Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,197
- 25,516
Ni taarifa rasmi iliyotolewa na CHADEMA kuwa Halima Mdee na wenzake 18 walifukuzwa uanachama wa CHADEMA kwa makosa mbalimbali waliyoyatenda dhidi ya chama chao. Walifukuzwa na Kamati Kuu ya chama hicho.
Ikaripotiwa na hata kusemwa na mmoja wa waliofukuzwa uanachama Bungeni Dodoma (Jesca Kishoa) kuwa wapo waliofukuzwa uanachama ambao walikata rufaa kupinga kufukuzwa kwao uanachama. Mamlaka ya rufaa imeripotiwa kuwa ni Baraza Kuu la CHADEMA.
Mamlaka za kibunge zinasubiri uamuzi wa CHADEMA juu ya rufaa ya akina-Halima Mdee ili ziweze kuchukua hatua stahiki. Spika Tulia ameshasema Bunge linaendeshwa kidemokrasia na kisheria. Unasubiriwa uamuzi tu wa CHADEMA.
Ni miezi mingi sasa imepita tangu akina Halima Mdee wafukuzwe uanachama na baadhi yao kukata rufaa. Lini hasa rufaa zao zitasikilizwa na uamuzi wa mwisho kichama kutolewa juu yao? Ukimya huu ni baraka za kificho kuwa akina Halima Mdee waendelee na mambo yao ukiwemo Ubunge?
Ikaripotiwa na hata kusemwa na mmoja wa waliofukuzwa uanachama Bungeni Dodoma (Jesca Kishoa) kuwa wapo waliofukuzwa uanachama ambao walikata rufaa kupinga kufukuzwa kwao uanachama. Mamlaka ya rufaa imeripotiwa kuwa ni Baraza Kuu la CHADEMA.
Mamlaka za kibunge zinasubiri uamuzi wa CHADEMA juu ya rufaa ya akina-Halima Mdee ili ziweze kuchukua hatua stahiki. Spika Tulia ameshasema Bunge linaendeshwa kidemokrasia na kisheria. Unasubiriwa uamuzi tu wa CHADEMA.
Ni miezi mingi sasa imepita tangu akina Halima Mdee wafukuzwe uanachama na baadhi yao kukata rufaa. Lini hasa rufaa zao zitasikilizwa na uamuzi wa mwisho kichama kutolewa juu yao? Ukimya huu ni baraka za kificho kuwa akina Halima Mdee waendelee na mambo yao ukiwemo Ubunge?