia mada humu JF kuna vichwa, vipaji na uwezo na kuna wasindikizaji.
Waandishi wa Bongo kwa kweli ni kazi ya kujitolea kama kazi ya kanisa, hata wasio na wito, vipaji wala uwezo wamo. Tuwaunge mkono na kuwapongeza kwa jinsi wanavvyojitolea hata kwa hicho kidogo kinachiopatikana.

kwani edita siyo mwandishi?
 
lakini kuna point muhimu hapa, hawa wananchi wamezinduka toka zindiko la amani yetu idumu milele, ningekuwA MMI ZITO NINGEHUTUBIA HIVI:

NDUGU WANANCHI WATUKUFU WA KANGA, MTAGUNDUA KUWA RAIS WENU NI MTUMISHI WENU MLIYEMWAJIRI KWA KUMPIGIA KURA NA MNAMLIPA MSHAHARA MZURI KILA MWEZI!

SASA MWAJIRI ANAPOAMUA KUMDHARAU TAJIRI YAKE YAANI NDIYE WANANCHI WA KANGA, KWA KUSHINDWA KUWATOLEA KERO ZENU, KWA KUWA HAPA KERO HAMNA ZAHANATI, BARABARA NK, TENA KWA DHARAU KUBWA ANAWAPITA KAMA GARI MOSHI KUWAHI VIMADA MBEYA, MLIKUWA NA NJIA MBILI ZA KWADHIBU

1. KUSUBIRI HADI KIPINDI CHAKE KIISHE MUMNYIME KURA ZENU, INGWA NJIA HII NI YA MUDA MREFU

2. KUONYESHA HASIRA ZENU KWA KUANDAMANA KUSHINIKIZA AJIUZULU, HII NAYO NI NGUMU KWA KUWA SEHEMU KUBWA YA NCHI WASINGEWAUNGA MKONO KWA AJILI YA UNAFIKI WA CCM.

KWA HIYO KITENDO CHA KUAMUA KUUSHAMBULIA MSAFARA ULE KWA MAWE NI SAHIHI KABISA, TENA 100%, KWA KUWA AMEIPATA FRESH KUHUSU HISIA ZENU ATAAMUA MWENYEWE KUJAZA! TENA KWA KITENDO CHENU KILE KINAFANANA NA YULE MWANDISHI WA HABARI WA IRAQ ALIYEAMUA KUMTUPIA GEORGE BUSH KIATU, KWA HIYO NYIE NDO MASHUJAA MLIOBAKI KWA MFANO WA KINJEKITILE NA WENGINE! MDUMU MILELE
 
Ivyo vichwa vya habari huwa wanavicoin kuweza kuuza magazeti bila kujua kuwa wanawapotosha wananchi.
Bse mara ya kwanza mtanimislead kwa kichwa cha habari nitanunua kichwa cha habari na habari haviendani nitavumilia,second time ivyo ivyo.Third time ilo gazeti au mwandishi nitamwingiza kwenye kundi la waandishi wa mambo ya udaku pamoja na gazeti lake
 
lakini kuna point muhimu hapa, hawa wananchi wamezinduka toka zindiko la amani yetu idumu milele, ningekuwA MMI ZITO NINGEHUTUBIA HIVI:

NDUGU WANANCHI WATUKUFU WA KANGA, MTAGUNDUA KUWA RAIS WENU NI MTUMISHI WENU MLIYEMWAJIRI KWA KUMPIGIA KURA NA MNAMLIPA MSHAHARA MZURI KILA MWEZI!

SASA MWAJIRI ANAPOAMUA KUMDHARAU TAJIRI YAKE YAANI NDIYE WANANCHI WA KANGA, KWA KUSHINDWA KUWATOLEA KERO ZENU, KWA KUWA HAPA KERO HAMNA ZAHANATI, BARABARA NK, TENA KWA DHARAU KUBWA ANAWAPITA KAMA GARI MOSHI KUWAHI VIMADA MBEYA, MLIKUWA NA NJIA MBILI ZA KWADHIBU

1. KUSUBIRI HADI KIPINDI CHAKE KIISHE MUMNYIME KURA ZENU, INGWA NJIA HII NI YA MUDA MREFU

2. KUONYESHA HASIRA ZENU KWA KUANDAMANA KUSHINIKIZA AJIUZULU, HII NAYO NI NGUMU KWA KUWA SEHEMU KUBWA YA NCHI WASINGEWAUNGA MKONO KWA AJILI YA UNAFIKI WA CCM.

KWA HIYO KITENDO CHA KUAMUA KUUSHAMBULIA MSAFARA ULE KWA MAWE NI SAHIHI KABISA, TENA 100%, KWA KUWA AMEIPATA FRESH KUHUSU HISIA ZENU ATAAMUA MWENYEWE KUJAZA! TENA KWA KITENDO CHENU KILE KINAFANANA NA YULE MWANDISHI WA HABARI WA IRAQ ALIYEAMUA KUMTUPIA GEORGE BUSH KIATU, KWA HIYO NYIE NDO MASHUJAA MLIOBAKI KWA MFANO WA KINJEKITILE NA WENGINE! MDUMU MILELE

Na ndio maana wewe sio Zitto. Madaraka ni majukumu/dhamana kaka....

Tanzanianjema
 
"Zitto Anusurika Kupigwa Mawe" sio kichwa sahihi kwa raarifa iliyoelezea matukio katika vijiji vya Kanga na Mkwajuni, Wilayani Chunya wakati wa ziara ya Mhe. Zitto.

Zitto alikuwa na ahadi ya kuhutubia vijiji hivi viwili katika Wilaya ya Chunya. Aliamua kuhutubia Mkwajuni kwanza, na ili kufika huko ukitokea Mbeya ni lazima kupitia Kanga. Shauku ya wakazi wa Kanga kumsikia mwanasiasa huyu kijana machachari iliwafanya baadhi yao kumkumbusha kwamba kuna wenzao wanasota rumande kutokana na kumrushia Rais mawe aliposhindwa kuwahutubia. Zitto aliwashukuru kwa kupenda kumsikia na aliwahakikishia atarudi siku hiyo hiyo na alifanya hivyo saa za alasiri.

Zitto katika hotuba yake kwa wakazi wa Kijiji cha Kanga amedhihirisha umahiri wake wa kisiasa na kizalendo kwa kuwaeleza na kuwaelimisha wananchi juu ya athari za kitaifa kama tutakuwa na utamaduni au tabia ya kurushia mawe viongozi pale tusiporidhika na mienendo au maamuzi yao. Licha ya kwamba Zitto ni kiongozi katika kambi ya upinzani, hii inanipa matumaini kwambaTanzania tunakua.

Kilasara (Junior JF Member)
 
Back
Top Bottom