Amefariki muda si mrefu kwa ajali ya gari akitokea Dodoma kuelekea Dar es Salaam eneo la Pandambili (kama sijakosea).
PICHA:
Marehemu Chacha Wangwe...
Mzee Mwiguni George aliyefika katika eneo na kumsaidia Chacha na wenzake!
Deus Francis Mallya aliyetoa maelezo yenye utata na sasa watu wanamgeuzia kuwa kuna jambo analificha! (Huyu pia aliwahi kujitambulisha kuwa yeye ndiye (mimi) Invisible wa JF.
Gari lililohitimisha maisha ya Chacha likiwa limeharibika vibaya
RIP Wangwe...Natumia FURSA HII PIA KUFUTA USEMI WA KULIMWA RISASI KWA WANGWE.
Bwana ametoa...Na Bwana ametwaa.
Pia naomba radhi kwa Mgagagigikoko...Na wale waliokuwa na mawazo ya tofauti kama ilivyojionyesha kwenye issue ya Marehemu Bhoke...Tutoe nafasi hii kwa wanachadema na wanafamilia bila kusahahu Taifa kwa ujumla kwenye majonzi haya.
Kweli wanadamu si kitu na ni budi tufanye majukumu yetu mara moja kwani maisha haya ni mafupi na tuko duniani kwa malengo...Tuhakikishe tunayatambuwa malengo ambayo Mungu ametuleta hapa Duniani kuyatimiliza.
Ili tusije kuondoka kabla ya kuyatimiliza.
La kujiuliza hapa...Je Wangwe aliyafanya yale aliyoletwa kuyafanya na MUNGU ALIYEKUWA AKIMWAMINI?
Kama watu kuugua mafua tu na kulazwa Muhimbili kwa mapumziko mafupi inahusishwa mara moja na mambo ya kisiasa sembuse huyu aliyekuwa mlengwa mkuu katika mgogoro wa uongozi hapo Chadema.