Kijana: Kama upo kwenye mahusiano, hakikisha una "marafiki" wengine angalau watatu nje

TheChoji

JF-Expert Member
Apr 14, 2009
4,975
15,316
Sio lazima uwe unatembea nao kingono, ila at any time T hakikisha una wanawake angalau watatu warembo "standby", ambao una mawasiliano nao ya karibu. Ukiweza kuwa unawatafuna ni added advantage.

Hii itakusaidia sana kudumisha mahusiano yako ya SASA kwa njia zifuatazo:

1. Itakujengea komfidens ya kuishi na mpenzi wako. Unapokua na wanawake wengine, hata kama huwatafuni lakini inakupa moyo fulani kwamba hata huyu nilie nae akizingua au akiniacha poa tu, kuna wengine wengi.

Hii itabadilisha kabisa maamuzi unayofanya na jinsi unavyom handle mpenzi wako na itakuepusha kufanya mambo mengi ya kiboya. Mathalan, itakuondolea kabisa tabia ya kumlilia lilia mpenzi wako na kumnyenyekea kifala na hata akikupiga chini ni nadra wewe kuumia sana na kuja kulia lia JF nk achilia mbali kujinyonga.

2. Mpenzi wako atakupenda zaidi akijua/akihisi una wanawake wengine unawasiliana nao! Akili za wanawake wanazijua wenyewe. Wanawake wanaamini kwamba mwanaume anaependwa na wanawake wengine huyo ndio mwanaume hasa!😂 Thamani yako kwake inashuka sana akigundua huna mwanamke mwingine yeyote yule zaidi yake!

3. Itapunguza sana migogoro kati yako na mpenzi wako. Mara nyingi unapokua na mpenzi mmoja tu kama roho, hata kosa dogo sana linaweza kukuzwa na kuwa kubwa na kwavile huna pa kupumulia mnajikuta mnagombana sana mara kwa mara. Ukiwa nao wengi, utashangaa vitu vidogo vidogo unapuuzia tu na maisha yanaendelea.

Mfano ukinyimwa gemu wala hauta mind, tena ndio unashukuru maana kwanza unakua umechoka. Ukituma msg asipojibu wala sio ishu maana hapo una watu wengine watatu unawasiliana nao.

4. Inasaidia ku balance attention yako kwa mpenzi wako. Twende mbele turudi nyuma, japokua wanawake hua wanadai wanapenda attention, ila kiukweli ukiwapa sana attention wanakuona boya tu! Mwanamke akishakuona mda wote wewe unamuwaza yeye tu, unachat nayeye tu, mda wowote akikuhitaji upo tu, anakuona lofa tu na anaanza kukuchoka.

5. Inaimarisha tendo la ndoa! Amini usiamini hakuna kitu kinaua "vaibu" kama kua na mwanamke mmoja tu. Kuna kitu wazungu wanaita "sexual monotony" yaani ile hali ya kukinai ku sex na mtu huyohuyo kila siku. Ukiwa na kitu ya pembeni, utashangaa unaimarika hata kwa huyu wa sasa maana ukienda nje ukija kurudi ndani inakua mpya na gemu linakolea hatar.

6. Inakupunguzia gharama! Ukiwa na ka mwanamke kamoja tu, hukawii kujikuta unaanza kuwaza kukafanyia mambo (ya kifala) makubwa kama kukajengea nyumba, kukanunulia gari, kulipa kodi, ada nk!

Kiasi kwamba siku huyo mwanamke akikupiga chini lazima udate ukiwaza uwekezaji uliofanya. Ukiwa nao watatu - wanne, utajikuta unawaza kijanja "hivi kila mmoja akitaka nimjengee nyumba/gari/ada itakuaje?" Utajikuta unafutilia mbali hayo mawazo ya kifala.

NB: Hata kama huna mwanamke nje, tengeneza mazingira ya kumfanya mpenzi wako AHISI kwamba unae. Mfano, potea ghafla hewani kwa muda mrefu, weka simu yako ma passwedi, ma fingerprint nk.

Ukipigiwa simu hata na mshkaji, kaongelee nje. Ukiwa ofisini sema uko home and vice versa ili akija asikukute ahisi upo na mwanamke. Yaani kifupi kuwa mtu usieeleweka eleweka! Utapendwa balaa !! 😁😁
 
Mwenye akili ataelewa,
Mimi nilikuwa na watano 2009 watatu mkoa mmoja wawili mikoa tofauti,
Ndoa nikafunga 2011 Safi na hakuna niliyemwacha na maaumivu!
Kuna mmoja tu alikuja kuniambia "kumbe ulikuwa serious"nikacheka sana alafu ndiye nilikuwa naye karibu sana.
 
Ukwel mtupu ukiwa na mwanamke mmoja kuna possibility ya kua unampa muda wako sana huyo mwanamke na nature ya binadamu akishajua anapendwa sana hata kama na yy anakupenda kuna possibilty ya kuja kuumizwa mbeleni..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom