Intelligent businessman
JF-Expert Member
- Sep 6, 2022
- 26,102
- 52,801
Mwanamke, mwanamke, mwanamke, mwanamke, mwanamke.
Kuna mamilioni ya wanaume ndoto zao zilikufa kwa sababu ya wanawake, na kuna mamilioni ya wanaume ndoto zao zilisonga na kufanikiwa kwa sababu ya wanawake. Mpaka leo sijaoa, sijaoa kwa sababu sijaona sababu ya kufanya hivyo kwanza.
Naona ndoa nyingi zikianguka, naona ndoa nyingi zikiingia kwenye umasikini, naona mambo makubwa na ya kutisha sana kwenye ndo, mambo ambayo mtu yanakupa hofu ya kutaka kufanya maamuzi ya kuingia kwenye ndoa.
Nawaona watu wengi waliokuwa na ndoto kubwa wakizipoteza baada ya kuoa, nawaona watu wakiharibikiwa maisha yao baada ya kuingia kwenye ndoa. Nawaona wanandoa wanaofanikiwa ni wachache kuliko wanaoanguka na kupoteza misingi ya ndoto zao.
Mimi sio Muislamu, mimi si Mkristo, nitakapooa, no turning back. Nikimpa mwanamke ambaye hana ndoto kubwa, nini kitatokea endapo nitamshikirisha na kumwambia ndoto zangu? Ataniona mjinga fulani ninayekaribia kuchanganyikiwa ama ataniona mtu mwenye akili.
Siku Nikipata mpenzi, nitajiuliza, huyu mwanamke ataweza kuishi na mwanaume mwenye bilioni kumi kwenye akaunti? Je, anaweza kuzifanya zile bilioni kumi ziwe ishirini ama hamsini? Huwa ninawaza mambo mengi sana ambayo mwisho wa siku nasikia sauti ikiniambia “Subiri”.
Siku ukiwa huna je atakuwa na wewe au ndo itakuwa ndo Safari ya kwenda?!,
Jifunze kuchagua kitu sahihi kwako, mtu ambaye mna weza kwenda speed moja.
Kuna mamilioni ya wanaume ndoto zao zilikufa kwa sababu ya wanawake, na kuna mamilioni ya wanaume ndoto zao zilisonga na kufanikiwa kwa sababu ya wanawake. Mpaka leo sijaoa, sijaoa kwa sababu sijaona sababu ya kufanya hivyo kwanza.
Naona ndoa nyingi zikianguka, naona ndoa nyingi zikiingia kwenye umasikini, naona mambo makubwa na ya kutisha sana kwenye ndo, mambo ambayo mtu yanakupa hofu ya kutaka kufanya maamuzi ya kuingia kwenye ndoa.
Nawaona watu wengi waliokuwa na ndoto kubwa wakizipoteza baada ya kuoa, nawaona watu wakiharibikiwa maisha yao baada ya kuingia kwenye ndoa. Nawaona wanandoa wanaofanikiwa ni wachache kuliko wanaoanguka na kupoteza misingi ya ndoto zao.
Mimi sio Muislamu, mimi si Mkristo, nitakapooa, no turning back. Nikimpa mwanamke ambaye hana ndoto kubwa, nini kitatokea endapo nitamshikirisha na kumwambia ndoto zangu? Ataniona mjinga fulani ninayekaribia kuchanganyikiwa ama ataniona mtu mwenye akili.
Siku Nikipata mpenzi, nitajiuliza, huyu mwanamke ataweza kuishi na mwanaume mwenye bilioni kumi kwenye akaunti? Je, anaweza kuzifanya zile bilioni kumi ziwe ishirini ama hamsini? Huwa ninawaza mambo mengi sana ambayo mwisho wa siku nasikia sauti ikiniambia “Subiri”.
Siku ukiwa huna je atakuwa na wewe au ndo itakuwa ndo Safari ya kwenda?!,
Jifunze kuchagua kitu sahihi kwako, mtu ambaye mna weza kwenda speed moja.