Kifo cha CCM kimetimia

activisty

JF-Expert Member
Apr 1, 2012
315
107
Ikiwa ni muda mrefu umepita,tokea watanzania tupate uhuru, tukiwa chini ya utawala wa TANU, hatimaye CCM bado mabadiliko makubwa hayajafanyika kuonesha malengo ya kulipatia taifa letu maendeleo. Awamu ya kwanza ilianza vyema, lakini mawazo ya Mwalimu JK Nyerere yalipoanza kukiukwa katika awamu ya pili, ya tatu na hatimaye ya nne ndio sasa watanzania tunaona tuko katika jehanamu iliyojaa chuki,njama,ufisadi, na umaskini uliokithiri.

Ni ukweli usiofichika CCCM na uongozi wake wote imeshindwa kutatua matatizo yanayotukabili, na niseme imekuwa ikituongezea tabu kila kukicha. Nianze na MGOMO WA MADAKTARI, AJALI ZA ZANZIBAR, SUALA LA MUUNGANO,KILIMO n.k vyote vinatabiri kifo cha CCM, kwa kuzingatia kuongezeka kwa machafuko nchini.

Watanzania walio wengi wenye akili timamu na hekima nadhani tayari wameshajiandaa kufanya mabadiliko makubwa 2015 ,na namini itakuwa ndio mwisho wa utawala wa kidhalimuna dhaifu wa CCM!

NA HICHO NDICHO KIFO CHA CCM 2015!

-------------------------------

Kwa wapenzi wote wa mapinduzi na chama cha mapinduzi, ninasikitika kwatangazia kuwa kile chama chetu kipenzi, CCM kimeaga dunia ya siasa za Tanzania. Aidha, maandalizi ya nyimbo za maombolezo kutoka kwa mtunzi wetu maarufu Yohana Simba na kunafanyika utaratibu wa kisheria wa kukabidhi madaraka kwa chama kingine 2015 kwa amani, kabla ya kuizika CCM rasmi 5/2/2017 wakati kimetarajiwa kutimiza umri wa miaka.

Hakuna utawala wa milele hapa duniani na historia haionyeshi kuwepo kwa chama kichotawala hata kwa miaka 100 mfululizo kama makada wachumia tumbo wa CCM wanavyotoa propaganda zao. Hizo ni propaGammba tu.Roman empire na Hata Mkwawa Chiefdom ni mfano mdogo tu. Kwa kawaida, viumbe wafao wakiwa wametulia ni wachache sana, hata watu.Mara nyingi, hata yule mgonjwa mahututi anapoaga dunia anaweza kuhangaika kiasi cha kuwa na nguvu ambazo hapo awali alidhaniwa kutokuwa nazo. Mambo yanayoendelea sasa ni dalili tosha hata na kwetu tusiojua kufa kuwa chama chetu kipenzi kimeshatuacha.

Nawaomba wote,wapenzi na maadui wa CCM msitaharuki kwa msiba huu mkubwa.Mtakumbuka kuwa aliyekuwa katibu wake mkuu alishasema kuwa CCM imepoteza dira na hii ilitokana chama hicho kupoteza fahamu.Hapo wakakipeleka ICU kule Chimwaga na kwa batati mbaya sana, mgunduzi wa ugonjwa ule akafariki dunia kama watafiti na wagunduzi wengine wanavyoathirika na tafiti zao juu ya visivyojulikana . Na kabla ya hapo mwanzilishi wake na mwenyekiti wake wa kwanza, alipoona kuwa hali ni mbaya akatumia hekima kuishinikiza serikali ikubali kuwepo vyama vingine vya siasa na akaona kuwa CHADEMA ndiyo chama makini na chama mbadala kwa CCM aliyoiasisi.Jitihada za kukinusuru chama kisife zilishashindikana kutokana na chama hicho kukumbwa na ugonjwa hatari unaojulikana kitaalam 'scalosis' yaani utokaji wa magamba sehemu zote kuanzia kamati kuu na magaba hayo kuendelea kukua na kukomaa na kukakamaa kiasi cha kusababisha maumivu makubwa na migawanyiko ya kimakundi(scales) yasiyoweza kutoweka kwa dawa yoyote inayojulikana.

Swali sasa si kama CHADEMA kipo tayari kuwa chama tawala au la bali uhai wake kisiasa halali za kuongoza nchi kwa kuimbiwa nyimbo za hamasa na wananchi wengi kama ilivyokuwa kwa marehemu CCM utadumu hadi lini?Je ugonjwa wa 'scalosis' uliokiua CCM hautakipata na chenyewe?Ujonjwa huu ambao kinga yake pekee ni kuondoa sehemu iliyoathirika mapema iwezekanavyo na kuichoma moto chini ya uangalizi mkali ili mavumbi yake yasiguse sehemu nyingine ya mwili unahitaji umakini sana kwani hiyo kinga isipotumia vema inakumaliza pia.Ni jukumu la wanaCHADEMA wote, kutuhakikishia watanzania uwezo wenu wa kutuongoza vema bila ya ugonjwa huu hatari.

