Shituka kijana, wewe sio benki kwenye mahusiano yako

Intelligent businessman

JF-Expert Member
Sep 6, 2022
26,110
52,836
Vijana wengi wasio na wake wanapaswa kuwa na mafanikio zaidi kuliko walivyo sasa, Lakini kwa sababu wanatumia pesa nyingi kwa wanawake ambao sio wake zao, ndio maana hawafanikiwi.

Bro unajua mapenzi yanaweza kukurudisha nyuma kama usipoingia kwa akili?Ila mapenzi ni matamu sometimes lakini mpaka upendwe kwa dhati.

Unaamini demu wako anawezakuwa drawback yako katika maendeleo? Sa skia mwanangu, usiruhusu mwanamke akutengenezee failure.

Kuna maoni mengi potofu kuhusu pesa na mahusiano kwa baadhi yetu vijana.
Vijana tunapaswa kudhibiti uwezo wetu wa kutaka kuaminisha upendo kwa kuwapatia wanawake ambao sio wake zetu pesa.

Je, huna Mama, Baba, ndugu wanaohitaji?Hao ndio unapaswa kuwasaidia na sio mpenzi wako na familia yake. Hautasonga mbeleMungu hatakubariki kwa kile unachofanya.
Utabarikiwa na Mungu pale tu unapowasaidia wenye uhitaji, wazazi wako, mke wako na watoto wako.

Je, mpenzi wako ni mtu mwenye uhitaji maalum?Je, ulikutana nae kwenye nyumba ya watoto yatima?Ulikutana nae mitaani?Je, alikuwa akiishi vipi kabla ya kukutana nae?Nyote mnahitaji kuwa waangalifu juu ya jinsi mnavyojaribu ku'show love kwa mademu wenu.

You also have to know that women are more loyal to their feelings than your sacrifices.Ni bora mkewako akuulize kwamna"what have you ever done for me?"Kuliko akuulize dem hilo sio jukumu lako we sio baba yake. Wanawake wanapenda pesa, na ukitaka kuwapa kwa sana, hawata zikataa.

Lakini usifikiri kwamba matumizi yako juu yake, yatakuhakikishia chochote. Tumeona mara ngapi jinsi wanaume wanavyolipia ada mademu chuo, Na mwisho wake waliwaacha??Unatakiwa kumpa nini mpenzi wako?Zawadi za hapa na pale, kulipa bili unapoenda maeneo ya starehe, na mara chache unaweza kumsaidia kwa fedha kidogo pale tu inapohitajika.

Na hata sio inshu ya kufanya wiki chache baada ya kukutana nae. Lazima uchukue muda kumjua ni mtu wa aina gani.

Pesa yoyote unayotumia kwa demu sio investiment, haijalishi ni kidogo kiasi gani. So, fanya kidogo unachopaswa kufanya where necessary, Lakini usije kuingia kwenye deni kwa sababu yake.

Usikope pesa kwa sababu ya mpenzi wako.Usilipe ada zake Usimlipie kodi.Ngoja nikuambie.Unachodaiwa na mpenzi wako ni yeye kukuona ukiendelea.

Acha akuite bahili lakini akiona maendeleo unayo yapata katika maisha atalazimika kuendana na mifumo yako kwa sababu anajua unajenga maisha yajayo.Kama hataki kuwa na subira, mwache aende zake.

Yeye hatokulisha wewe.Wewe ndiye utamlisha.Kumpa pesa sana, unajiweka kwenye hali ya kushindwa kufanya maendeleo yako.
Hutakuwa na akiba na hutapata baraka zozote kutoka kwake Utakachopata ni usaliti, majuto na machozi.

Mnapopigiwa mademu hamuumii kisa kukaziwa, Mnaumizwa na pesa na muda mliopoteza kwa watu ambao sio sahihi.

I mean no malice to nobody!
FB_IMG_17085026693220480.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom