Kifo cha CCM kimetimia

Kifo cha CCM kimetimia

WaTanganyika wenzangu.

Ni wakati muhimu sasa tukatambua kwamba, kwa miongo mingi ya utawala wa serikali ya CCM, nchi imekuwa ikiendeshwa kama taasisi ya watu binafsi. Chini ya uongozi na himaya ya CCM na serikali zake, Tanganyika imekuwa ikifisadiwa huku waTanganyika tuki dhulumiwa katika nyanja zote kiuchumi, kisiasa na kijamii pia.

Mateso kwa waTanganyika yamefikia kiwango cha juu kiasi kwamba wengi wetu tunaona ni afadhali nchi hii ingeendelea kuwa chini ya utawala wa kikoloni.

Nasema "RAIS WA KUJENGA NIDHAMU YA SERIKALI HAWEZI KUTOKA CCM" kwa sababu viongozi waliopo ndani ya CCM, wote ni zao la "SERIKALI ISIYO KUWA NA NIDHAMU".
 
Kwa hiyo mnataka viongozi wa CCM wawafundishe mpaka nidhamu ya kuacha uzinifu?
 
Thatz true, hawa wenzetu wameigeuza nchi kama taasisi yao binafsi. Leo watanzania wanasema huwezi kupandishwa cheo kama wewe cyo Ccm, inamaana utaalamu na taaluma hawavitambui ila wao wanatambua uanachama wa kuwa Ccm. Sasa tutafika kweli?
 
Fanya kazi kwa bidii ujenge maisha yako. Acha porojo...

Bora uumshauri naye aje hapo Lumumba ili awe mwanachama wa jf kwani hata wewe unashinda hapa jf wakati unawashauri wenzako wafanye kazi. Acha ujinga wewe.
 
Fanya kazi kwa bidii ujenge maisha yako. Acha porojo...
Cc: Nape Nnauye , KINAna jangili , Ritz Simiyu Yetu and all LB7 project
988346_353943881409285_817670396_n.jpg
 
Last edited by a moderator:
Licha ya jitihada wanazofanya CCM za kuzima upinzani kushika kasi nchini kwangu mimi inatosha kusema CCM ni lazima iondoshwe madarakani.

CCM wala wasijidanganye kuwa kuiua Chadema au chama chochote cha upinzani kinachotishia uwepo wake madarakani ndio itawafanya waiongoze nchi hii daima na milele!

Na kama wameweza kuisikia kauli 'nchi hii haitatawalika' in theoretical frame work basi wategemee vitendo zaidi katika kulitekeleza hilo, hasa baada ya njia ya sanduku la kura kushindikana.

Nayasema haya kwa kupima muelekeo wa Tanzania yetu, hali ngumu ya kimaisha kwa watanzania, wizi wa rasilimali, ufisadi kwa viongozi ndani ya CCM, umasikini uliokithiri kwa watanzania, kasi ya ujangiri nchini inayohisishwa na viongozi ndani ya CCM na maovu mengi yamayotokea nchini.

CCM haiwapendi watanzania na ndio haiwajali. Naandika thread hii kwa uchungu sana hasa ukizingatia CCM inafanya jitihada kubwa sana kuwapoteza inaowakosoa.

Kama hatutawaondoa hawa manyang'au kwa kura basi tutawaondoa kwa namna nyingine yoyote ile. CCM wamepoteza legitimacy ya kuiongoza hii nchi. Umeona wapi nchi ikaongozwa na kauli mbiu.

Nataka niwambie, wakati mkiwa mnafurahi malumbano ya Lema na Zitto kwa wakati huu mkiwa mnaamini kuwa chadema inadhoofika, mkae mkijua kuwa kifo chenu kimewadia. Hiyo siku mtaifahamu vizuri Tanzania na Watanzania. Hapo ndipo mtajifunza kilichomkuta Fuldencia Batista kule nchini Cuba.
 
Wadau

Nimetafakari kwa makini sana,Kuna kila dalili kwamba CCM wanatengeneza migogoro ndani ya Chama kikuu cha Upinzani nchini Tanzania,Chama hicho ni CHADEMA ambacho kinatakiwa kife kabla ya 2014/2015,Hiyo ni kwa mujibu wa WanaCCM Kama Wassira,

Kwa mtazamo wangu,Hata kama Chadema kitakufa, Wananchi watakiondoa CCM madarakani kwa namna yoyote kwa kuwa Chama hiki kimeshindwa kabisa kulisaidia Taifa hili,Kwa mfano mdogo tu,CCM imeamua kwa makusudi kuua elimu yetu kwa kuanzisha division five;

CCM inaondoka.
 
mjomba , kila wanachopanga kinatufikia hata kabla hakijapauka ! Akili ndogo haiwezi kuua chadema .
 
wadau

nimetafakari kwa makini sana,kuna kila dalili kwamba ccm wanatengeneza migogoro ndani ya chama kikuu cha upinzani nchini tanzania,chama hicho ni chadema ambacho kinatakiwa kife kabla ya 2014/2015,hiyo ni kwa mujibu wa wanaccm kama wassira,

kwa mtazamo wangu,hata kama chadema kitakufa, wananchi watakiondoa ccm madarakani kwa namna yoyote kwa kuwa chama hiki kimeshindwa kabisa kulisaidia taifa hili,kwa mfano mdogo tu,ccm imeamua kwa makusudi kuua elimu yetu kwa kuanzisha division five;

ccm inaondoka.

cdm imeletwa na mungu , mkazi wa bagamoyo hana uwezo wa kuiua !
 
Wadau

Nimetafakari kwa makini sana,Kuna kila dalili kwamba CCM wanatengeneza migogoro ndani ya Chama kikuu cha Upinzani nchini Tanzania,Chama hicho ni CHADEMA ambacho kinatakiwa kife kabla ya 2014/2015,Hiyo ni kwa mujibu wa WanaCCM Kama Wassira,

Kwa mtazamo wangu,Hata kama Chadema kitakufa, Wananchi watakiondoa CCM madarakani kwa namna yoyote kwa kuwa Chama hiki kimeshindwa kabisa kulisaidia Taifa hili,Kwa mfano mdogo tu,CCM imeamua kwa makusudi kuua elimu yetu kwa kuanzisha division five;

CCM inaondoka.

Refer to mheshimiwa Wasira,alisema cdm hisinge fika 2013,Leo hii ndio cdm inazidi kuchapa mwendo,wanachama lukuki wazee kwa vijana.
 
chadema haifi wewe, acha woga, chadema ndo inazidi kuimarika.
 
Chadema sio ya kufa,iliyokwisha kufa kiuongozi ni ccm yasubiriwayo ni mazishi yake 2015 kisha chadema ipokee kijiti kuendeleza mapambano na harakati za bara africa kwa ujumla.>>>"aluta continua".
 
Wadau

Nimetafakari kwa makini sana, CHADEMA kinatakiwa kife kabla ya 2014/2015, Hiyo Kwa mtazamo wangu,Hata kama Chadema kitakufa, Wananchi watakiondoa CCM madarakani kwa namna yoyote CCM inaondoka.
Mkuu Frank, kama Chadema itakufa, na 2015 CCM itaondoka au itaondoshwa, then Tanzania itatawaliwa na nani?.
Naomba nichukue fursa hii kukuandaa kisaikolojia ili usije kuishiwa kuwa frustrated ile 2015!.

Kwanza ondoa wasiwasi, Chadema haifi!, ila kwa 2015, Chadema itakuwa bado!, hivyo ni CCM tena!. Si unaona uchaguzi wa serikali za mitaa ni kesho tuu!, angalia leo Chadema wako busy na nini!, ingekuwa ni CCM ndio wanaowakeep busy, ungesema ni mbinu za kuwadhoofisha, lakini wako busy wenyewe tuu, maandalizi ya 2015 watafanya saa ngapi?, wakati determinant ya ushindi wa 2015, ni ushindi wa 2014!.

CCM ni chama cha mafisadi, CCM imekubuhu kwa rushwa, yaani imeoza, inanuka!, kwa kifupi, CCM ni li zimwi!. Kama mpaka 2015, Tanzania bado tutakuwa hatuna mbadala wa CCM, then nakuhakikishia kuwa kuliko kuchagua upepo kutuendeshea nchi, Watanzania, wataamua bora wairudishe hiyo hiyo CCM!, japo ni li zimwi!, lakini ndilo zimwi pekee likujualo!, halikuli likakwisha!, litakubakisha japo mifupa!.

Hata hivyo, kwa vile Mungu yupo, na miujiza pia ipo, au tusubirie miujiza, au jiandae kwa CCM tena, ile 2015!.

Pasco.
 
Mkuu Frank, kama Chadema itakufa, na 2015 CCM itaondoka au itaondoshwa, then Tanzania itatawaliwa na nani?.
Naomba nichukue fursa hii kukuandaa kisaikolojia ili usije kuishiwa kuwa frustrated ile 2015!.

Kwanza ondoa wasiwasi, Chadema haifi!, ila kwa 2015, Chadema itakuwa bado!, hivyo ni CCM tena!. Si unaona uchaguzi wa serikali za mitaa ni kesho tuu!, angalia leo Chadema wako busy na nini!, ingekuwa ni CCM ndio wanaowakeep busy, ungesema ni mbinu za kuwadhoofisha, lakini wako busy wenyewe tuu, maandalizi ya 2015 watafanya saa ngapi?, wakati determinant ya ushindi wa 2015, ni ushindi wa 2014!.

CCM ni chama cha mafisadi, CCM imekubuhu kwa rushwa, yaani imeoza, inanuka!, kwa kifupi, CCM ni li zimwi!. Kama mpaka 2015, Tanzania bado tutakuwa hatuna mbadala wa CCM, then nakuhakikishia kuwa kuliko kuchagua upepo kutuendeshea nchi, Watanzania, wataamua bora wairudishe hiyo hiyo CCM!, japo ni li zimwi!, lakini ndilo zimwi pekee likujualo!, halikuli likakwisha!, litakubakisha japo mifupa!.

Hata hivyo, kwa vile Mungu yupo, na miujiza pia ipo, au tusubirie miujiza, au jiandae kwa CCM tena, ile 2015!.

Pasco.

Wewe mara nyingi una hoja kuu 3 linapokuja suala la CDM, 1 ni ccm inahitaji mbadala nayo ni CDM, 2 ni CDM hawako organized ktk mambo mengi na 3 ni Zitto anaonewa na CDM, mi nakubaliana nawe kwa 1 na 2 ila ya 3 hapana, moja ya sababu kwanini zito anaihujuma CDM ni kwa kuwa hoja namba 2 ina ukweli
 
Wadau

Nimetafakari kwa makini sana,Kuna kila dalili kwamba CCM wanatengeneza migogoro ndani ya Chama kikuu cha Upinzani nchini Tanzania,Chama hicho ni CHADEMA ambacho kinatakiwa kife kabla ya 2014/2015,Hiyo ni kwa mujibu wa WanaCCM Kama Wassira,

Kwa mtazamo wangu,Hata kama Chadema kitakufa, Wananchi watakiondoa CCM madarakani kwa namna yoyote kwa kuwa Chama hiki kimeshindwa kabisa kulisaidia Taifa hili,Kwa mfano mdogo tu,CCM imeamua kwa makusudi kuua elimu yetu kwa kuanzisha division five;

CCM inaondoka.

Ikitokea CDM ikafa itakuwa ni wao wenyewe kushindwa kujimudu na kulewa sifa. Ni lazima wathibiti hali ya hewa ndani ya chama ili kipate dhamana ya kuongoza nchi. Kama misuguano ya ndani itaendelea wajikumbushe NCCR MAGEUZI ilivyokuwa 1995 na nini kiliiangusha.
 
Wewe mara nyingi una hoja kuu 3 linapokuja suala la CDM,
  1. ni ccm inahitaji mbadala nayo ni CDM,
  2. ni CDM hawako organized ktk mambo mengi na
  3. ni Zitto anaonewa na CDM,

mi nakubaliana nawe kwa 1 na 2 ila ya 3 hapana, moja ya sababu kwanini zito anaihujuma CDM ni kwa kuwa hoja namba 2 ina ukweli
Mkuu JGG, kwanza naomba nikupongeze kwa kukubali kuwa mkweli, watu wakweli humu jf, wanaokubali ukweli halisi jinsi ulivyo ni wachache, na wewe uu mmoja wao!. Wengi wa member humu, wanaukubali ule ukweli wao tuu, sometimes sio ukweli halisi!.

Naimba kukurekebisha na kukusaidia kidogo ila pia kukuongezea kidogo na ukweli mchungu!.

  1. Sio kweli kuwa CCM, inahihitaji mbadala!, CCM inatamani kutawala milele, kama hapatokea mbadala, CCM itaendelea kutawala, na kutawala na kutawala!, kwa wale waliotangulia mbele ya haki, na wale watakaotangulia mpaka 2015, kwao CCM imetawala milele yao yote mpaka mwisho wa maisha yao!, na kwa 2015 itaendelea kutawala milele ya wengine wengi!.
  2. Ili CCM iondoke, lazima kwanza apatikane mbadala na sio lazima Chadema!, ila mpaka hapa tulipofikia, Chadema ndicho chama pekee kimeonyesha dalili ya angalau angalau, lakini tatizo lao ndiolo hilo hili nililowaambia "Hawajajipanga!' japo walikuja juu, facts are facts hazina mjadala, ni ama wajipange, ama 2015 ni CCM tena!.
  3. Hili za ZZK kuonewa Chadema naomba let me reserve my comments, si umeona juzi baada ya yule "chalii wa kijiweni" kututapikia humu ule utumbo,humu sebuleni, kale "ka kinda ka juzi" nacho kakasupport kuongeza matapishi!, na uha.. kujazia!, una sasa sebule nzima imechafuka!, jee umeona mpaka leo wenye nyumba wamefanya nini?, nilitegemea wakekuja mbia kusafisha matapishi yale!, lakini kila siku wanapita tuu hapo sebuleni kwa kutafuta pa kukanyaga ili wasijichafue na matapishi hayo lakini sio kutasafisha!. Kama matapishi yale yangekuwa ni wa "wapendwa wao" hata kabla wenye nyumba hawajafika, ungeshuhudia "madekio yao humu" jinsi wanakimbizana kugombea kusafisha uchavu ule, na wengine ambao hawana mop, wangekuwa tayari hata kuyafuta kwa ulimi, na hata kama hakuna mahali karibu pa kutupa, wangeamua hata kuyameza matapishi hayo kuliko sebule kuchafuka!. (Hapa ndio nime reserve my comments!, ningeamua kusema!, patakuwa hapatoshi hapa!).
Pasco.
 
Back
Top Bottom