Ushauri wangu kwa watanzania wote, wakati kipindi hiki kigumu cha msiba wa mpendwa wetu CCM, tusitafutane uchawi kwani 'kazi ya mungu haina makosa'.Tusizushiane na kutoana kucha kwani tunaumizana bure wakati kila chenye mwanzo kina mwisho.Iacheni CCM yetu ipumzike kwa 'amani na utulivu' uliyojivumia kuuleta. Tanzania ni yetu sote hivyo ni vema tuepukane na vurugu ambazo hazitatusaidia kwa vyovyote vile. Na wale ambao wana dhamana yoyote kijamii ni vema wakitumia fulsa zao vema ili baadae wasijisikie vibaya wakati wa kuijenga Tanzania mpya yenye katiba mpya, mtazamo mpya na matumaini mapya. Sisi wa CCM tuwe tayari kushirikiana na wengine wakati huu wa mazishi ya kipenzi chetu CCM hata wakati ule wa maziko rasmi pale Chimwaga.Wale wa CHADEMA, huu si muda mzuri wa kumsimanga marehemu bali timizeni wajibu wenu kwa jamii kwa kuwa fair kwa wote hata wale wanaowatendea vibaya sasa kwani kisasi ni cha Mungu kulipa na si ninyi.Hatimaye watu wengi watawaelewa na kuwakubali kwani ukombozi ni 'process'.

Mwisho, ninawapa pole wote walioguswa na msiba huu na nawasihi wawe watulivu na wavumilivu hadi pale mwenyekiti wetu atakapotuongoza katika maziko pale Chimwaga 5/2/2017.
Amina.

CCM ya Kikwete imewafikisha watu waamini kwamba amani na usalama ni kukaa kimya kama kondoo wenye hofu. CCM inatumia hofu hii iliyopandikizwa kuendeleza dhuluma, kukalia haki za watu na kutumia polisi kuaminisha kwamba Tanzania leo kuna magaidi. CCM walianza kupandikiza hofu ya "magaidi' katika uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga mwaka juzi, wakati aliyekuwa Katibu mkuu wa CCM, Wilson Mukama alipotangaza kapata habari kwamba CHADEMA wameingiza Mungiki wa Kenya. Polisi hawakuwa na habari na hawakumhoji Mukama.

Mwaka jana, Katibu wa Uchumi wa CCM, Mwigulu Nchemba alizunguka nchi nzima akidai ana mkanda unaoonyesha ugaidi wa CHADEMA. Polisi walijiweka kando na madai hayo. Na pale walipoona wimbi la watu kuhama analojia na kuingia digitali (CHADEMA) linazidi kuongezeka ndipo ‘CCM' wakamkamata Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa CHADEMA, Wilfred Lwakatare kwa madai ni gaidi.
Mwaka jana Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alizunguka nchi nzima akitangaza kwamba Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa ana kadi ya CCM.

Siku Juliana Shonza alipotimuliwa uanachama wa CHADEMA, alikusanya waandishi wa habari na kutapika mambo mengi, mojawapo ni kwamba kuna matumizi mabaya ya fedha za chama. Baada ya kusomea propaganda ndani ya CCM na wakahitimu, wiki iliyopita Shonza na Mtela Mwampamba waliibuka na kudai Dk. Slaa ana mpango wa kumuua Naibu wake, Zitto Kabwe. Makada wawili hao wakaeleza hata mpango huo ulivyo.

Pamoja na kwamba tuhuma hizo nzito zinahitaji Jeshi la Polisi kufanyia kazi, Shonza na Mwampamba wameachwa huru hata kukemewa tu. Hapo ndipo ujue Shonza na Mwampamba, kama ilivyokuwa kwa Nape, Mwigulu na Mukama wametumwa na CCM kutia hofu kama rais mwenyewe aliyedai amesomewa itikafu na misikiti mitatu, lakini amekaa kimya. Kweli rais wa nchi anaombewa afe lakini hachukui hatua? Hii ndiyo CCM!
Nini maana yake CCM? Mtambo huu wa analojia CCM unapaswa kuzimwa 2015 ili kupitia digitali wananchi wapate usikivu mzuri wa habari na waone picha nzuri ya uhuru wao, demokrasia, uchumi, elimu, afya, ustawi wa jamii, mazao yao, barabara zao, uhusiano wao, heshima yao, utu wao na viongozi wasioshinda misibani.

Mimi kama mwananchi mwenye kuipenda nchi yangu, nasikitika kwa ninayoyaona kwa miaka hii. Na kwa haya napenda kuitahadharisha serikali kuwa Michezo yao ndio mauti yetu. Tumefikia mahali, kila kitu kinakwenda hovyo hovyo. Si elimu, si afya, si nishati, si madini, si usalama wa nchi. What the hell is going on? A bunch of overgrown teenagers are running the country into chaos, viongozi wapo wanachekelea tu. Nchi inapiga siasa, asubuhi mpaka jioni. Hata vyombo visivyo vya kisiasa na vyenyewe vimejikita kwenye siasa.

Tanzania imekuwa kama Somalia, Afghanistan! where is the government and its institutions? Nimeangalia tukio la hivi karibuni la kuhusu Lwakatare na kwa kiasi kikubwa nimeshangazwa kuwa wapo watu au kikundi cha watu walioko juu ya sheria na sheria za nchi haziwahusu wao hata kidogo.

Hivi kama polisi wangekuwa wanatenda haki, yule kiongozi wa kisiasa aliyesema ana mkanda wa video kuonyesha viongozi kadhaa wakipanga mauaji, je waliwahi kumkamata na kumuhoji? Na iweje aseme yeye halafu baada ya muda ndio video hiyo ionekane, je si yeye aliyeiweka kwenye you tube? Yeye ndiye suspect wa kwanza kwenye hili.

Naiasa serikali kuwa Michezo Yenu Ndio Mauti Yetu. Amani ya nchi ikipotea kuirudisha ni ngumu, mifano ipo mingi. Na wenzangu tunaoshabikia vitu havina mbele wala nyuma vya kutoka sijui twitter, you tube na face book, tunaofurahia na kuendeleza ubaguzi wa kisiasa, kidini, kikanda n.k hatutakuwa salama mambo yakiharibika. Hata wenye dhamana ya vyombo vya ulinzi na usalama, hamtakuwa salama hali ya amani ya nchi ikitoweka.

Oneeni huruma watoto wenu hata kama ninyi mmechoka kuishi.Tuungane kulaani kwa nguvu zote matukio ya kihuni tunayoyashuhudia kwenye nchi yetu, mauaji na mateso ya raia wasio na hatia. Upendeleo wa waziwazi wa polisi na kukosa uwajibikaji wa dhati kwa wananchi walioapa kuwalinda pamoja na mali zao. Siku moja haki itapatikana na watanzania tutarudi kuishi kwa amani tukijua sote tu sawa mbele za sheria.

Mungu Ibariki Tanzania.

ukabila, udini, ukanda na sasa ugaidi wa chadema ni kifo kwa ccm 2015

Udini, ukabila, ukanda, na sasa ugaidi ni propaganda ambazo zimetawala kwenye vichwa vya wanaccm dhidi ya chadema na zimekuwa zikitukera sana wanachama, wafuasi na wapenzi wa chadema huku ikiwa ni shangwe na furaha kwa ccm wakiamini kuwa chama hichi kitakufa hivi karibu kutokana na propaganda hizo

Nianze kwa kusema tu kwamba mchimba kaburi huingia mwenyewe kabla ya marehemu kuzikwa.Hivyo basi mchimba kaburi hulijua vizuri joto, mazingira na dhahama japo kidogo ya kaburi.Nianze kuzifafanua hizi propaganda za udini, ukabila, ukanda na ugaidi na ni jinsi gani zitaipeleka ccm kuzimu katika uchaguzi ujao wa mwaka 2015

udini
Moja. Kama chadema ni chama cha udini yaani chama cha wakristo basi tunaomba wakristo wote warudi kwenye chama chao na wakipigie kura chama chao kwa misingi ya dini zao. Na kwa maana hiyo mwaka 2015 wakristo wote wakipigie kura chadema.watu hao kama wakina Pinda, Job ndugai, Mkapa, Malecela,Membe,anna makinda na wakristo wengineo

Pili. Kwasababu ndani ya chadema kuna waislamu safi kama Zitto kabwe, Prof. Safari, Mh Arfi, Mh Halima na wengine basi tunaomba waislamu wote wanaowasupport hawa makamanda wawapigie kura na kuuaminisha umma kuwa chadema siyo chama cha udini ndiyo maana kuna waislamu safi ndani ya chama. Hivyo basi mwaka 2015 kuna kundi kubwa la waislamu wanaokisupport chadema na hawaamini hii propaganda za udini watakipigia kura chadema

ukabila
Moja. Kama chadema ni chama cha kikabila basi tunaomba wachaga wote warudi kwenye chama chao na kukipigia kura chadema mwaka 2015 kwa misingi ya kabila lao. Watu hao kama Sumaye,Mama anna mkapa, Mrema na wachaga wengineo

Pili. Kwasababu kuna makabila kama wasukuma ambao wana wabunge wengi kuliko hata hao wachaga. Basi wasukuma, waha, wahehe, wafipa, wanyiramba na makabila mengine yenye wabunge wa chadema yaikomoe ccm kwa kuichagua chadema mwaka 2015 na kuionesha ccm kuwa chadema siyo chama cha kikabila ndiyo maana makabila mengine yana wabunge wengi kuliko hao wachaga

ukanda
Moja. Kama chadema ni chama cha kikanda basi tunaomba kanda ya kaskazini yote yaani Arusha, kilimanjaro mi mikoa mingine ya kanda ya kaskazini warudi kwenye chama chao na kukipigia kura chadema mwaka 2015 kwa kufuata misingi ya kanda zao

Pili. Kwasababu kuna kanda ambazo ni ngome ya chadema na haziamini kuwa chadema ni chama cha kikanda hivyo basi kanda ya ziwa yaani mwanza na shinyanga zenye wabunge wengi wa chadema, kanda ya kusini na kanda nyingine ziikomoe ccm kwa kuionesha kuwa kanda zao ndiyo zenye wabunge wengi kuliko hata hiyo kanda ya kaskazini hivyo basi chadema siyo chama cha kikanda

ugaidi
Moja. Kama chadema ni chama cha magaidi basi tunawaomba magaidi wote wakiwemo wale wa usal.... na watekaji wote warudi kwenye chama chao na kukipigia kura chadema mwaka 2015 kwa misingi ya kuwa ni chama cha ugaidi

Pili. Kwasababu kuna watanzania wengi wasioamini kuwa chadema ni chama cha kigaidi. Hivyo basi watanzania wote tusioamini kuwa chadema ni chama cha magaidi wapige kura kuichagua chadema mwaka 2015 na kutuma salamu kuwa wanaokiita chadema ni chama cha magaidi wao ndiyo magaidi ndiyo maana wanawateka wapenzi wa haki na wanaharakati wanaopinga uonevu na dhuluma ndani ya taifa hili

hitimisho
Kwa idadi hii ya wapiga kura wa chadema. Chadema itashinda kwa zaidi ya asilimia 70. Lakini hoja ya msingi hapa ni kwa propaganda hizi za udini, ukabila, ukanda na ugaidi je zinaingia akilini. Je kama tuliyempa madaraka anakuwa muongo wa kuzushia watu mambo ya mabaya je yeye atakuwa salama. Je ni kwanini anazusha mambo hayo ukizingatia kuwa yeye amekaa madarakani miaka mingi?
Basi hizo ndiyo sababu zitakazoiua ccm kutokana na propaganda za udini,ukabila,ukanda na ugaidi inayozushiwa wa chadema

Mohamed ally aliwahi kusema ukiona watu wanakusemasema sana ujue wanakuogopa na ni changamoto zinazoashilia upo karibu kufanikiwa
baada ya miaka kupita Mohamed ally alifanikiwa na kuwa the greatest boxer in the world

NAOMBA NIWASILISHE WADAU

Hakika CCM Haitavuka 2015

Mara zote nimependa kutokuwa na siasa za kishabiki, tangu uchaguzi wa mwaka 2010 umarufu wa chama hiki kikongwe ulianza kuporomoka japo haikuwa kwa kasi kubwa, lakini kuanzia mwaka 2013 kasi ya kuporomoka imekuwa bayana, katika historia ya chama hiki sikuwahi kusikia eti kimeshindwa kusimamisha mgombea katika chaguzi ndogo mfano za vitongoji, vijiji na kata. Lakini hayo mambo kwa chama hicho ni kawaida tu kukosa wagombea wa kusimamisha

Ipo mifano mingi ambayo ccm kwa miaka ya hivi karibuni baadhi ya maeneo katika chaguzi ndogo hawasimamishi wagombea, huko ni kuporomoka, na hii inamanisha kwamba katika baadhi ya maeneo hakikubaliki kabisa

Dalili nyingine ya kuporomoka kwa ccm ni hali inayoendelea sasa, ccm imeamua kutumia dola zaidi kuthibiti upinzani badala ya kujenga hoja au kuelezea nini walichokifanya kutekeleza ilani yao. Inashangaza sana kusikia kiongozi wa ccm na msomi kabisa Bwana Mwigulu nchemba anaongoza siasa chafu za matusi, uongo na mipango michafu ili kudhibiti upizani huko nako ni kuporomoka, wanajua fika wasipofanya hivyo hawezi kuvuka 2015

Suala la katiba ni la wananchi wote wa Tanzania , lakini kwa ccm limeonyesha kuwachanganya zaidi, mimi najiuliza kwa nini kuchanganyikiwa kote huko ? Rasimu iliyotolewa inaonekana kuwa ndio hasa watanzania walio wengi walikuwa wakiitaka kwa muda mrefu, sasa imekuja hawa ccm wanachanganyikiwa tena , binafsi sielewi kwa nini wamechanganyikiwa kiasi hiki, wanamshambulia mzee WARIOBA, wakumbuke wajumbe wa tume ile ni zaidi ya WARIOBA
wamo majaji wengi , wanasheria pia na watu wengine wenye weledi wa kutosha.

Hivi tunategemea mapendekezo ya wanaccm wakupandikizwa kwenye mabaraza yakatoa mapendekezo sahihi tunayoyahitaji ?

Wanakubali wanakataa ukweli ni kwamba ccm imeporomoka na imekosa mvuto kwa watanzania, wanao muda wa kujitafakari na kuangalia ni wapi walipojikwaa, hilo linaweza likawasaidia, naiona ccm 2015, ikiwa nyuma ya vyama vingi vya upinzani, sioni tena kama inaweza ikaongoza nchi hii endapo haitajirekebisha

Awali ya yote nishukuru JF kunipokea jamvini.

Kwa muda nimekuwa nafuatilia siasa za CCM, na sasa nimeamini kuwa CCM kama chama cha siasa, ilishakufa miaka takribani kumi iliyopita na sasa ni masalia yanayomalizikia.

CCM imekuwa kama genge la watu wenye malengo fulani huku wakitumia jukwaa la siasa kufanikisha mambo yao.
Siasa anazofanya Mwigulu zingefanyika kabla ya facebook na mchina kutengeneza kila simu na facebook

Kwa speed ya Mwigulu, CCM haichukui miaka miwili unless abadilishe kabisa strategy zake (Siasa za matusi, uzushi,Kumwaga damu za watu kwa lengo fulani, kuwatishia wananchi kama wewe ndo wa milele, unrealistic debates, , siasa za kueneza chuki, udini, kuvuruga amani yetu hivi hivi mbele ya watu wa usalama na badae kusema CHADEMA ndo wanavuruga amani!!!!!!!.

Mimi naona kwa bali Mwigulu, Nape, Kinana, Serikali, na Vyombo vya ulinzi na usalama, wote kwapamoja na kwa speed kubwa wanapeleka katiba na makabrasha ya CCM makumbusho ya taifa na maktaba ya taifa.

Mimi nikiangalia kwa mbali naona CCM imebakia makumbusho na maktaba ya taifa!. Let us wait and see the very death of CCM 2014-2015,June.

Ushauri:CCM inauliwa na viongozi wake. Kupona kwake,lazima wachague moja kati ya biashara safi na siasa au biashara chafu bila siasa.

Ili chama kiweze kuongoza dola kwa ufanisi; vinahitajika vitu viwili vikubwa.

(i) Kukalia ofisi (kushika dola) (ii) kukubalika na wananchi.

Kuhusu kukalia Ofisi; chama kinaweza kuwa madarakani iwe kwa kuchaguliwa au kwa njia yeyote ila kikawa hakikubaliki kwa wananchi walio wengi wakati huo kikiwa madarakani kwa sababu mbalimbali. Katika mazingira hayo ni vigumu sana kwa chama hicho kuongoza dola .Rejea kesi ya Muslim Brother hood ya Misri.

Kuhusu kukubalika na wananchi; Chama chochote kinapokuwa madarakani , ni lazma kitafute mbinu ya kukifanya kikubalike na wananchi ili kiendelee kuwepo.Njia kubwa zinazotumika huwa ni mbili;



(I) Chama kinaweza kujitahidi kutekeleza ilani na majukumu yake mengine na wananchi wanapoona jitihada hizo ; moja kwa moja hukikubali chama bila kushinikizwa na mtu.

(II) Kutumia propaganda.

Tukianza na mbinu ya kwanza; Tunaona wazi kwamba CCM imeshindwa kutekeleza majukumu yake ya kuisimamia serikali kufanya mambo yenye tija kwa wananchi. Kushindwa huko kunasababishwa na mambo mbalimbali miongoni ikiwa ni pamoja na kushindwa kabisa kufanya siasa za kisayansi na kuwa na migongano ya kimaslahi miongoni mwa wana CCM wenyewe. Kwa mfano mdogo tu; Tarehe 27/08/2013, (ndani ya bunge) Mh. Israel Natse (mbunge CHADEMA) alitaka "Serikali itoe kauli ni kwa nini Rais na miongoni mwa viongozi wa nchi hii wanasema wana orodha ya wafanyabiashara ya madawa ya kulevya lakini hawawataji?". Katika kujibu hoja hiyo kwa niaba ya serikali; Waziri Lukuvi alisema "Tukiamua kuwataja; wengi wenu hapa bungeni mtatajwa". Hii ni dhahiri kwamba CCM na serikali yake haiwezi tena kuvuta utashi wa wananchi kuikubali kwa kutenda mambo yanayotamaniwa na wananchi kwa sababu ya migongano ya kimaslahi ndani ya viongozi wa ccm wenyewe kwa wenyewe. Katika mazingira kama hayo CCM hulazimika kuwekeza nguvu kubwa zaidi katika propaganda ili kuwafanya wananchi waikubali.

Tukija kwenye Propoganda; Propaganda ni taarifa, mawazo, itikadi au jitihada maaluum zinazofanyika ili kuathiri fikra, hisia na hata tabia ya umma kwa manufaa ya mdhamini wa propaganda yenyewe. Propaganda zinaweza kuwa za aina kuu mbili .

(i) Propaganda safi; Inayolenga kuupa umma matumaini ya kuvutia kama wakikiunga mkono chama chenye dola.

(ii) Propaganda chafu; Hizi kwa kiwango kikubwa hulenga kuutisha umma .Hapa umma hujazwa hofu nyingi kwamba kama wakionesha kutokukubali chama chenye dola basi wanaweza kudhuriwa vibaya.

Propaganda safi mara nyingi hutumiwa na huleta ufanisi wakati ambapo chama tawala hakijachukiwa sana na kupoteza imani kabisa kwa umma. Kwa Mfano CCM; Walitumia propaganda safi kama ifuatavyo na kujifanikiwa kuwavuta watu wengi kipindi cha nyuma.
Mfano;Walianza na " Ari mpya kasi mpya na nguvu mpyaa!" Wakavuta watu wakawaamini hata hivyo matarajio ya umma yakawa tofauti. Wakabadili wakaja na "Kasi zaidi, ari zaidi na nguvu zaidi", safari hii matokeo yakawa mabaya zaidi na uungwaji mkono kutoka kwa umma nao ukapungua. Wakaja na "Maisha bora kwa kila mtanzania!". Nayo ikawa kinyume kabisa. Wakaja na "Idumu CCM mpya!" Upya ambao haukuonekana mpaka leo. Katika mazingira hayo ilikuwa ni vigumu sana kwa CCM kupata propaganda nyengine chanya (safi). Basi wakachagua kuzama kwenye propaganda chafu.

Maurice Tugwell Kwenye kitabu chake "Terrorism and Propaganda" (2010), anasema; inapotokea chama tawala kimekosa kukubalika na upinzani unapata uungwaji mkono mkubwa; basi mbinu inayoweza kutumika ni kutumia propaganda ya kuwatisha watu ili waunge mkono chama tawala/utawala wowote kwa sababu ya woga. Maurice anasema mara nyingi njia ya kuwahusisha wapinzani na ugaidi hutumika. Kulifanikisha hilo, Mdhamini wa propaganda huweza kuua watu wasiokuwa na hatia na kisha akawasingizia wapinzani wake. Lengo linakuwa ni kutengeneza hali ya woga katika jamii kwa ujumla wake.

Ni sahihi kujiaminisha kwamba matokeo ya kudhuru yenye muelekeo wa kisiasa nchini yamefanywa na CCM kwa sababu tajwa hapo juu.Hii ni kwa sababu ; licha ya kwamba katika matukio yote , Waliokuwa wamepelekwa mahakamani ni wapinzani, wapinzani walishinda kisheria.Sasa ikiwa wapinzani walishinda kisheria, na wakati huo huo matukio ya kudhuru kwa lengo la kuutisha umma yalifanyika ni sahihi kusema waliokuwa wameyafanya ni CCM , nawalifanya kama sehemu ya propaganda ( propaganda chafu baada ya kukwama kwenye propaganda safi).

Kwenye kikao cha CC ya CCM Kilichomalizika 26/08/2013, CCM wanasema wamekubaliana kufanya mabadiliko makubwa ndani ya chama; mabadiliko ambayo safari hii hawakuyataja. Nina uhakika CCM wenyewe hawana uhakika kwamba ni mabadiliko gani wanataka kuyafanya. Kadhalika hakuna mbinu nyengine yeyote ya kisayansi iliyobakia ambayo inaweza kuisaidia CCM kukubalika tena kwa umma.Katika hili naamini wote tutakubaliana. Kwa sababu hiyo basi tutarajie kuona CCM wakiendelea kutia aibu kwenye hii miaka miwili iliyobakia.

Kwa hali ilivyo kwa sasa katka siasa za tanzania,ni wazi kuwa ccm aka chama cha magamba,aka chama cha majambaz, aka chama cha mafisadi,aka chama cha mauaji,aka chukua chako mapema nk.

Viashiria hvo ni mengi ikiwemo haya yafuatayo:

1.kila kesi muhimu wanayowachongea chama kilichopo ndan ya mioyo ya watanzania yaan chadema, wanashindwa vibaya mahakaman.mfano mojawapo ni ya leo ambapo lisu kawashinda tena magamba,huku wakili akiachwa mwenyew bila hata mfuasi wa ccm au kiongoz wao wa rufan kinana,,,ccm inakufa.

Pili,kesi za ugaid zote cdm kushinda,ni dalili kuwa chama cha wazee ccm kinakufa.

2.kitendo cha kulazimisha muswada wa sheria ya mabadiliko ya rasim ya katiba kupita bungen bila nchi ya zanzibar kuhusishwa ni uoga wa kutoka madarakani.

3.kitendo cha rais wa nchi na mwenyekit wa ccm taifa Jakaya mrisho kikwete akiwa mwanza na shinyanga kusema kuwa '' ccm itashindwa vibaya katka uchaguz wa 2015,na kuwa viongoz wa ccm wengi ni wavivu kufanya kzi,ni mojawapo ya kusambaratika kwa chama hiki cha wala kodi za watanzania.

4.kitendo cha waziri mkuu pinda kutamka hadharan bungen kuwa serikali imechoka na kuwa raia wapigwe,ni dalili tosha kuwa ccm chama cha wala unga kinakufa mapema.

5.kitendo cha ccm na serikali yake kushindwa kudhibiti au kutoa adhabu kali kwa wauza au wasafirisha madawa za kulevya na kuwa tanzania tunayoipenda,imechafuliwa kwa sakata la madawa ya kulevya,ni dalili tosha kuwa ccm chama cha maaramia kimebaki fuvu tu.

6.kitendo cha viongoz wao kuporomosha matusi akiwemo mwigulu,serukamba na mukulo aliewah kusema kuwa,kila mtanzania atakula kwa urefu wa kamba yake,na kuwa pesa zetu wao wanakula kwa kamba fupi kwa kuwa wameficha uswis ili zisiishe haraka,ni dalili tosha kuwa ccm kimekufa kimebaki alama ya jembe na nyundo tu kichwani.

7.kitendo cha wazir wa madini na gesi muhongo kuwaambia watanzania kuwa '' watanzania hawana ujuzi na uwezo wwote wa kuwekeza kwenye gesi labda kwenye juice'' ni matusi kwa watanzania na dalili za chama cha wenye nacho kufa.

8.kitendo cha kufukuza madiwan na kurudia matapishi tena,ikiwa ni uchafu ambao hata mnyama fulani akitapika hali matapishi yake,ni dalili ya chukua changu mapema kufa.

9.kitendo cha kupigwa 4-0 arusha mjini ni dalili tosha ya chama cha matapeli kufa.

10.kitendo cha serikali yake kuwa na bajeti ya robo tatu asilimia kuwa tegemezi wahisani na kuwa pombe ndo kipaombele chako na bado watanzania maskini wanakatwa kodi za simu ni dalili tosha kuwa chama cha majanga ccm kinakufa.

Nb: unga mkono hoja,na kama unapinga hoja toa uthibitisho mathubuti...

Nilikuwa katika ziara ya kikazi kwa maeneo ya Arusha, Babati, Singida na Dodoma. Tulipofika eneo moja la Tanga linaitwa komkonga tukasimama kwa ajili ya kujisaidia na kupata maji, nikiwa hapo nikaona bendera tatu na zote mpya, moja ya CCM, nyingine CUF na ya Tatu Chadema, Nikauliza wale wenyeji kuwa hapo kwenu kuna Vyama 3 tu vingine havisikikii, akanijibu akaniambia vipo vingine lkn kwa sasa hakuna chama kina wafuasi wengi kama Chadema, yaani kimekuwa na watu wengi sana, na watu hao wanaokiunga mkono wanatoka CCM na CUF, wakanihakikishia kama hakutakuwa na Uwizi CCM 2015 wanaondoka. Sikuridhika na majibu hayo nikaenda kwa mtu mwingine.. yeye akaniambia kuwa ni mfuasi wa CCM lkini Chadema ka sasa kina nguvu sana kwao.

Nikaendelea na safari yangu Arusha, Kule nadhani kila mahali ni chadema..kwani nilikwenda dukani kununua mahitaji unapotoa hela wanakwambia asante kamanda. Yaani kamanda ndiyo lugha ya Arusha.

Babati nilikutana na afande mmoja ambaye ni rafiki yangu nikajaribu kumuulizia ni chama gani chenye nguvu hapo kwao.. akaniambia brother bila kukuficha chadema kina nguvu sana, sikuridhika nikauliza baadhi ya raia wakaniambia vivyo hivyo.

Nilipokuwa singida watu wa kule wakaniambia Lissu amewafungua macho kwa mambo mengi sana hivyo hakuna kama Chadema.

Dodoma vijana wengi nao wanasema hivyo hivyo lkn wengine wa CCM wakaniambia kwa sasa inabidi watafute mbinu mmbadala kuidhibiti chadema bila hivyo CCM hawana chao.

Sasa kwa utafiti huo mdogo katika maeneo hayo ndiyo maana nasema CCM 2015 wataondoka kupitia sanduku la kura.

Salaam makamanda!

Wingi wa maneno sio ukweli wa mambo. Kwa kifupi CCM ina hali mbali sana kwenye siasa za hapa Tanzania, huo ni ukweli ulio wazi. Wenye upeo wa kutosha wameshang'amua hilo muda mrefu sana, wanasema its just a matter of time. Mabadiliko wananchi wanayataka iwe kupitia chadema ama kupitia njia yeyote ile lakini ccm bye bye hawataki kuisikia tena. HIKI NI KIZAZI KIPYA WANATAKA KUSIMIKA UTAWALA WAO IWE KUPITIA CHADEMA AMA CHAMA CHOCHOTE KILE, LAKINI LAZIMA WASIMIKE UTAWALA WAO. Fuatilia historia ya vyama vingine kwenye mataifa mengine vyenye hadhi ya CCM utanielewa kwa urahisi zaidi. Tazama haya machache:-

1.Viongozi njaa wa chadema wanatangaza kujiuzulu lakini hawatangazi wapi wanahamia, tofauti na miaka ya zamani kiongozi akihama anatangaza amehamia wapi asap

2.Zitto, Mkumbo, Samson wamesimamishwa nyadhifa zao lakini hawataki kuondoka, wanapambana wabaki mle!

3.Mtela, Habib, Juliana, Kisandu wamefukuzwa lakini bado wanang'ang'ania chadema; bado wana mapenzi ya moyoni na chadema; japo baadhi wapo ccm lakini ni kwa sababu ya dhiki tu si kwa kupenda. Mioyo yao ipo chadema

4.Beneficiaries wakubwa wa mfumo wa ccm (wenye upeo mkubwa wa kuona jinsi upepo wa mabadiliko unavyovuma nchini) hawajitokezi waziwazi kuiponda chadema badala yake wanawatumia akina Mwigulu Nchemba (aka aibu katibu mkuu wa ccm na sio naibu katibu mkuu wa ccm) na akina Nape Nnauye, wao wanafanya mambo yao kimya kimya kwa kuelewa kuwa ccm days are just numbered!

Lumumba FC B7 project wanatumika tu na wenye upeo kujaribu kuchelewesha siku za CCM kuondoka lakini mwisho wa siku ccm wanapoteza huu mchezo, huu sio utabiri ni hali halisi wenye upeo wa kutosha wananielewa! Lumumba FC b7 project hawapendi kutumika lakini dhiki iliyoletwa na ccm ndio inayowafanya kukubali kutumika na si vinginevyo! Unajua dhiki ikizidi unakuwa nusu msukule akili inastak kufikiri, nadhani naeleweka! Usidhani Simiyu Yetu na wenzake mfano chamvida wanafanya wanachojua la hasha tatizo ni dhiki kuu iliyoletwa na ccm, wamepumbazika ila soon watarejewa na ufahamu wao halisi!

5.Kwa ujumla chuki ni kubwa sana kwa ccm toka kwa watu wa kawaida na wasio wa kawaida

NB:Wingi wa maneno sio ukweli wa mambo, kwa kifupi ccm hours are numbered! Naomba tuishie hapo!

Wenu katika ukombozi! TeamChadema
 
Mojawapo ya hadithi za kusisimua na kusikitisha katika meli iliyovuma enzi hizo na kupoteza maisha ya watu wengiNi kwamba baada ya nahodha kuona meli hiyo inazama aliwatangazia abiria kuhusu hatari hiyo ili wachukue tahadharikujiokoa na walitangaziwa na kusikia kupitia vipaza sauti na speaker zilizokuwemo melini.Abiria walisikia tangazo la hatari lkn kwa kuwa meli hiyo ilikuwa na kila aina ya starehe na burudani,ikiwa ni pamoja nana kasino viwanja vya michezo,bar nk walipuuza wakileweshwa na anasa za melini,walipuuza tangazo hilo lilipotua masikioni mwao na wengine wakadhani NI MOJAWAPO YA VIKOROMBWEZO VYA NAHODHA WA MELI!!!!Hakuna aliyedhani wala kuota kuwa meli hiyo ingekuja kuzama na kupotea kabisa ktk historia ya ulimwengu na ukweli ni kwamba MELI YA TITANIC ILIZAMA NA MAMIA YA WATU WALIPOTEZA MAISHA.Nimeilinganisha meli hii ya zamani na chama kikongwe CCM,kelele za mwangwi zinasikika kila kona zikitahadharisha anguko Kuu lake,lkn abiria(wanachama)wametia pamba masikoni wengine wakiwa wameleweshwa na anasa (ufisadi)ndani ya ccm.Wengine wakiona km kelele za wpinzani wao lkn ukweli ni kwamba si mbali chama hiki kitaanguka,dalli zote zinaonesha si mbali,ufisadi,makundi ,rushwa ,udhaifu nk ni dalili toshaBado kitambo kidogo.
 
Mmoja wetu humu jukwani aliwahi kuandiks kuwa " mchwa anapojaribia kufa huota mbawa". Hii ni kuonesha mbawa zishaota sasa tusubiri yatimie.
 
Wanaopenda kushuhudia CCM ikisambaratika ni wengi kuliko wanaoiombea mema. Je wimbi la mabadiliko litaiacha CCM madarakani kwa muongo mmoja au miwili ijayo? Jibu wanalo viongozi wa CCM. Wanachama wa CCM wamegawanyika vipande vipande, wengine wanasema potelea pote, maana wanajihisi kutengwa na chama chao, huku wakishuhudia nguvu ya pesa katika chaguzi zote za ndani ya chama. Jambo lililo wazi ni kwamba CCM inapita katika kipindi kigumu haijawahi kutokea, na kama watavuka salama basi ni kwa kudra za Mwenyezi Mungu.

Binafsi siwaombei mabaya, lakini muda wa kujirekebisha unazidi kuyoyoma. Mdharau mwiba huota matende, viongozi wa CCM amkeni kabla jua halijakucha. Huu ni mchango huru wa mawazo, unaweza kuwa na manufaa au kupuuzwa, yote sawa.
 
Dalili nyingine ni mparaganyiko wa wazi miongoni mwa makada waandamizi na rubani wa chama kushindwa kusimamia miiko ya chama ni ishara tosha ya anguko la chama hicho.

Watu wanaongea kwa ndimi mbili mbili,hii ni hatari kubwa
Wenye pesa wanaabudiwa,nivyema waadilifu wachache watakaosikia sauti ya nahodha wakajisalimisha kwa kuondoka mapema.
 
CCM ni sawa na Kabuli kwa nje zuri ila kwa ndani limejaa mifupa na harfu mbaya

Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
Wakati huo huo wajiandae woote waliofisadi hii nchi kwenda segerea na wale wezi wa kuku na waliosingiziwa kesi akiwemo NGUZA wakiachiwa huru kwa furaha siku hiyo haiko mbali yaja!!
 
CCM yafaa ikae kwanza kwenye upinzani nadhani ikirudi itafanya vema zaidi
 
Wanaopenda kushuhudia CCM ikisambaratika ni wengi kuliko wanaoiombea mema. Je wimbi la mabadiliko litaiacha CCM madarakani kwa muongo mmoja au miwili ijayo? Jibu wanalo viongozi wa CCM. Wanachama wa CCM wamegawanyika vipande vipande, wengine wanasema potelea pote, maana wanajihisi kutengwa na chama chao, huku wakishuhudia nguvu ya pesa katika chaguzi zote za ndani ya chama. Jambo lililo wazi ni kwamba CCM inapita katika kipindi kigumu haijawahi kutokea, na kama watavuka salama basi ni kwa kudra za Mwenyezi Mungu.

Binafsi siwaombei mabaya, lakini muda wa kujirekebisha unazidi kuyoyoma. Mdharau mwiba huota matende, viongozi wa CCM amkeni kabla jua halijakucha. Huu ni mchango huru wa mawazo, unaweza kuwa na manufaa au kupuuzwa, yote sawa.


Can you boy wake up a dead? Dont think about it.
 
Anguko la CCM limefikia 40%...teh teh teh 2015 wanaanguka kifo cha mende! miguu juu!
 
Kama viongozi wameonywa mara zote na hawakusikia,siku mbaya inayo kuja hawatakuwa na wakumlilia zaidi ya nafsi zao.
 
One million dollar question; is CHADEMA ready for the take over? Baada ya anguko kuu la CCM, kama kweli litatokea kama inavyotazamiwa na wengi, CHADEMA peke yao wataweza? Au waungane na CUF ili kuondoa dhana ya udini na ukanda.

Lipumba na Mbowe watafakari kwa pamoja jinsi ya kuchukua hatamu za CCM kwa mustakabali wa maendeleo ya Taifa letu.

Ni wazo huru, linaweza likawa la manufaa au likapuuzwa, yote sawa.
 
U-mimi, majungu na damu ya ubaguzi yote iliopata mimba na sasa kuzaa uchakachuaji sasa yaua CCM tokakila kona ya nchi.
 
Hilo la nne....wazee wa busara ni pamoja na Sumaye? Okay angalau nimejua leo
 
Kadri siku zinavykwenda naona dalili zote za CCM kuanguka. Hakuna atakayeweza kuiokoa chama hiki kongwe. Naona anguko hilo litatokea ndani ya miaka kumi na tano (15). Watakaokingusha CCM ni wana CCM wenyewe, si vyama vya upinzani.

Zifuatazo ni dalili ya kuanguka kwa CCM
1. Upendo kati ya wanachama umekwisha, ni ugomvi usiokwisha ( Sitta camp Vs Rostam camp)

2. Fedha ni kipaumbele siyo Sera au hoja.

3. Wasemaji wa chama ni wapayukaji ( makamba, Hiza Tambwe, Sofia simba)

4. Wazee wenye busara wamesusa chama ( Warioba, Salim, Butiku, Sumaye)

5. Familia ya viongozi wamekiteka chama ( Makamba's, JK's, )

6. Kampeni zimebadilika kuwa concert ( wanamuziki kibao)

7. Kununua wapinzani

8. Kukataa midahalo ( mchakato majimboni- TBC)

9. Ahadi nyingi wakati huu wakati za mwaka 2005 hazijatekelezwa ( Mikopo ya wanafunzi maisha bora kwa kila mtz n.k)

10. Chama kujadili issue binafsi zaidi badala ya maslahi ya wananchi.

CCM kwa sasa ina uwoga sana kuliko cha chama chochote hapa nchini. Wanaelewa wanakoelekea.

Tumekusoma mbuyi twite
 
Na nukuu baba wataifa alisema watanzani wakikosa mambo ambayo wanayataka ndani ya ccm watayatafuta nje ya ccm,baadhi wamesha anza kuyatafuta nje,wamesha gundua kumbe hii nchi bila magamba inawezekana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom